Mc wa dar na lugha mbovu na mambo ya hovyo

Mc wa dar na lugha mbovu na mambo ya hovyo

azonto

Member
Joined
Aug 9, 2012
Posts
5
Reaction score
0
Nasikitishwa na watu waliokimbilia fani bila kujua maudhui yake,wasiopenda kujifunza maudhui ya kazi yenyewe kwa kusoma ama kujifunza toka kwa wateja wao wastaarabu wanowapa kazi mbalimbali waziongoze ama kusimamia.

Hivi majuzi nimesikia mc akiandaa watu kupokea mwili /jeneza la marehemu akitamka kwa msisitizo kabisa ...... Tujiandae kupokea dead body !!!!!!!! hivi kuna haja gani kuchanganya kiswahili na lugha usioijua (english) wakati unazungumza na jumuia inayojua kiswahili kwa ufasaha na pia kwa baadhi pia wanajua kiingereza fasaha??????

Mbwembwe za nini hapa.

Upuuzi mwingine ni pale mc huyu huko makaburini katika ibada ya mazishi alipotoa wasifu wa mfiwa ( auto mechanic ) kuwa eti huyu ni fundi wa magari si ya watu wote bali ya sisi (yeye mc na anaowajua limbukeni wenzake) tuliojaliwa kuwa na magari!!!!!!!!!!

sehemu ya umati wa waombolezaji waliguna na kusikitishwa na upuuzi huu??????.

Je saa km chama tunachukua hatua gani kukomesha tabia hizi za mbwembwe

yatupasa kukua kimwili na kifikra pia kusoma alama za nyakati na mazingira

saa daima
 
kiukweli inaudhi na kuboa sana mkuu!!
 
kiukweli inaudhi na kuboa sana mkuu!!

Yaani hata maudhui ya tukio hawajui yanakuwaje!!
 
Mtaje ili akirudi huku tumsake tumseme live maana yawezekana huyo mtu si mwanachama wa JF na hivyo si rahisi kufikiwa na ujumbe wako kwake ajirekebishe
 
Why msiba uwe na mc?
The Boss unashangaa msiba kuwa na Mc?Siku hizi pakitokea msiba vikao bar,na michango kama ya harusi,tena meseji za kukualika kwenye kikao!Na kamati zinaundwa na vikundi mbalimbali mpaka vya kuomboleza(waliaji),vinaalikwa!!
 
Last edited by a moderator:
Inaudhi zaidi pale unapoweka MC kwenye msiba!! Mbwembwe hizo za nini?
 
Back
Top Bottom