Mbwana Samatta kumuona Lissu?

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,724
Reaction score
165,132
Tundu Lissu anaenda kulazwa Ubelgiji nchi ambayo mwanasoka wa kimataifa wa kitanzania, Mbwana Samatta anacheza soka(mpira wa muguu).

Swali ni je,mwanasoka huyu maarufu atakwenda kumuona hospitalini mwanasiasa huyu maarufu na ambae ni mtanzania mwenzake?

Iwapo atakwenda kumuona na wakapiga picha ya pamoja, unadhani picha hiyo itasambaa kwa kiasi gani?

Wacha tusubiri.
 
Kama hata mzee Mwinyi na mama Samia walikwenda kumjulia hali Lisu kuna ubaya gani Samatta kwenda kumjulia hali huyo Lisu wako? Acha upuuzi.
 
Kwani kuna ulazima upi wa Samatta kumuona Lisu?

Wewe upo Dar ni lini umekwenda Muhimbili kutembelea wagonjwa?

Kwanza msipende sana Lisu kutembelewa na watu ni hatari sana, zipo sumu za aina nyingi na ndio maana viongozi wengi huwa wanauguzwa kwa siri na baadaye updates za afya yake zinatolewa kwa public na siyo kugeuza hospitali kama sokoni.
 
Wewe hakika dish limeyumba....
Kwani watu hawana shughuli ya kufanya zaidi ya kumtembelea Lissu?
 
Mwacheni Samatta acheze mpira mmeanza kumhusisha na siasa zenu za Bavicha.

Hata kama ataenda sawa tu lakini sio kuchukulia pointi za kisiasa.
 
Nazan Kuna Watu Uelewa Wao Mfinyu Sana Yan Mtu Akienda Kumuona Mgonjwa Anachanganya Mpira Na Siasa Hapa Nawakatalia Mbona Baraka Da Prince Alienda Kumuona Ina Mana Na Yeye Anachanganya Mziki Na Siasa Hilo Napinga Ngoja Nimtag [HASHTAG]#georgeweah[/HASHTAG] Atusaidie Hili
 
Ukikuaa utaacha
 
siasa na michezo wapi na wapi ???? acheni umburura
 
Chadema mnaelekea ukingoni......muda si mrefu mtasshaulika kabisa na dalili ni mada kama hizi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…