Mshume Kiyate
JF-Expert Member
- Feb 27, 2011
- 6,766
- 894
Ikiwa leo ni kilele cha maadhimisho ya wiki ya maji, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (Chadema) ameitaka serikali kutumia siku hiyo kutoa taarifa za kina kuhusu utatuzi wa kero ya maji kwa wananchi wa Mkoa wa Dar es salaam. Mnyika alisema Rais Jakaya kikwete, atumie siku hiyo kutoa kauli kuhusu utekelezaji wa ahadi mbalimbali za kuboresha huduma ya maji na kwamba kinyume chake itaunganishwa nguvu ya umma katika kuchukuwa hatua za ziada kukabiliana na kero husika. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Mnyika ilieleza kuwa licha ya serikali kutoa ahadi mbalimbali za kuboresha na kutokomeza kero ya maji jijini, lakini zimekuwa hazitekelezwi.
Mwananchi Machi 22 2011
Mwananchi Machi 22 2011