Amedai wabunge toka kwenye majimbo mengine waombe ruhusu ya kuzuru kwenye majimbo mengine kupitia mbunge wa Jimbo husika. Hapa nahisi alikuwa anawasema Lisu na Lema kwamba waombe ruhusa yake kuzuru Tarime! Kwa maelezo yake ni kwamba alikuwa anaomba ushirikiano na Wanatarime kwa kuwa wanaipenda CCM na serikali iliyopo madarakani ila anasikitika kuna wahuni wachache wanatumiwa na vyama vingine kuvuruga mambo huko Tarime; akaongeza pia kuwa Wanatarime wamechoka na hali hii wanataka watulie wafanye kazi za kujiletea maendeleo. Nimkumbushe tu Mh. Nyambari wakati yeye anauza vitabu Lisu alikuwa na Wanatarime kwenya matatizo mbali mbali ya Migodi ya Tarime toka Buhemba na sasa chini ya Barrick. Lisu amejijengea imani kwa Wanatarime na wanamhesabu si kama mtetezi wao bali kama ndugu yao. Taarifa nilizonazo ni kwamba wakati wa msiba wa mama yake Lisu kulikuwa na watu zaidi ya ishirini toka Tarime walioshiriki kwenye msiba huko Singida. Sasa kwa hali hii Lisu asikie kuna maafa yamefanyika Tarime asiende aombe hurusa toka kwa wewe Nyambari??? Joandae Kukabidhi Jimbo maana umewakimbia wananchi wakati wakikuhitaji!!