Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Bakari Shingo ashindwa kuendelea kwenye kinyang'anyiro kwa kushindwa kukidhi kigezo cha lugha ya Kiingereza

Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Bakari Shingo ashindwa kuendelea kwenye kinyang'anyiro kwa kushindwa kukidhi kigezo cha lugha ya Kiingereza

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Bakari Shingo, amejiondoa katika kinyang’anyiro cha kuwania nafasi za uwakilishi wa Tanzania kwenye taasisi muhimu za kimataifa za mabunge baada ya kushindwa kukidhi kigezo cha umahiri wa lugha ya Kiingereza wakati wa mchakato wa uteuzi.

Uchaguzi huo ulifanyika ili kupata wawakilishi wa Tanzania katika Bunge la Afrika (Pan-African Parliament), Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) pamoja na Jukwaa la Mabunge ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu.

Nafasi hizo zilikuwa wazi kufuatia kumalizika kwa muda wa Bunge la 12, hivyo kulazimu kufanyika kwa kura mpya za kuteua wajumbe wapya.

Hata hivyo, Mbunge huyo wa Ukonga alishindwa kuendelea na mchakato wa kuwania nafasi hizo baada ya tathmini ya lugha kuthibitisha kuwa hakukidhi kiwango kinachohitajika cha umahiri wa Kiingereza, ambacho ni sharti muhimu kwa ushiriki katika vikao na shughuli za mabunge hayo ya kimataifa.



 
baada ya kushindwa kukidhi kigezo cha umahiri wa lugha ya Kiingereza wakati wa mchakato wa uteuzi.
Tungependa hii iongezwe kwenye vigezo vya mbunge kupitishwa kua mbunge wa eneo fulani itatusaidia mambo mengi sana kwa dunia inapoelekea sasa Mbunge hata Kingereza kuandika na kuzungumza tu mtihani hii inatupeleka wapi, wapi Mchengerwa ushawahi msikia akibonga ung'eng'e na kile kigugumizi ukamsikiliza kwa makini ukatoka na point 3? Kuna mbunge mwingine wa kuitwa DAB bila kumsahau J Homela vingereza vyao dah naomba unifundishe kunyamaza, where does this shit come from, from shithole country?, tunachagua madushu ambayo hata Kingereza hayajui?
 
Lakini si kushindwa hata kiingereza cha kuombea maji ya kunywa.

Eksichuzi me!
Hicho ndio ambacho watu wengi wanakitumia nasema kile cha kuombea kazi kama hapo jamii ikuelewe utafanya nini huko ndio mtihani maana jamaa ni tamaa tu ndio zimempeleka hapo kwa kitu asichoweza kaona ataweza sasa hawa ndio watunga sheria zetu ambazo zipo kwa kimalkia wao ndio wanazipitisha kama sheria za kodi si mtihani huu unakuta mtu mpaka anatoka Bungeni hajui alipitisha nini akisikia kelele mtaani nae anasema yupo na Wananchi.
 
Hicho ndio ambacho watu wengi wanakitumia nasema kile cha kuombea kazi kama hapo jamii ikuelewe utafanya nini huko ndio mtihani maana jamaa ni tamaa tu ndio zimempeleka hapo kwa kitu asichoweza kaona ataweza sasa hawa ndio watunga sheria zetu ambazo zipo kwa kimalkia wao ndio wanazipitisha kama sheria za kodi si mtihani huu unakuta mtu mpaka anatoka Bungeni hajui alipitisha nini akisikia kelele mtaani nae anasema yupo na Wananchi.
😁eti akisikia kelele mtaani na yeye anasema yupo na wananchi😆
 
Na kinakuwa kigumu zaidi kama mtu hafanyi practice ya mala kwa mala.. unajikuta unabaki na English ya kichwani
FB_IMG_1762413672161.jpg
 
Lakini si kushindwa hata kiingereza cha kuombea maji ya kunywa.

Eksichuzi me!
Tunashangaa lakini nakuhakikishia asilimia 85 ya wabunge level yao ni hii. Kiswahili ni lugha inayotumika kuficha vilaza sana kwa sababu haina jagon za kitaalam. Ingekuwa ni amri yangu ningesema bunge la Tanzania lugha rami iwe kiingereza (angalau kwa muda wa miaka 20) ili kuchja vilaza.
 
Tunashangaa lakini nakuhakikishia asilimia 85 ya wabunge level yao ni hii. Kiswahili ni lugha inayotumika kuficha vilaza sana kwa sababu haina jagon za kitaalam. Ingekuwa ni amri yangu ningesema bunge la Tanzania lugha rami iwe kiingereza (angalau kwa muda wa miaka 20) ili kuchja vilaza.
Hapo unaweza acha vipanga wasiojua kingereza na unaweza pakua vilaza wanaojua kingereza🤔
 
Back
Top Bottom