Mbunge wa dodoma mjini vip?

Mbunge wa dodoma mjini vip?

Joined
Jun 15, 2013
Posts
22
Reaction score
5
Japokuwa Umepata Bahati Jimbo Lako Halina Changamoto Nyingi Kama Lile La Mzee Wa Kusinzia Pale Mjengoni, Kwani Miundombinu Ya Barabara Na Maji Pamoja Na Huduma Za Kijamii Kama Hospital Na Shule Zote Zinajengwa Na Kukurabatiwa Na Serikali Pasipo Na Msukumo Wako, Hii Imekufanya Ukae Kimya Kama Vile Jimbo Halina Matatizo Mengine. Kila Kukicha Kuna Migogoro Baina Ya CDA na wananchi pia matatizo ya ajira kwa vijana yapo ila wewe umekaa ata bungeni kupaza sauti yako amna, umekuwa mtu wa kugonga meza na kujibu ndiyo na muda mwingine uko bize na shule yako ya CITY. utaki ata kuitisha mikutano na wananchi kujadili changamoto zinazolisumbua jimbo. tutaonana mwakani tunakusubiri.
 
amekusikia atafanyia kazi ila waambie wanzako mheshimu mamlaka ya cda
 
Tembelea Makulu utaona vijumba visivyo na mipangilio vinavyoota kama uyoga. Hakuna hata barabara, miundo mbinu ni very poor. Vilabu vya pombe za kienyeji vimeshamiri. Hapo ni Makulu ipo Mjini inaongozwa na Diwani Bilingi wa Chadema. Ni sehemu iliyosahaulika na kutelekezwa na Uongozi wa Mkoa, Wilaya na pia CDA.

Kitongoji kipo kama uwanja wa fisi. Mkuu wa Mkoa analifahamu vema suala hili na hapendi kukwazwa kwa kushamiri kwa hali hii.
 
Tembelea Makulu utaona vijumba visivyo na mipangilio vinavyoota kama uyoga. Hakuna hata barabara, miundo mbinu ni very poor. Vilabu vya pombe za kienyeji vimeshamiri. Hapo ni Makulu ipo Mjini inaongozwa na Diwani Bilingi wa Chadema. Ni sehemu iliyosahaulika na kutelekezwa na Uongozi wa Mkoa, Wilaya na pia CDA.

Kitongoji kipo kama uwanja wa fisi. Mkuu wa Mkoa analifahamu vema suala hili na hapendi kukwazwa kwa kushamiri kwa hali hii.

Napafahamu kaka ila si mbunge wala serikali ya mkoa wote wapo kimya yeye MALOLE(mbunge) anasubiri muda wa uchaguzi akawape pombe na doti za kanga ili wamchugue, namkumbuka wakat akitaka kura alivyokuwa anatembelea vijiweni kwa kuustarabu kuzungumza na vijana juu ya dodoma mpya ila leo anatuona kama mabwege vile, tunamsubiri tu mwakani, watu wanaishi kama mateka kwenye ardhi yao kisa CDA na amekaa kimya tu.
 
Hawa wabunge si wana ofisi zao? Fanya umtembelee zaidi ya umsubiri hadi mwakani!
 
Back
Top Bottom