Mbunge wa Chalinze asifia shule binafsi mkoa wa Pwani matokeo kidato cha 4

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
6,067
10,936
Kikwete.jpeg

Katika hali isiyo ya kawaida, mbunge wa Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete mwenye dhamana ya kusimamia na kupigania maendeleo jimboni kwake ikiwa ni pamoja na kuhakikisha anaibana serikali ili iweke miundombinu mizuri ya shule zetu za serikali almaarufu kama za KATA/KAYUMBA ili ziweze kutoa elimu bora kwa watoto wa masikini, amezisifia shule TATU ZA BINAFSI zilizofanya vizuri kwenye matokeo ya kidato cha nne.

Shule hizo ni 4. MARIANI GIRLS, 5. MARIANI BOYS na 6. ST ALOYSIUS GIRLS. Shule hizi zipo zinamilikiwa na KANISA KATOLIKI ambapo zinatoza ada kubwa sana kiasi kwamba wazazi wengi wa Chalinze na Pwani kwa ujumla hawawezi kusomesha watoto wao pale.

Aloshiba hamjui mwenye njaa. Sidhani kama Ridhiwani anaweza kumpeleka mtoto wake shule yoyote ya kata, masikini watoto wetu hatujui mbele yao.

Kufeli kwa shule za kata ilibidi iwe changamoto kwa mbunge huyo ili ajipange cha kuongea kwenye bunge lililoanza leo.

Ameshindwa kuonesha uzalendo hata kwa shule ya VIPAJI MAALUM Kibaha Boys ambayo inakufa kutokana na sera mbovu ya elimu. Nakumbuka mtoto wa Kikwete wakati huo ni RAIS alipelekwa Kibaha kwa mbwembwe lakini akahamishwa na kupelekwa shule ya mamilioni.

Haya bhana, Juzi Kigwangallah katutusi, leo nawe tumetusiwa sie watoto wa masikini ambao ndio wapiga kura wakubwa.
 
Hta kama ni za private ila zikifanya vizuri kuna ubaya kuzisifia?
Ni sawa na baba yako amsifie mtoto wa jirani kufaulu kisa wewe umefeli, wakati anajua fika hajaweka jitihada zozote kwenye ufaulu wa mtoto wa jirani. Kumbuka huyu ni mbunge.
 
Amekuwa mkweli maana kama wamefanya vizuri asiseme? huyu dogo anaanza kuacha unafiki nimempenda bure tangu issue ya daimond
 
Katika hali isiyo ya kawaida, mbunge wa Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete mwenye dhamana ya kusimamia na kupigania maendeleo jimboni kwake ikiwa ni pamoja na kuhakikisha anaibana serikali ili iweke miundombinu mizuri ya shule zetu za serikali almaarufu kama za KATA/KAYUMBA ili ziweze kutoa elimu bora kwa watoto wa masikini, amezisifia shule TATU ZA BINAFSI zilizofanya vizuri kwenye matokeo ya kidato cha nne.

Shule hizo ni 4. MARIANI GIRLS, 5. MARIANI BOYS na 6. ST ALOYSIUS GIRLS. Shule hizi zipo zinamilikiwa na KANISA KATOLIKI ambapo zinatoza ada kubwa sana kiasi kwamba wazazi wengi wa Chalinze na Pwani kwa ujumla hawawezi kusomesha watoto wao pale.

Aloshiba hamjui mwenye njaa. Sidhani kama Ridhiwani anaweza kumpeleka mtoto wake shule yoyote ya kata, masikini watoto wetu hatujui mbele yao.

Kufeli kwa shule za kata ilibidi iwe changamoto kwa mbunge huyo ili ajipange cha kuongea kwenye bunge lililoanza leo.

Ameshindwa kuonesha uzalendo hata kwa shule ya VIPAJI MAALUM Kibaha Boys ambayo inakufa kutokana na sera mbovu ya elimu. Nakumbuka mtoto wa Kikwete wakati huo ni RAIS alipelekwa Kibaha kwa mbwembwe lakini akahamishwa na kupelekwa shule ya mamilioni.

Haya bhana, Juzi Kigwangallah katutusi, leo nawe tumetusiwa sie watoto wa masikini ambao ndio wapiga kura wakubwa.

Kama wamefanya vizuri kwa nini wasisifiwe wakati wanaosoma pale ni watanzania? Acha ubaguzi wewe.
 
Huu ushabiki mwngne ni njaa sasa na unafiki...neno mwafwa lanini sasa wakat mbunge toka mkoa wa pwani kasifia mkoa wake kwa kuingiza shule top ten,acheni chuki za kitoto!
 
Toa sifa inapostahili. Kusifia ni uungwana,kama wamefanya vizuri kwa nini wasisifiwe.
 
Ni sawa na baba yako amsifie mtoto wa jirani kufaulu kisa wewe umefeli, wakati anajua fika hajaweka jitihada zozote kwenye ufaulu wa mtoto wa jirani. Kumbuka huyu ni mbunge.
Ombara, nimesema time and again kuwa humu JF baadhi ya wachangiaji ni too myopic. Nobody bothers to have a critical analysis of issues! To go beyond the nose! Mbunge huwezi kusifia shule za matajiri wakati 100% ya wananchi unaowawakilisha watoto wao wamefeli....almost all division za mwisho. Lengo si hao matajiri, lengo la ubunge wako ni hawa Kapuku!
Nakubaliana na andiko lako
 
Ni sawa na baba yako amsifie mtoto wa jirani kufaulu kisa wewe umefeli, wakati anajua fika hajaweka jitihada zozote kwenye ufaulu wa mtoto wa jirani. Kumbuka huyu ni mbunge.
Mbunge anawakilisha watu na taasisi zote katika jimbo. Ana haki kuwapongeza wale wanaofanya vizuri katika majukumu yao. Mkoa wa Pwani kuwa na shule 3 bora kati ya shule 10 bora kitaifa ni mfano mzuri na wa kuigwa na shule zingine mkoani Pwani na taifa kwa ujumla. walioshinda ni watanzania na watakuja kuwatumikia watanzania wenzao.. Kitu cha msingi kwa Mh. Mbunge nikuweka wazi kama ana mkakati wa kuboresha elimu kwenye shule za umma katika jimbo lake. Kuwapa shime waliofanya vizuri ni haki na wajibu wa kiongozi ambaye hana ubaguzi kwa wale anaowaongoa
 
Ni sawa na baba yako amsifie mtoto wa jirani kufaulu kisa wewe umefeli, wakati anajua fika hajaweka jitihada zozote kwenye ufaulu wa mtoto wa jirani. Kumbuka huyu ni mbunge.
Kwani unabaya uko wapi hapo kama we bogasi bogasi tu kwa nini asimsifie
 
Ombara, nimesema time and again kuwa humu JF baadhi ya wachangiaji ni too myopic. Nobody bothers to have a critical analysis of issues! To go beyond the nose! Mbunge huwezi kusifia shule za matajiri wakati 100% ya wananchi unaowawakilisha watoto wao wamefeli....almost all division za mwisho. Lengo si hao matajiri, lengo la ubunge wako ni hawa Kapuku!
Nakubaliana na andiko lako
Yani wewe ulitegemea aseme hizi shule binafsi kwa nini zimefanya vibaya au ulitaka aziponde kwa kufanya vizuri kwani wanaosoma pale ni nani?
 
Hatukatai yeye kutoa pongezi,lakini pia alipaswa kutoa pole kwa Shule ya Secondary Masaki ambayo ni miongoni kwa Shule 10 zilizofanya vibaya na inatoka hukohuko Pwani,au kuboronga kwa hiyo Shule hakumuhusu badala yake anahusika na Shule zilizofanya vizuri tu?
 
Hta kama ni za private ila zikifanya vizuri kuna ubaya kuzisifia?

Anazisifia zimefanya vizuri kwa jitihada za mbunge au za serekali? Anasifia za binafsi halafu hana maelezo kwanini za serekali inayomlipa zimefanya vibaya. Halafu utakuta wapiga kura wa jimbo lake hakuna anayemudu kusomesha mtoto kwenye shule hizo. Mwambie ajikalie kimya hizo shule kanisa ndio linapaswa kujisifia.
 
Tatizo watu mnataka kubadilisha maana.. Mbunge ametoa pongezi, hajasifia. Kutoa pongezi sio vibaya regardless ni private schools. Mbona wale top 10 or 20 waliwahi kwenda bungeni? Ile ilikua pongezi na kuwapa motisha, haikua kuwasifia.
 
Back
Top Bottom