Gagurito
JF-Expert Member
- Feb 11, 2011
- 5,600
- 803
MBUNGE wa CDM jimbo la Mbozi Magharibi, David Silinde ameahidi kuwasomesha wanafunzi watakaopata daraja la kwanza katika mtihan wa kidato cha nne kuingia cha tano kwa kutumia mfuko wa jimbo ili kuleta maendeleo kwa kuwapunguzia mzigo wazazi. Akiongea ktk mkutano wa hadhara na wananchi wa kata ya itaka mh. Silinde alisema ameamua kufanya hivyo ili kuweka ushindan kwa wanafunzi wa sekondari wasome kwa bidii wawapo darasani na kuwapa hamasa wazazi kuwahimiza watoto wao wasome kwa bidii zaidi.
Aitha Silinde alisema ifikapo mwaka 2015 atahakikisha ujenzi wa shule ktk kata ambazo hazina unakamilika na kufutilia mbali suala la kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ktk jimbo lake kuepusha kero ya michango isiyokwisha kwa wananchi.
Source; mwananchi newspaper
Aitha Silinde alisema ifikapo mwaka 2015 atahakikisha ujenzi wa shule ktk kata ambazo hazina unakamilika na kufutilia mbali suala la kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ktk jimbo lake kuepusha kero ya michango isiyokwisha kwa wananchi.
Source; mwananchi newspaper