Interest
JF-Expert Member
- Apr 11, 2015
- 3,434
- 7,055
Sugu ni mwanasiasa mzuri. Angekuwa na akili za mahesabu, angeshaukwaa uwaziri na kutumikia wananchi wa Mbeya kwa scope pana zaidi.
Ukweli mchungu ni hawezi kushindana na CCM kama imeamua 2020 asirudi bungeni. Siasa zimebadilika sana. Kama Magufuli na timu yake wameamua Mbeya irudi CCM, itarudi CCM.
Hata Maalim Seif aliamini atakuwa Rais wa Zanzibar 2015. Akajitangaza mshindi. Akavunja Katiba. Uchaguzi ukarudiwa, akasusa, akajua wananchi watafanya kitu. Hakuna lililofanyika. Akategemea Jumuiya za Kimataifa zitaingilia, yakatoka matamko mepesi tu. Sasa hivi kajiunga ACT anazeekea huko.
Sugu meza jeuri yako. Chagua upande unaoweza kukukuza kisiasa na kuwasaidia wananchi. Dunia ya sasa haijali harakati.
Ukweli mchungu ni hawezi kushindana na CCM kama imeamua 2020 asirudi bungeni. Siasa zimebadilika sana. Kama Magufuli na timu yake wameamua Mbeya irudi CCM, itarudi CCM.
Hata Maalim Seif aliamini atakuwa Rais wa Zanzibar 2015. Akajitangaza mshindi. Akavunja Katiba. Uchaguzi ukarudiwa, akasusa, akajua wananchi watafanya kitu. Hakuna lililofanyika. Akategemea Jumuiya za Kimataifa zitaingilia, yakatoka matamko mepesi tu. Sasa hivi kajiunga ACT anazeekea huko.
Sugu meza jeuri yako. Chagua upande unaoweza kukukuza kisiasa na kuwasaidia wananchi. Dunia ya sasa haijali harakati.