Mbunge Prof. Muhongo Achangia Mifuko 200 ya Saruji Ujenzi wa Zahanati

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,908
945

WANAKIJIJI WAMEAMUA KUFUFUA MRADI WA UJENZI WA ZAHANATI YAO - MBUNGE ACHANGIA SARUJI MIFUKO MIA MBILI (200)

Kijiji cha Chimati cha Musoma Vijijini ni moja ya vijiji vitatu vya Kata ya Makojo. Vijiji vingine ni Chitare na Makojo

Kwa muda wa miaka mingi, Kata hii yenye vijiji vitatu ilikuwa inahudumiwa na Zahanati moja tu ya Kijijini Chitare.

Utoaji wa Huduma za Afya kwenye Kata ya Makojo inaenda kubadilika kwa maboresho makubwa. Kituo cha Afya cha Kata hii kimejengwa Kijijini Makojo. Kijiji cha Chimati kimeamua kufufua mradi wa ujenzi wa Zahanati yao ulioanza Mwaka 2018 na kusimama hadi leo.

Harambee ya Mbunge wa Jimbo:
Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo ameungana tena na Wana-Chimati kuendelea na ujenzi wa Zahanati ya Kijiji chao.

Ujenzi ulipoanza Mwaka 2018, Mbunge huyo alianza kutoa michango yake kwa kuchangia Saruji Mifuko 50.

Juzi Jumatano, 10.8.2023, Mbunge huyo, akiambatana na Kamati ya Siasa ya CCM ya Wilaya ya Musoma Vijijini, aliendesha HARAMBEE kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati ya Kijiji hicho.

Matokeo ya HARAMBEE ya Kijijini Chimati:

*Wanakijiji & Wazaliwa wa hapo
Saruji Mifuko 123

*Kamati ya Siasa (CCM) ya Wilaya
Saruji Mifuko 25

*Mbunge wa Jimbo
Saruji Mifuko 200

Kero na matatizo yaliyowasilishwa na wananchi wa Kata ya Makojo:
*Mbunge wa Jimbo alipokea kero na matatizo yanayowakabili wananchi, na kuyatolea majibu.

*Mwenyekiti wa Chama Wilaya, Ndugu Denis Ekwabi, na Katibu wa Chama Wilaya (CCM), Ndugu Valentine Maganga walijibu maswali yaliyoelekezwa kwenye Chama. Vlevile, walitoa elimu na ufafanuzi kwa masuala mengine yaliyoulizwa.

Jimbo la Musoma Vijijini linaendelea kuboresha utoaji wa Huduma za Afya na takwimu za sasa ni hizi hapa:

*Hospitali ya hadhi ya Wilaya:
1 (moja), imeanza kutoa huduma

*Vituo vya Afya (6)
2 vinatoa huduma
2 vinatoa huduma kwa hadhi ya Zahanati
2 ni vipya vinasubiri kufunguliwa

*Zahanati 42
24 zinatoa huduma (za Serikali)
14 zinajengwa (Wananchi & Serikali, baadhi)
4 ni za Binafsi

Picha zilizoambatanishwa hapa zinaonesha matukio mbalimbali ya tarehe 10.8.2023 ya Harambee ya Kijijini Chimati.

Tenki la maji la ujazo wa lita 75,000 (pichani) linakamilishwa ujenzi Kijijini Chimati kwa ajili ya maji ya bomba ya Kijiji hicho.

SHUKRANI:
Wananchi na Viongozi wote wa Jimbo la Musoma Vijijini wanaendelea kuishuruku Serikali yetu chini ya uongozi mzuri wa Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutupatia fedha za miradi mbalimbali ikiwemo ya Sekta ya Afya - ahsanteni sana!

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Jumamosi, 12.8.2023
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-08-12 at 18.10.57(2).jpeg
    WhatsApp Image 2023-08-12 at 18.10.57(2).jpeg
    78.8 KB · Views: 5
  • WhatsApp Image 2023-08-12 at 18.10.57(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-08-12 at 18.10.57(1).jpeg
    94.6 KB · Views: 4
  • WhatsApp Image 2023-08-12 at 18.10.57.jpeg
    WhatsApp Image 2023-08-12 at 18.10.57.jpeg
    106.5 KB · Views: 4
  • WhatsApp Image 2023-08-12 at 18.10.56(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-08-12 at 18.10.56(1).jpeg
    109.1 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2023-08-12 at 18.10.56.jpeg
    WhatsApp Image 2023-08-12 at 18.10.56.jpeg
    110.5 KB · Views: 2

WANAKIJIJI WAMEAMUA KUFUFUA MRADI WA UJENZI WA ZAHANATI YAO - MBUNGE ACHANGIA SARUJI MIFUKO MIA MBILI (200)

Kijiji cha Chimati cha Musoma Vijijini ni moja ya vijiji vitatu vya Kata ya Makojo. Vijiji vingine ni Chitare na Makojo

Kwa muda wa miaka mingi, Kata hii yenye vijiji vitatu ilikuwa inahudumiwa na Zahanati moja tu ya Kijijini Chitare.

Utoaji wa Huduma za Afya kwenye Kata ya Makojo inaenda kubadilika kwa maboresho makubwa. Kituo cha Afya cha Kata hii kimejengwa Kijijini Makojo. Kijiji cha Chimati kimeamua kufufua mradi wa ujenzi wa Zahanati yao ulioanza Mwaka 2018 na kusimama hadi leo.

Harambee ya Mbunge wa Jimbo:
Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo ameungana tena na Wana-Chimati kuendelea na ujenzi wa Zahanati ya Kijiji chao.

Ujenzi ulipoanza Mwaka 2018, Mbunge huyo alianza kutoa michango yake kwa kuchangia Saruji Mifuko 50.

Juzi Jumatano, 10.8.2023, Mbunge huyo, akiambatana na Kamati ya Siasa ya CCM ya Wilaya ya Musoma Vijijini, aliendesha HARAMBEE kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati ya Kijiji hicho.

Matokeo ya HARAMBEE ya Kijijini Chimati:

*Wanakijiji & Wazaliwa wa hapo
Saruji Mifuko 123

*Kamati ya Siasa (CCM) ya Wilaya
Saruji Mifuko 25

*Mbunge wa Jimbo
Saruji Mifuko 200

Kero na matatizo yaliyowasilishwa na wananchi wa Kata ya Makojo:
*Mbunge wa Jimbo alipokea kero na matatizo yanayowakabili wananchi, na kuyatolea majibu.

*Mwenyekiti wa Chama Wilaya, Ndugu Denis Ekwabi, na Katibu wa Chama Wilaya (CCM), Ndugu Valentine Maganga walijibu maswali yaliyoelekezwa kwenye Chama. Vlevile, walitoa elimu na ufafanuzi kwa masuala mengine yaliyoulizwa.

Jimbo la Musoma Vijijini linaendelea kuboresha utoaji wa Huduma za Afya na takwimu za sasa ni hizi hapa:

*Hospitali ya hadhi ya Wilaya:
1 (moja), imeanza kutoa huduma

*Vituo vya Afya (6)
2 vinatoa huduma
2 vinatoa huduma kwa hadhi ya Zahanati
2 ni vipya vinasubiri kufunguliwa

*Zahanati 42
24 zinatoa huduma (za Serikali)
14 zinajengwa (Wananchi & Serikali, baadhi)
4 ni za Binafsi

Picha zilizoambatanishwa hapa zinaonesha matukio mbalimbali ya tarehe 10.8.2023 ya Harambee ya Kijijini Chimati.

Tenki la maji la ujazo wa lita 75,000 (pichani) linakamilishwa ujenzi Kijijini Chimati kwa ajili ya maji ya bomba ya Kijiji hicho.

SHUKRANI:
Wananchi na Viongozi wote wa Jimbo la Musoma Vijijini wanaendelea kuishuruku Serikali yetu chini ya uongozi mzuri wa Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutupatia fedha za miradi mbalimbali ikiwemo ya Sekta ya Afya - ahsanteni sana!

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Jumamosi, 12.8.2023
Nikajua ametengeneza mwenyewe mwanzo mwisho. Mifuko 200 kwa mbunge?

Sent from my SM-A515F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom