Stroke
JF-Expert Member
- Feb 17, 2012
- 38,638
- 49,048
Hivi majuzi katika ufunguzi wa chaguzi za baraza la wanawake Chadema, KUB, Bw, Mbowe alitoa wasaa na nina mnukuu;
" ili kuwa na nchi yenye maendeleo, tunahitaji kuwa na taasisi imara za kidemokrasia, tusitumie muda na nguvu kuzibomoa, bali kuzijenga"
Nakiri kuwa hii ni kauli komavu kabisa ya kisiasa toka kwa mwenyekiti wa chadema, nampongeza kwa hilo.
Baada ya pongezi hizo, najikita kwenye lengo kuu la kujadili kauli hiyo,
Si kazi rahisi, nakiri kabisa, kujenga taasisi imara inayohusisha watu zaidi ya mmoja, ukizingatia kuwa watu hao, wana imani zao, vipato tofauti, uwezo tofauti wa kutazama mambo, malengo na matarajio pia, hivyo inahitajika busara ya hali ya juu kabisa kuhakikisha hayo yote yanafanikiwa chini ya mwavuli wa taasisi hiyo.
Naguswa kusema kwamba kauli aliyoitoa bwana mbowe haiendani na matendo halisi na picha tunayoiona sisi wananchi kwa kuangalia mwenendo mzima wa Chama anachokiongoza.
Waingereza wanasema " Charity Starts at Home" Bwn. Mbowe unaitimiza vipi kauli yako kulingana na msemo huu wa waungwana hawa.
Katika vipindi tofauti tumekuwa tukisikia malalamiko mbali mbali toka kwa baadhi ya wanachama na waliowahi kushika nafasi za uongozi ndani ya chama kuwa, ndani ya chama kuna siasa za kikanda, kikabila na kidini....tumeona baadhi , wakijiuzulu nyadhifa zao na wengine kuondolewa nyadhifa zao kwa tuhuma za usaliti...
Tuhuma hizo za usaliti zimekuwa zikiibuliwa mara baada ya wahusika kuhoji baadhi ya mambo na mienendo ndani ya chama, tuna mifano hai ya hayo...yaliyowakuta sote tunayajua...
Kuna makelele ya wanachama kuhusiana na kutokuwepo na ukomo wa muda wa kugombea kwa nafasi za uenyekiti na nyinginezo za juu katika chama.....agenda ya hili ni ipi....
sidhani kama kuwa mwenyekiti wa milele, au kuwa katibu wa milele katika chama ndio kujenga taasisi imara ya kidemokrasia, nahisi ni tofauti..
kuhodhi madaraka kwa muda mrefu, ni kubomoa taasisi ambayo ulitumika muda kuijenga, bila wasiwasi wanachama wataanza kuingiwa hofu na kuhisi kuwa taasisi fulani ni kwa ajili ya watu flani.....
NI imani yangu kwamba, lengo kuu la kuanzishwa kwa chadema ilikuwa ni kufanya yale ambayo waanzilishi waliona yakifanyika na wengine katika hali ya kimakosa, hivyo kujaribu kurekebisha....
Taifa, ili likue, linahitaji kuwa na watu walio katika taasisi shindani huru na zenye tija...malengo ikiwa ni kupeana changamoto za kimaendeleo na si zaidi ya hapo..
Ni imani yangu kwamba taasisi zote za kidemokrasia , ikijumuishwa na chadema, zitakuwa taasisi huru, na imara zisizo na mawaa.
Nawasilisha.
====================
Bonyeza hapa chini kusikiliza alichokisema Freeman Mbowe
[JFMP3]https://www.jamiiforums.com/attachment.php?attachmentid=184543&d=1410432197[/JFMP3]
" ili kuwa na nchi yenye maendeleo, tunahitaji kuwa na taasisi imara za kidemokrasia, tusitumie muda na nguvu kuzibomoa, bali kuzijenga"
Nakiri kuwa hii ni kauli komavu kabisa ya kisiasa toka kwa mwenyekiti wa chadema, nampongeza kwa hilo.
Baada ya pongezi hizo, najikita kwenye lengo kuu la kujadili kauli hiyo,
Si kazi rahisi, nakiri kabisa, kujenga taasisi imara inayohusisha watu zaidi ya mmoja, ukizingatia kuwa watu hao, wana imani zao, vipato tofauti, uwezo tofauti wa kutazama mambo, malengo na matarajio pia, hivyo inahitajika busara ya hali ya juu kabisa kuhakikisha hayo yote yanafanikiwa chini ya mwavuli wa taasisi hiyo.
Naguswa kusema kwamba kauli aliyoitoa bwana mbowe haiendani na matendo halisi na picha tunayoiona sisi wananchi kwa kuangalia mwenendo mzima wa Chama anachokiongoza.
Waingereza wanasema " Charity Starts at Home" Bwn. Mbowe unaitimiza vipi kauli yako kulingana na msemo huu wa waungwana hawa.
Katika vipindi tofauti tumekuwa tukisikia malalamiko mbali mbali toka kwa baadhi ya wanachama na waliowahi kushika nafasi za uongozi ndani ya chama kuwa, ndani ya chama kuna siasa za kikanda, kikabila na kidini....tumeona baadhi , wakijiuzulu nyadhifa zao na wengine kuondolewa nyadhifa zao kwa tuhuma za usaliti...
Tuhuma hizo za usaliti zimekuwa zikiibuliwa mara baada ya wahusika kuhoji baadhi ya mambo na mienendo ndani ya chama, tuna mifano hai ya hayo...yaliyowakuta sote tunayajua...
Kuna makelele ya wanachama kuhusiana na kutokuwepo na ukomo wa muda wa kugombea kwa nafasi za uenyekiti na nyinginezo za juu katika chama.....agenda ya hili ni ipi....
sidhani kama kuwa mwenyekiti wa milele, au kuwa katibu wa milele katika chama ndio kujenga taasisi imara ya kidemokrasia, nahisi ni tofauti..
kuhodhi madaraka kwa muda mrefu, ni kubomoa taasisi ambayo ulitumika muda kuijenga, bila wasiwasi wanachama wataanza kuingiwa hofu na kuhisi kuwa taasisi fulani ni kwa ajili ya watu flani.....
NI imani yangu kwamba, lengo kuu la kuanzishwa kwa chadema ilikuwa ni kufanya yale ambayo waanzilishi waliona yakifanyika na wengine katika hali ya kimakosa, hivyo kujaribu kurekebisha....
Taifa, ili likue, linahitaji kuwa na watu walio katika taasisi shindani huru na zenye tija...malengo ikiwa ni kupeana changamoto za kimaendeleo na si zaidi ya hapo..
Ni imani yangu kwamba taasisi zote za kidemokrasia , ikijumuishwa na chadema, zitakuwa taasisi huru, na imara zisizo na mawaa.
Nawasilisha.
====================
Bonyeza hapa chini kusikiliza alichokisema Freeman Mbowe
[JFMP3]https://www.jamiiforums.com/attachment.php?attachmentid=184543&d=1410432197[/JFMP3]