Mbowe: Magufuli pambana na wauza gongo Kilimanjaro

R.B

JF-Expert Member
May 10, 2012
6,296
2,573
Akiongea katika kikao cha 34 cha kamati ya ushauri ya mkoa, Mbunge wa Hai amemuomba rais na serikali yake kuweka mkazo katika kupambana na uuzaji pombe aina ya gongo mkoani Kilimanjaro;\

Amesema utengenezji pombe umezidi kushamili. Amesema kuna mtandao mkubwa wa wapika gongo kiasi kwamba wakikamatwa muda si mrefu wanaonekana mitaani.

Waziri Magembe ameunga mkono na kusema watendaji kata ndio tatizo. Hilo tatizo linahitaji nguvu ya kiroho na kiserikali, haswa iliyopo chini ya JPM.
 
Mkoa wa Kilimanjaro nguvu kazi inaishia kwenye pombe za kienyeji yaani Kwisha kabisa vijana wamekuwa wazeee gafla
 
Mkoa wa Kilimanjaro nguvu kazi inaishia kwenye pombe za kienyeji yaani Kwisha kabisa vijana wamekuwa wazeee gafla

Sehemu ambazo CHADEMA imeshika kuna vijana wengi walevi kupindukia nenda kilimanjaro,nenda,arusha,nenda mbeya mjini,nenda tunduma ni balaa.Na wote sifa zao kubwa ni kutembea na viroba mifukoni.

CHADEMA ijitathmini kwa nini maeneo yake vijana wanaharibika hivyo?
 
Sehemu ambazo CHADEMA imeshika kuna vijana wengi walevi kupindukia nenda kilimanjaro,nenda,arusha,nenda mbeya mjini,nenda tunduma ni balaa.Na wote sifa zao kubwa ni kutembea na viroba mifukoni.

CHADEMA ijitathmini kwa nini maeneo yake vijana wanaharibika hivyo?
Na wanachaguana kutoka miongoni mwao....angalia hata wabunge wa maeneo hayo, ni utata mtupu.
 
Mbowe mtu wa ajabu sana. Kabla ya kuomba msaada kwa Magufuli, yeye na CDM wamefanya nini kulikabili tatizo kwenye halmashauri wanazoziongoza?
Wabunge na madiwani wengi ni wa kwake. Serikali za mitaa inakotengenezwa gongo zinaongozwa na chama chake.
Polisi peke yake bila viongozi wa mitaa, madiwani na halmashauri hawaelewi kukomesha suala la gongo
 
Jamani tuweni serious kidogo hivi wakuu wa mikoa,wilaya wabunge,madiwani watendaji na hata Polisi ngazi hizo wameshindwa kweli kuelimisha jamii inayowazunguuka kuacha kutumia gongo km kinywaji hadi ishu hiyo ije ifuatiliwe na Rais ama Waziri Mkuu ????dah pumu zikawaa mkorozi kweeli
 
wakati wa kampeni wao ndio wanawanunulia hizo gongo au umesahau hao ndio walikupa kura.Rais hatakiwi kufanya kazi kama hizo ndio maana kuna wakuu wa mikoa,wilaya,makatibu tawala wakurugenzi wa miji wilaya hata kwa kutumia madiwani mnaweza kufanya hiyo kazi hii inaonyesha wazi hamna uelekeo wowote kama kiongozi wa chama anatamka hayo mambo
 
Akiongea katika kikao cha 34 cha kamati ya ushauri ya mkoa, Mbunge wa Hai amemuomba rais na serikali yake kuweka mkazo katika kupambana na uuzaji pombe aina ya gongo mkoani Kilimanjaro;\

Amesema utengenezji pombe umezidi kushamili. Amesema kuna mtandao mkubwa wa wapika gongo kiasi kwamba wakikamatwa muda si mrefu wanaonekana mitaani.

Waziri Magembe ameunga mkono na kusema watendaji kata ndio tatizo. Hilo tatizo linahitaji nguvu ya kiroho na kiserikali, haswa iliyopo chini ya JPM.
Hivi kweli hata mapambano dhidi ya pombe haramu yanamsubiri rais? Viongozi wa vijiji/serikali za mitaa madiwani na wabunge wa maeneo husika nini wajibu wao. Polisi jamii na polisi hakuna huko?
 
Vijana wa Kilimanjaro huwa wananikera Sana yani yamekaa kulewa tu..yanafanyiwa kazi na wazee yenyewe ni gongo na dadii tu..ukifika huko wanaanza kujazana eti wanaomba hela..wengine wanapigwa hadi na wake zao kisa ulevi wa banana..
 
Jamani tuweni serious kidogo hivi wakuu wa mikoa,wilaya wabunge,madiwani watendaji na hata Polisi ngazi hizo wameshindwa kweli kuelimisha jamii inayowazunguuka kuacha kutumia gongo km kinywaji hadi ishu hiyo ije ifuatiliwe na Rais ama Waziri Mkuu ????dah pumu zikawaa mkorozi kweeli
Kumbe ukitulia zinachaji sana kichwani eeeeh! Uachage kujifanya zezeta na ubavicha wako. Tunataka mitazamo kama hii.
 
Hii ni kazi ya DC na katibu kata. Rais ashughulikie majipu kabla ya vipele

Akiongea katika kikao cha 34 cha kamati ya ushauri ya mkoa, Mbunge wa Hai amemuomba rais na serikali yake kuweka mkazo katika kupambana na uuzaji pombe aina ya gongo mkoani Kilimanjaro;\

Amesema utengenezji pombe umezidi kushamili. Amesema kuna mtandao mkubwa wa wapika gongo kiasi kwamba wakikamatwa muda si mrefu wanaonekana mitaani.

Waziri Magembe ameunga mkono na kusema watendaji kata ndio tatizo. Hilo tatizo linahitaji nguvu ya kiroho na kiserikali, haswa iliyopo chini ya JPM.
 
Mbowe mtu wa ajabu sana. Kabla ya kuomba msaada kwa Magufuli, yeye na CDM wamefanya nini kulikabili tatizo kwenye halmashauri wanazoziongoza?
Wabunge na madiwani wengi ni wa kwake. Serikali za mitaa inakotengenezwa gongo zinaongozwa na chama chake.
Polisi peke yake bila viongozi wa mitaa, madiwani na halmashauri hawaelewi kukomesha suala la gongo
Hadi mameya ni wa kwao.Tatizo CHADEMA wanachotaka ni madaraka sio kazi.Unakuta wakishapata wanaanza kusukumia serikali.Waliimba serikali ya CCM haijafanya kitu tupeni sisi madaraka muone.Wananchi wakawapa kura kuanzia madiwani,wabunge hadi mameya.Wamepata madaraka Porojo zile zile zinaendelea serikali ishughulikie wanywa gongo!!!

Nakumbuka vizuri serikali ilikuwa ikipiga vita gongo na viroba hawa hawa CHADEMA WALIKUWA WAKIPITA KUPINGA KUWA SERIKALI INAPIGA VITA BIASHARA ZA WATU WADOGO za kuuza pombe na viroba bila kuwapa kitu kingine mbadala ili wapate wafuasi na watu wa kuwapigia kura.Sasa wameendekeza hilo muda mrefu hadi wengine walidiriki kusema mkichagua CCM itapiga marufuku gongo na viroba mtajua wenyewe mtaishije wakati hamna starehe ingine na biashara ingine.CCM kweli walikuwa wakipiga vita hasa na walianza kupiga marufuku viroba mfano toka Malawi kuingia nchini na kuteketeza vile vinavyoshikwa.CHADEMA walitumia nguvu wanayoita ya umma kupinga na wakatumia kama agenda ya kuibwaga CCM maeneo ya Tunduma ,MBEYA mjini na Arusha mjini na Rombo.Sawa wameshinda lakini madhara ndio hayo.Wanywa gongo na viroba wanajisikia raha mstarehe wakiwa Chini ya CHADEMA. Sasa hayo matokeo yameanza unasikia majogoo hata ya vijana wa kiume Rombo hayawiki tena inabidi kuagiza wakenya washughulikie watoto wa kike wa kirombo.Kushinda wameshinda lakini kwa gharama ya afya za watu.

Siasa zimesababisha vita ya kupambana na gongo na viroba mikoa hiyo kuwa ngumu.Ufumbuzi wake uko mikononi mwa CHADEMA.
 
Apambane nao kivipi wakati chadema ilikuja na sera ya kuhalalisha gongo? Hii kweli ni kubadili gea angani
 
Mkoa wa Kilimanjaro nguvu kazi inaishia kwenye pombe za kienyeji yaani Kwisha kabisa vijana wamekuwa wazeee gafla
Ni kweli mkuu...ushahidi upo wa kutosha tu
 

Attachments

  • 1455351069742.jpg
    1455351069742.jpg
    50.1 KB · Views: 39
Bila ya Gongo,Viroba na bhangi Chadema ingepataje vijana wa kusafisha barabara na kuzungusha Mikono?
Chadema inaongoza Mkoa wote wa Kilimanjaro pamoja na Manispaa zake, iweje ishu ya Gongo tu mpaka JPM aingilie
 
Back
Top Bottom