Mbowe anastahili heshima

Mbowe anastahili heshima

Ashasembeko

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2017
Posts
226
Reaction score
914
Katika viongozi ambao wamepitia katika changamoto nyingi miaka mitano iliyopita ni Freeman Mbowe anashika nafasi ya pili baada ya Tundu Lissu.

Tukianza na kwamba ameharibiwa biashara zake. Wamemvunjia Club Bilcanas, Mashamba yake Hai na wamelifungia gazeti lake.

Tukumbuke mwaka 2018 yeye na Esther Matiko walikaa jela karibia miezi sita na kunyimwa dhamana.

Kuna kipindi walitaka hadi kumpora chama.

Mwaka huu, yeye na viongozi wengine wa Chadema, walihukumiwa kifungo cha miezi mitano au faini ya million 350. Tunajua lengo lilikua kukifilisi chama kuelekea uchaguzi lakini waliumbuka baada ya wananchi kwa ujumla wao kuwachangia na kulipa faini yote.

Wakaona haitoshi, wakamshambulia katika makazi yake Dodoma ili asiweze kufanya kampeni. Wakaenda mbali na kumdhalilisha bungeni na kwenye magazeti yao ya propaganda wakasema eti alikuwa amelewa.

Na yule DC wa Hai anaemfanyia unyama kila kukicha. Juzi tu nyumba yake ilivamiwa na fundi wake kupigwa risasi. Wakaona haitoshi wakaenda mvamia hadi Hoteli aliyokuwepo.

Wakati uchaguzi unaendelea vijana wa Sabaya walimuweka kizuizini na hakuweza hata kwenda kupiga kura.

Leo tunaskia amekamatwa na polisi kwa kuchochea maandamano.

Huyu mtu hata kama upo CCM, anastahili heshima yako. Mambo aliyoyapitia na aliyoyapoteza binadamu wa kawaida hawezi kustahimili.

Ni wazi kuwa watawala wanamchukia sana Mbowe, na bado nashindwa elewa hii chuki inatoka wapi. Kwanini Mbowe?

Zitto Kabwe aliwahi hadi andika barua kuomba mkopo wa WB usitishwe ili hatuoni akisumbuliwa sana kama Mbowe – japo na yeye kapitia magumu pia.

Kuna nini nyuma ya haya mashambulio ya bwana Mbowe?
 
Kuna nini nyuma ya haya mashambulio ya bwana Mbowe?
Acha kujiliza na kuomba huruma
Kama mtu hajiheshimu wala kumuheshimu mkewe,hiyo heshima unayotaka apewe itatoka wapi?
Mtu anamsaliti mkewe mpaka amezaa na kimada,halafu unataka kutueleza nini wewe tanapa tu
 
Freeman Elikael Mbowe ni kada mtiifu wa CCM,ana posho yake kila mwaka yupo pale kwa kazi maalum,hamjiulizi mioango yte ya Chadema CCM wanaigundua mapema??
 
Chuki inasababishwa na ushamba tu, wanadhani utajiri alionao kawaibia serikalini, kumbe mtu kazaliwa ameukuta upo nyumbani.

Tuwe makini sana tunapotoa madaraka ya juu kwa watu wasiojua hata mjini kunafananaje, haya ndio madhara yake.
 
Freeman Elikael Mbowe ni kada mtiifu wa CCM,ana posho yake kila mwaka yupo pale kwa kazi maalum,hamjiulizi mioango yte ya Chadema CCM wanaigundua mapema??
Then kwanini wamuharibie mali zake kama ni mwenzao?!
 
Hata kama anaigiza basi sterling atakuwa amepata hadi ajali.
 
Mfalme hataki kuona mwingine anatajwa na kuheshimika.Pia pamoja na masibu yote hajawahi piga magoti kwa mfalme kusujudu.
 
Back
Top Bottom