Mbosso Khan, fundi mpya Mjini

Slowly

JF-Expert Member
Jul 7, 2016
10,486
34,789
Aiseee nimesikiliza goma jipya la Mboso Khan linaitwa "Yalaah" nimehitimisha Kwa kusema kuwa Mbosso ni fundi mpya wa mashairi hapa mjini......

Director Hanscana ni legend

Kitu kingine nilichogundua ni kuwa Diamond anapomsajili msanii anaangalia Sana uwezo wa kutunga mashairi mana ndo njia pekee itakayomvusha msanii kwenye vikwazo vingi .....

Kuanzia Harmonize , Rayvanny, Zuchu na Mbosso ni mafundi Sana wa mashairi , .... Wanaweza kukosea Ngoma moja ama mbili Ila dude la tatu linamrudisha kwenye mstari.....

Lava lava ,qeen Darling hawa daaaah .....!!! Wanahtaji maombi ya kutambika ...

Ila zaidi ya yote mbosso ni fundi

diamondplatnumz-___CMZQ2fPFgV7___-.jpg
 
Mimi sio shabiki wa wasafi but i think Kati ya album zilizotoka wasafi mbosso ndo katisha,
Kafanya vizuri na albamu yake tofauti na rayvanny
Jamaa fundi Sana ....
 
Ukimtoa diamond platnumz kama mmoja wa waimbaji waliofanya kazi wakiwa peke yao, Mbosso ndio msanii namba mbili kwa kutengeneza views nyingi youtube akiwa kaimba mwenyewe(sole artist kama sijakosea).

Kwa sasa sina shaka na mbosso kama ndio msanii pekee anae umiza kichwa akiwa peke yake na kutoa vibao vinavyogusa sehemu husika sio mtu wa copy and paste kabisa akiwa peke yake.

Kuna baadhi wanasema nyimbo za mbosso acheni aimbe yeye haziigiki.
 
Watu mnawezaje kumsikiliza Mbosso? And I love bongo fleva.
 
Back
Top Bottom