JUST
JF-Expert Member
- Dec 10, 2010
- 552
- 234
Kama kweli unaipenda nchi yako basi utatoa maoni yako ya chanya na si hasi
sababu za ccm kufika ukoomo wa kuongoza nchi ni:-
a) mosi ccm kama chama kiweruhusu na kuwakumbatia viongozi ambao sio wazalendo na wasio na uchungu na maisha ya mtanzania wa hali ya chini.
B)pili ccm kimekua ni chama kilichotupa ahadi za matumaini kwa muda mrefu ili hali mabadiliko hatuoni zaidi ya kuendelea kupata shida.
C) tatu ccm ni chama kinachounganisha serikali na chama, hili linajionyesha kwa matendo ya viongozi wa kichama kuwa na maamuzi yanayoendana na serikali katika utekelezaji wa kazi zao. Athari yake ndio ufisadi na mengineo mengi ikiwemo unyanyasaji wananchi.
D) nne ccm imeongoza kwa miaka 50 imebakiza miaka mitano ya umri wa mfayakazi kustaafu kwa hiari, hivyo nadhani na wao ni muda wa kupumzika kustaafu sio tu kwa hiari bali kwa manufaa ya uma.
E) tano ccm haina ridhaa ya wanchi kwa sababu takwimu zinaonyesha ccm imeweza kupata wanachama milioni 5 kati ya watanzania milioni 40 ndani ya miaka hamsini. Hii ni fedheha kwa sababu watanzania milioni 15 wenye uwezo wa kupiga kura na kuwa wanachama hai hawakipendi.
2.mbinu makakti wa kukiondoa ccm madarakani kwa halali
a) moja, safari ya uchaguzi 2015 inaanza sasa kwa hiyo tufanye shughuli zetu tukiangalia kama hiki chama bado kinaweza. Na kama hakiwezi hakuna sababu ya kuendelea nacho.
B) pili, kila unapokaa na wale tunaosema wamekosa fursa ya elimu waelezee kiufasaa na kwa lugha adilifu mambo ambayo viongozi wa ccm wanafanya na madhaufra yake kwake na kwa taifa kwa ujumla.
C) tatu, viongozi wetu wa dini zetu wote waeleze ukweli waumini wao kwamba chama kilichopo madarakani kimepoteza dira na hivyo tutafute mbadala kwa manufaa ya wananchi. Kazi ya kuchunga kondoo wa bwana ni pamoja na maadili ya viongozi wa serikali.
D) naomba mwenye mbinu zaidi achangie kwa pamoja tutaweza.
sababu za ccm kufika ukoomo wa kuongoza nchi ni:-
a) mosi ccm kama chama kiweruhusu na kuwakumbatia viongozi ambao sio wazalendo na wasio na uchungu na maisha ya mtanzania wa hali ya chini.
B)pili ccm kimekua ni chama kilichotupa ahadi za matumaini kwa muda mrefu ili hali mabadiliko hatuoni zaidi ya kuendelea kupata shida.
C) tatu ccm ni chama kinachounganisha serikali na chama, hili linajionyesha kwa matendo ya viongozi wa kichama kuwa na maamuzi yanayoendana na serikali katika utekelezaji wa kazi zao. Athari yake ndio ufisadi na mengineo mengi ikiwemo unyanyasaji wananchi.
D) nne ccm imeongoza kwa miaka 50 imebakiza miaka mitano ya umri wa mfayakazi kustaafu kwa hiari, hivyo nadhani na wao ni muda wa kupumzika kustaafu sio tu kwa hiari bali kwa manufaa ya uma.
E) tano ccm haina ridhaa ya wanchi kwa sababu takwimu zinaonyesha ccm imeweza kupata wanachama milioni 5 kati ya watanzania milioni 40 ndani ya miaka hamsini. Hii ni fedheha kwa sababu watanzania milioni 15 wenye uwezo wa kupiga kura na kuwa wanachama hai hawakipendi.
2.mbinu makakti wa kukiondoa ccm madarakani kwa halali
a) moja, safari ya uchaguzi 2015 inaanza sasa kwa hiyo tufanye shughuli zetu tukiangalia kama hiki chama bado kinaweza. Na kama hakiwezi hakuna sababu ya kuendelea nacho.
B) pili, kila unapokaa na wale tunaosema wamekosa fursa ya elimu waelezee kiufasaa na kwa lugha adilifu mambo ambayo viongozi wa ccm wanafanya na madhaufra yake kwake na kwa taifa kwa ujumla.
C) tatu, viongozi wetu wa dini zetu wote waeleze ukweli waumini wao kwamba chama kilichopo madarakani kimepoteza dira na hivyo tutafute mbadala kwa manufaa ya wananchi. Kazi ya kuchunga kondoo wa bwana ni pamoja na maadili ya viongozi wa serikali.
D) naomba mwenye mbinu zaidi achangie kwa pamoja tutaweza.