Mbinguni ni wapi?

Hapo ndio mnachanganyaga mambo mnatumia Falfasa na mawazo ya kibinadamu kumuelezea Mungu! sijui mfinyanzi sijui udongo sijui Muda weka maandiko mzee unamzungumzia Mungu kwa mifano yako badala ya maneno yake mwenyewe!
Maandiko matakatifu yanasema hivi katika Ayubu 36:26 "Tazama, Mungu ni mkuu, nasi hatumjui; Hesabu ya miaka yake haitafutiki" ukisoma KJV ndio unapata maana nzuri Job 36:26 "Behold, God is great, and we do not know Him; Nor can the number of His years be discovered."
Mungu ni mkubwa sana kwa hizi akili zetu za kibinadamu hatuwezi kumjua kabisaaaa,tunajitahidi kumuelezea tu kwa vitu vyake vichache alivyotufunulia na kajifunua kwetu kwa asilima ndogo sana kuliko alivyo kiuhalisia ndiomaana imeandikwa "HATUMJUI"!!!,Pia biblia imeandika HEKIMA na MAARIFA yake Mungu HAYACHUNGUZIKI na NJIA ZAKE MUNGU HAZITAFUTIKANI!!!! (WARUMI 11:33)
Ndiomaana Mungu alivyokuwa anajifunua kwa baadhi ya Mitume hakuna aliyeona ukuu woote wa Mungu!(total completion) walikuwa wanaona vitu vichache sana,wengine walikuwa wanasikia sauti,wengine ndoto,Musa alifanikiwa kumuona kidogo upande,usije na falsafa zako ukaanza kumchambua Mungu hadi na makazi yake wakati hamna reference yoyote ya maandiko!
 
Mleta mada iwapo mungu anaishi mbinguni au la sijui, ila mbingu ni kule unapoziona nyota na celestial bodies nyingine
 
Habari mkuu.

Umetaja maneno au mistari kutoka kwa Ayubu wa agano la kale sio. Kwani Ayubu ndio Mungu. Si binadamu kama mimi au unataka niandike kitabu then wasema niliambiwa na Mungu niseme.

Agano la kale lilitenguliwa na Yesu. Wakati ilikuwa dhambi kulitamka jina la Mungu. Yesu alisema yeye ni mtoto Mungu.

Wayahusi walimashangaa wakiona anamtusi kamtusi Mungu wao. Walipo muuliza Tohala inaumuhimu gani kwa Mungu aliwaambia kama Baba Mungu angiliona ni Muhimu basi wangetahiliwa wakiwa mimba tumboni mwa mama zao.
Wayahudi walikuwa wanaitambua siku ya Sabato yeye aliponya

Wakati wakisema haiwezekani kumjua Mungu, Yesu anasema anayo njia ya Uzima wa milele, yeyote atakayemuamini atamuonyesha njia ya uzima wa milele na ata muona Mungu.

Nami nakwambia iko njia na njia hiyo inaanzia Rohoni kwako. Yohana 4: 20 -23. Roho yako ndio nafsi yako ya kweli. Ukiijua namna ya kuitumia utajijua na kwa sababu Mungu ni Roho pia na alikuumba kwa mfano wake. Utamjua pia.

Omba rehema uweze jua namna ya kumuabudu Mungu kwa njia ya Roho, utaijua KWELI. Usingoje ufe ilikujua Njia hiyo. Roho ilikuwepo, ipo na itakuwepo. Ndio daraja lakujua Kweli.
 
Mbinguni ni sehemu ambayo hakuna binadamu anayeweza kuijua ilipo

kama ilivyo bustani ya eden ambayo iliwekewa ulinzi kiasi kwamba hakuna binadamu anayeweza kufika wala kupaona

hii ni ktk imani... Siyo sayansi ya ulimwengu

ahsante
 
nitakujibu.
Kwenye hivyo vitabu hakuna aliyesema alikutana na Mungu na kasema. Bali yalikuwa na Maono yao ya kiroho.

Kama wao waliona hayo maona kwani nini mimi na wewe tuweze yaona. Biblia imepotoshwa sana sio kosa sababu kutunza simulizi kwa asilia 100 ni Ngumu sana.

Hivi inalijua Jina halisi la Yesu? Limepotoshwa pia. Kwa hiyo sio kila mstari kwenye biblia isomwe kama ulivyo.

Kuhusu Utatu mtakatifu ni tafsiri yangu nipoteyari kuitetea hata kama nitapingana na dunia nzima.

Lengo la kuzaliwa ndani ya mwili ni kupata kuwa moja na Mungu kuwa mtakatifu. Na mwilini ni mahali unapopigania utakatifu huo. Umeumbwa na Mungu Baba, Mungu Mama na Roho Mtakatifu. Roho ya Binadamu ni Mungu Mwana. Ni matokeo ya utatu mtakatifu huo, sio kati ya utakatifu huo.

Sija nukuu toka kitabu chochote bali Najua hivyo. Sasa sijui utataka ni prove vipi? Labda ukubali kuwa mwanafunzi wangu nami nikubali kuwa mwalimu wako, kitu ambacho siafikiani nacho.

Nikutake upate shauku ya kujua zaidi ya unayoyajua.

Asante.
 
Mwe!
Hata sijui nianzie wapi kukujibu maana umeonyesha hujui maandiko kabisaaaa hapo ulipokosoa kitabu cha ayubu maana yake wewe bado mchanga sana kiroho na kimaandiko unahitaji ufundishwe a e i o u za kimaandiko na sio vitu vyenye kina kirefu kama hii mada hapa huwezi kuielewa! jifunze kwanza kabla hujamjibu mtu au kama hujui kuwa muwazi ueleweshwe
 
Siku moja nilipofanya maombi mazito juu ya ndugu yangu mmoja nilionyeshwa akiwa anazini na wanawake wawili Basi mwanamke mmoja akanifata ili niweze kuzini nae Mimi nikamkataa pakatokeamu nyoka mdogo mweusi nikawapa maelekezo wamue nikawa nimefumba mamcho ndani ya ulimwengu wa Roho ndotoni ghafla nilifunuliwa Mbingu nzuri ya kustajabu hakika Mungu yupo na nina sababu nyingi za kuproof kuwa kuwa Mungu ya karibu nasi rohoni hio ni roho mtakatifu Ila yupo Mungu baba muweza wa yote.. Soma Matendo 10:11
pia Mungu huzungumza na watu kupitia ndoto muulize chochote anakujibu
swali lolote ...karibu Amen
 
Mimi na wewe tunatofauti ambayo mimi naikubali kwani ni dhahili;-

Wewe ni muumini na unasimamia imani yako (believer). Mimi sio muumini ni mtafuta Ukweli (seeker). Usitegemee mtu kama mimi kutegemea maandiko au simulizi tuu bali nitatafuta namna ya kujua kweli ya kile ninachokiamini.

Kuwa na imani kwa kiasi cha kupitiliza hakikujengie makuzi ya kiroho na hasa wakati hata hali ya kiroho huijui. Hebu niambie ikoje?

Ayubu uliyemtaja alikuwa binadamu kama wewe, ameandika aliyoyandika ni baada ya research yake na hiyo ndio ilikuwa conclusion yake. Hatuwezi kumjua Mungu.

Umesahau Yesu wa agano jipya yeye alizaliwa mtakatifu alibarikiwa kuijua njia ya Uzima wa milele amwaminie atamuonyesha nae atamwona Mungu na ataishi milele.

Hao ni watu wawili tofauti na Conclusion mbili tofauti, sasa utamwamini nani? Yesu au Ayubu.

Cha kushangaza sio kwa wewe tuu bali kwa waamini wengi wanazani wao wanahali dhaifu na hawewezi ku question bali wategemee maandiko ya mitume kama akina Ayubu bila wao jiuliza Kwanini Mambo yako kama yalivyo? Nini sababu ya kuzaliwa kwao? Kwa nini wanakufa? Asili yao ni nini? Kama kuna Mungu baasi ni nani na yuko wapi? Anadhamila gani na wao?

Kwa kujiuilza hayo maswali ambayo watu kama wewe unatafuta majibu kwenye biblia au Maandiko. Mimi nakwenda zaidi na ndani ya hapo. Nimetafuta katika kila maandiko Biblia, Bavaghad Gita, Upanishati, Sufis Vendhatta, Hindu philosophy na vingi tuu, lakini nakili kuwa sijasoma Korani na hii ni sababu ya language iliyotumika. Licha ya kusoma vitabu vyote hivyo nilichogundua ni kuwa jibu liko ndani yangu yaani kwenye MIMI.

Tuendelee a e i o u

Asante na naishia hapo.
 
Basi sawa endelea na Bavaghad Gita, Upanishati, Sufis Vendhatta, Hindu philosophy na hivyo vingine utapata maarifa unayoyatafuta πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€
 
Mkuu hapo unajichosha, huyu kiumbe mbishi balaa. Ashanibishia sana kua mama maria alikua na watoto wengine..nikimwambia weka ushahidi haweki
Duh! What a bland, hay bana, soma number 99. Iko kwenye Gospel of Thomas. Maria alikuwa watoto wengine.
 
Mkuu hapo unajichosha, huyu kiumbe mbishi balaa. Ashanibishia sana kua mama maria alikua na watoto wengine..nikimwambia weka ushahidi haweki
Pia soma Luka 8:19-21

19. Hapo mama na ndugu zake Yesu wakamjia, lakini hawakuweza kumkaribia kwa sababu ya umati wa watu.
20. Yesu akapewa habari kwamba mama na ndugu zake walikuwa nje, wanataka kumuona.
21. Lakini Yesu akawambia watu wote, "Mama yangu na ndugu zangu ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika".

Gospel of Thomas hakipo kwenye biblia haya huyo ni Luka kathibitusha. Acha kuwaita watu wabishi kisa hajalubaliana hoja yako. Tuheshimiane.
 
MAKOSHNELI na Tom McCarthy inaelekea hamfanyi reserch ya kutosha yet mnataka nikubaliane na mnayouataka.

MAKOSHNELI hujajibu swali langu ueleze kama unajua kuwa katika roho ni kufanyeje au kukoje? Hebu jibu basi, au wewe ni mchungaji aina ya akina Gwajima. Kujifanya maaskofu wakati hamjasomea theology.

Pia jibu controversal ya Ayubu na Yesu, Mungu hawezi julikana na Njia ya Uzima wa milele ya Yesu ?sasa unatakaje nisikie unjilisti wako Mfu?

Tom McCarthy nilikuwa na kuheshimu sana, ila nimegundua you are empty yaani.
Kitu kidogo sana ambacho kiko kwenye Biblia umeshindwa kusoma na kukiweka wazi leo unaniambia mbishi. Katika uzao wa maria mama aliyebarikiwa kuliko wanawake wote alizaa watoto watakatifu. Niendelee?

Umebandika andiko moja la silent sound i really wanted to contribute what i know about it but, althoung preliminary i did but that is it, i can not do it any more. Kumbe nyie mnapenda muonekane ma star kwenye Janvi. Is not fair, hatupo hapa kushindana tupo ku share our knowledges ambazo tunazipata through different means, imani, kusoma, meditaions, curts, yoga and all kinds of means possible, sasa msitulazimishe kumeza mind set zenu.

Tuelewane.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…