Mbatia asubiri tena huruma ya Rais ajaye apate ubunge wa kuteuliwa. Muda wote alikuwa anapiga domo akiwa Dar wakati akina Mnyika, Tundu Lisu na Mbowe wana ngome zao majimboni.
Mbatia amekuwa mtumwa wa lowassa ( Msukule wa lowassa) ili amsaidie kwenye mbio zake za ubunge huku akijua bila msaada wa Lowassa hawezi shinda. Naamini hivyo kwa Sababu:
1. Mwaka 1995 Mbatia aligombea ubunge akashinda, alishikwa mkono na Augustino Mrema na kuwaambia wana vunjo anaenda kugombea urais ila anawaachia kijana mbatia kuwa mbunge wao.
2. Mwaka 2000 Mbatia alimsaliti Mrema na alipogombea ubunge wana Vunjo walimwambia kama unataka ubunge aende kumwomba Mrema msamaha, kitu ambacho hakufanya kwa hiyo akapigwa chini na wana Vunjo. Pia, tukumbuke 1995 Mrema alipomshika mkono mbatia akipata kura 57,000 ambayo ilikuwa asilia 87 Ya kura zote. Alipomsaliti Mrema 2000 akipata kura 3,400 ambayo ni asilimia 2 ya kura zote.
3. Mwaka 2010 aligombea jimbo la Kawe akapata kura kiduchu akishika mkia kuwa mtu wa tatu, nyuma ya Mdee wa CHADEMA na mgombea wa CCM. Palikuwa hakuna mtu wa kumshika mkono.
4. Sasa 2015 anasubiria huruma ya Lowassa ndio maana habanduki ubavuni kwake na amekuwa msemaji wa CHADEMA huku chama chake cha NCCR kikiwa kinalegalega. Kweli lowassa amemhurimia ndio maana alikwenda Vunjo na kufanya mikutano mitatu Kahe, Kirua Vunjo na Himo. Hakuna jimbo jingine ambapo lowassa amefanya Mkutano zaidi ya mmoja. Lowassa hakufanya Mkutano Moshi mjini, Moshi vijijini waka Rombo.
Alipomaliza mikutano hiyo aliondoka.
Kila mgombea ubunge ameenda kujichimbia kwenye jimbo lake kusaka kura lakini yeye yupo ubavuni kwa Lowassa tu. Mfano Tundu Lissu yupo jimboni kwake anapambana ulitegemea ndio awe msemaji wa Lowassa lakini anapigana kiume jimboni kwake.