TUNTEMEKE
JF-Expert Member
- Jun 15, 2009
- 4,587
- 579
Habari zimevuja kuwa James Mbatia alipewa milioni 50 na Mustafa Sabodo kwa ajili ya kusaidia kampeni za NCCR - MAGEUZI mwaka 2010, lakini hakuzifikisha katika mfumo wa Chama, baada ya kuvuja kwa siri hiyo, baadhi ya viongozi walimfuata Mzee Sabodo ambaye alithibitisha hayo na walipomuuliza Mbatia juu ya hilo akasema ni kweli Sabodo alimpa milioni 20 si kama mchango bali alikikopesha chama na tayari wao na Ruhuza wamekwishamlipa Mzee Sabodo. Waandishi twawaomba mfuatilie suala hili kwa kuwauliza Mbatia, Sabodo na Ruhuza ili kuweka mambo hadharani na kuleta uwajibikaji wa rasilimali za wapenda demokrasia nchini.