ZionTZ
JF-Expert Member
- Oct 6, 2009
- 1,283
- 538
Siku chache baada ya kujifungua mwili wako utaanza kutoa maziwa ya awali(colostrum). Kwa baaadhi ya wanawake maziwa haya huwa mazito na kuwa na rangi ya njano, Kwa wengine ni mepesi na huwa ya maji maji.Maziwa haya ya awali hulinda mwili.
Mfano huzuia bacteria na huimarisha kinga ya mwili, hivyo ni muhimu sana kwa mwanao tofauti na maziwa mengine ambayo si ya mama.Maziwa haya hutiririka taratibu na hii humsaidia mwanao kujifunza jinsi ya kunyonya huku akipumua na kumeza maziwa.
Baadaya siku 3 hadi 4 za kunyonyesha, matiti yako yatazidi kuwa magumu kadri maziwa ya awali yanavyozidi kubadilika na kuwa maziwa ya kawaida.Maziwa hayo yatabadilika ndani ya siku 10 hadi 14 za mwanzo na kuwa maziwa kamili.
Katika kipindi hiki kiwango cha maziwa kitaongezeka ili kukidhi mahitaji ya mwanao.Kiwango cha maziwa hutegemeana na jinsi unavyochochewa kwa jinsi unavyonyonyesha.Hii inamaanisha kwamba mwanao anaponyonya maziwa mengi, mwili pia hutoa maziwa mengi zaidi.
Wanawake waliojifungua kwa njia ya operesheni, inaweza kuchukua muda mrefu maziwa yao kuongezeka. Wakati mwingine bila sababu yoyote inaweza kuchukua siku chache maziwa kuanza kutoka. Hili ni jambo a kawaida kabisa na hutokea pasipo sababu yoyote lakini hakikisha.
unamwambia daktari kuhusiana na suala hili.Ingawa watoto hawatahitaji chochote zaidi ya maziwa ya awali(colostrums) siku chache baada ya kuzaliwa daktari aatakushauri kuhakikisha kwamba mtoto anapata maziwa ya kutosha ikiwa na pamoja na kumuweka motto katika matiti yako kila baada ya masaa mawili hadi matatu.
Endapo maziwa hayajatoka siku tatu baada ya kujifungua unaweza kuongea na daktari wako kuhusu kumpa maziwa mengine kwa muda (hadi hapo maziwa yatakapotoka) ili mwanao apate lishe ya kutosha na asipoteze uzito bila sababu.
Usiogope endapo mwanao atapungua uzito siku za mwanzoni.Watoto wengi hupungua uzito hadi kwa asilimia 7% siku chache baada ya kuzaliwa.
[h=2]Ni wakati gani naweza anza Kunyonyesha?[/h] Ikiwezekana jaribu kuanza kunyonyesha saa moja baada ya kujifungua.Watoto wengi huanza kunyonya hata bia kufundishwa.Baada ya kuamka na kuchangamka motto mchanga utumia muda mwingi kulala kwa kiwango cha angalau masaa 24 hivi.
Hivyo itakuwa vigumu zaidi kumuona akitaka kunyonya saa chache baada ya kuzaliwa.
Hata kama mtoto wako hataki kunyonya ukianza mapema kumnyonyesha itakusaidia wewe na mwanao kujizoeza katika suala zima la kunyonyesha.
Inaweza kuchukua muda kwa mwanao kujua kunyonya vizuri. Lakini mwanao anatakiwa kunyonya akiwa amepanua mdomo na kuingiza sehemu nyeusi ya titi mdomoni(asiingize chuchu peke yake mdomoni).Endapo mwanao atasinzia wakati ananyonya jaribu kumuamusha kwa kumtekenya miguuni au kumvua nguo.
Pia unaweza kumpigia kelele na kumvalisha nepi akiwa ananyonya.
Ili kusaidia kuzoea haraka jaribu kunyonyesha kila baada ya masaa matatu hata wakati wa usiku.Katika hospitali nyingi unaweza kuomba ubaki na mwanao chumbani.Kwa akina mama wanaotaka kupumzika siku chache baada ya kujifungua, mwanao anaweza kulala na wauguzi wakati wa usiku na kuwaomba wakuletee mwanao kipindi cha kumnyonyesha.
[h=2]Je naweza kumnyonyesha mwanangu kwa kutumia chupa?[/h] Kama uko tayari kumnyonyesha mwanao hakuna haja ya kutumia chupa vinginevyo kuwe na sababu ya lazima sana kufanya hivyo.Mwanzoni ni muhimu kumzoesha mwanao kunyonya bila kutumia chupa.Baadhi ya wataalamu wanasema kwamba ukianza kutumia chupa mapema zaidi-kabla hajazoea kunyonya titi-anaweza kushindwa kunyonya na anaweza kupendelea chupa kuliko kunyonya titi.Hata hivyo watoto wengine huweza kunyonya kwa kutumia njia zote mbili.
[h=2]Je nitajuaje kama mwanangu anataka kunyonya?[/h] Ingawa baadhi ya akina mama wanadhani kwamba kulia ni dalili ya njaa, kulia ni dalili ya baadae sana.Unatakiwa kujaribu kumnyonyesha kabla mwanao hajapata njaa kali kiasi cha kukata tamaa na kuwa vigumu kumtuliza.
Dalili zinazoonyesha kwamba watoto wana njaa ni pamoja na;
Imeandaliwa na Dr.Raymond Bandio(MD).
kwa maelezo zaidi na kuuliza maswali na kujibiwa kitaalam tembelea Wanetu.com :: Elimu kuhusu Ujauzito na Uzazi, Malezi na makuzi ya watoto, Afya ya watoto, Saikoljia, Tabia na Haki za Watoto
Mfano huzuia bacteria na huimarisha kinga ya mwili, hivyo ni muhimu sana kwa mwanao tofauti na maziwa mengine ambayo si ya mama.Maziwa haya hutiririka taratibu na hii humsaidia mwanao kujifunza jinsi ya kunyonya huku akipumua na kumeza maziwa.
Katika kipindi hiki kiwango cha maziwa kitaongezeka ili kukidhi mahitaji ya mwanao.Kiwango cha maziwa hutegemeana na jinsi unavyochochewa kwa jinsi unavyonyonyesha.Hii inamaanisha kwamba mwanao anaponyonya maziwa mengi, mwili pia hutoa maziwa mengi zaidi.
Wanawake waliojifungua kwa njia ya operesheni, inaweza kuchukua muda mrefu maziwa yao kuongezeka. Wakati mwingine bila sababu yoyote inaweza kuchukua siku chache maziwa kuanza kutoka. Hili ni jambo a kawaida kabisa na hutokea pasipo sababu yoyote lakini hakikisha.
unamwambia daktari kuhusiana na suala hili.Ingawa watoto hawatahitaji chochote zaidi ya maziwa ya awali(colostrums) siku chache baada ya kuzaliwa daktari aatakushauri kuhakikisha kwamba mtoto anapata maziwa ya kutosha ikiwa na pamoja na kumuweka motto katika matiti yako kila baada ya masaa mawili hadi matatu.
Endapo maziwa hayajatoka siku tatu baada ya kujifungua unaweza kuongea na daktari wako kuhusu kumpa maziwa mengine kwa muda (hadi hapo maziwa yatakapotoka) ili mwanao apate lishe ya kutosha na asipoteze uzito bila sababu.
Usiogope endapo mwanao atapungua uzito siku za mwanzoni.Watoto wengi hupungua uzito hadi kwa asilimia 7% siku chache baada ya kuzaliwa.
[h=2]Ni wakati gani naweza anza Kunyonyesha?[/h] Ikiwezekana jaribu kuanza kunyonyesha saa moja baada ya kujifungua.Watoto wengi huanza kunyonya hata bia kufundishwa.Baada ya kuamka na kuchangamka motto mchanga utumia muda mwingi kulala kwa kiwango cha angalau masaa 24 hivi.
Hivyo itakuwa vigumu zaidi kumuona akitaka kunyonya saa chache baada ya kuzaliwa.
Hata kama mtoto wako hataki kunyonya ukianza mapema kumnyonyesha itakusaidia wewe na mwanao kujizoeza katika suala zima la kunyonyesha.
Inaweza kuchukua muda kwa mwanao kujua kunyonya vizuri. Lakini mwanao anatakiwa kunyonya akiwa amepanua mdomo na kuingiza sehemu nyeusi ya titi mdomoni(asiingize chuchu peke yake mdomoni).Endapo mwanao atasinzia wakati ananyonya jaribu kumuamusha kwa kumtekenya miguuni au kumvua nguo.
Pia unaweza kumpigia kelele na kumvalisha nepi akiwa ananyonya.
Ili kusaidia kuzoea haraka jaribu kunyonyesha kila baada ya masaa matatu hata wakati wa usiku.Katika hospitali nyingi unaweza kuomba ubaki na mwanao chumbani.Kwa akina mama wanaotaka kupumzika siku chache baada ya kujifungua, mwanao anaweza kulala na wauguzi wakati wa usiku na kuwaomba wakuletee mwanao kipindi cha kumnyonyesha.
[h=2]Je naweza kumnyonyesha mwanangu kwa kutumia chupa?[/h] Kama uko tayari kumnyonyesha mwanao hakuna haja ya kutumia chupa vinginevyo kuwe na sababu ya lazima sana kufanya hivyo.Mwanzoni ni muhimu kumzoesha mwanao kunyonya bila kutumia chupa.Baadhi ya wataalamu wanasema kwamba ukianza kutumia chupa mapema zaidi-kabla hajazoea kunyonya titi-anaweza kushindwa kunyonya na anaweza kupendelea chupa kuliko kunyonya titi.Hata hivyo watoto wengine huweza kunyonya kwa kutumia njia zote mbili.
[h=2]Je nitajuaje kama mwanangu anataka kunyonya?[/h] Ingawa baadhi ya akina mama wanadhani kwamba kulia ni dalili ya njaa, kulia ni dalili ya baadae sana.Unatakiwa kujaribu kumnyonyesha kabla mwanao hajapata njaa kali kiasi cha kukata tamaa na kuwa vigumu kumtuliza.
Dalili zinazoonyesha kwamba watoto wana njaa ni pamoja na;
- Kugeuza kichwa huku na huko
- kuachama
- kuweka mikono mdomoni
- Kukunja mdomo kama anayetaka kunyonya
- kujinyoosha
- kujisogeza karibu na matiti mama
Imeandaliwa na Dr.Raymond Bandio(MD).
kwa maelezo zaidi na kuuliza maswali na kujibiwa kitaalam tembelea Wanetu.com :: Elimu kuhusu Ujauzito na Uzazi, Malezi na makuzi ya watoto, Afya ya watoto, Saikoljia, Tabia na Haki za Watoto