Maxmalipo, Samsung, hamjawatendea haki Tecno

kimpe

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2012
Posts
911
Reaction score
862
Habari zenu wakuu,

Naomba niingie moja kwa moja kwenye huu uonezi wa kibiashara unaofanywa na hawa Max Malipo wakiwa kama wakala wa kuuza simu za Samsung.

Kuna tangazo lao linaonekana kwenye Runinga likimuonyesha mwanadada mmoja akimwambia mkaka 'Wewe mpaka leo unatumia simu zisizofaa?' Yule kaka amekaa juu ya ya Bodaboda ameshika simu wameonyesha mpaka brand yake kabisa ni Tecno.

Nimeshindwa kupata picha lakini wanajamvi kwa hili sio sawa kibiashara. Waswahili wanasema ''Kimfaacho mtu chake".

Hata kama Tecno ndo hivyo hawakupaswa kuwafanyia vile.

Wahusika waliangalie hili kwa undani.. Sio sawa
 
Ubora wa Tecno ni sawa sawa au hata zaidi ya Samsung, ila tatizo letu wabongo tunameza sana. Kamata Phantom Z ndio utajua what I mean here. Samsung ni very expensive for nothing.

Tecno hawalingani na Samsung, CHIEF MKWAWA atakufafanulia
 
Last edited by a moderator:
Hilo sio tatizo ni kuwachorea wenzao walitakiwa kujipima ubavu na kina i phone sio kuwafanyia hvo tecno

Kwani we ukiona lile tangazo unadhani wanatangaza nini?
Pale wanawaambia wenye simu ambazo sio kubwa kama samsung waende wakanunue za samsung, iphone iko level nyingine
 
Kwani we ukiona lile tangazo unadhani wanatangaza nini?
Pale wanawaambia wenye simu ambazo sio kubwa kama samsung waende wakanunue za samsung, iphone iko level nyingine
we unavyodhani inaruhusiwa kufanya hivyo kutumia jina bidhaa ambayo mko pamoja kwenye soko. Kwa kuiponda
 
we unavyodhani inaruhusiwa kufanya hivyo kutumia jina bidhaa ambayo mko pamoja kwenye soko. Kwa kuiponda


Sio sahihi habisa kufanya hivyo. Hairuhusiwi kuonyesha brand zingine pindi unapojitangaza. Kama Samsung wanajitangaza basi watumie mbinu mbadala na kuhakikisha wanaficha brand ya simu nyingine.
Kwa njia hiyo tecno wanaweza kabisa kuwa sue hao maxmalipo/samsung.
 
Hilo sio tatizo ni kuwachorea wenzao walitakiwa kujipima ubavu na kina i phone sio kuwafanyia hvo tecno
Soko la samsung hapa TZ limeathiriwa sana na TECNO na hali inazidi kuwa mbaya kwao..lazima wajitutumue sana. Hali ya maisha ngumu kwanini nikanunue samsung kwa bei ghali while kuna TECNO yenye application na uwezo zaidi ya samsung kwa bei ya kiungwana.
 
hawakuwa sawa hata hivo Tecno is too low mkuu!!
 
Hahahaa, wamejilinganisha na TECNO sababu hivyo ndiyo viwango vyao! Mwisho wa simu ni iPhone tu, Samsung ni waigizaji, wanatengeza matakataka na kuwasokomeza watumiaji....jinga sana! Hata waigeje kwa iPhone watangoja sana, Samsung simu za wanafunzi na mamburula!
 
Wabongo bhana, mtu kapanga, anapanda daladala kila siku, mlo mara mbili au moja, kijijini kwenu hata bati umeshindwa kuwanunulia wazee wako, chumba chenyewe ulichopanga hata marafiki kuwapeleka unaona aibu, leo hii unasema Tecno is inferior, too low, haina hadhi. Hizi tabia za kimaskini tuziache we kama unaona haikufai n wewe lakini usikashifu wengine wakati unaishi kwa kujionyesha tu.

Note: walengwa wanajijua sio wote.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…