Maxcom Africa yatolea ufafanuzi tiketi zisizo za kielektroniki kwenye Mwendokasi. Yafungua kesi ya Madai dhidi ya UDA-RT

Kunguru Mjanja

JF-Expert Member
Aug 22, 2012
2,036
3,929
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Ufafanuzi juu ya utoaji wa huduma ya Ticketi za kielektroniki kwenye Mradi wa mabasi ya mwendo kasi.

Kampuni ya Maxcom Africa PLC ni mmoja kati ya wabia wanaoshiriki katika utoaji huduma katika Mradi wa uendeshaji wa Mabasi ya mwendo kasi Jijini Dar es Salaam, Kazi ambayo ilianza mnamo tarehe 16 Mei 2016 pindi tu Mradi huu ulipozinduliwa katika awamu ya Kipindi cha mpito (Interim period).

Kuanzia tarehe 13 Aprili 2018 kumekua na hali ya sintofahamu katika vituo vya Mwendo kasi, na kumekuwapo na uuzwaji wa tiketi za karatasi (za vishungi) ambazo hazitolewi kwenye mfumo wa Tiketi za Kielektroniki ulioidhinishwa na wasimamizi wa mradi huu (DART Agency), na pia kumekuwapo na nyakati ambazo abiria wanasafirishwa bila kulipa nauli.

Tunaomba ifahamike kwamba haya yanayoendelea yanaratibiwa na kampuni ya UDA-RT ambayo mbia wake mkubwa ni Simon Group ambao wanamiliki mabasi haya ya Mwendokasi. Maxcom Africa PLC waliingia mkataba kutoa huduma ya tiketi za kielektroniki katika mradi huu wa Mwendokasi chini ya kampuni ya UDA-RT kutokana na maagizo yaliyotolewa na serikali.

Kutokana na Mkataba huo Maxcom Africa PLC tuliweka Mifumo, Rasilimali watu, teknolojia na wasimamizi katika mradi huu. Ila katika hali isiyo ya kawaida tangu mradi huu umeanza Kampuni ya UDA-RT imeshindwa kuilipa kampuni ya Maxcom Africa PLC gharama za uendeshaji, uwekezaji na hata stahiki za wafanyakazi (ikiwamo michango ya hifadhi za jamii na tiba) hivyo mnamo Februari 2017 kampuni ya Maxcom Africa PLC tuliamua kufungua kesi ya madai katika Mahakama kuu ya Tanzania, Kesi ambayo mpaka sasa inaendelea kusikilizwa.
Kwa zaidi ya Miaka 2 sasa UDA-RT wamekua wakikwepa kulipa stahiki hizi za wafanyakazi, japo Maxcom imeendelea kutoa huduma iii kulinda heshima ya Mradi na nchi yetu.


Mnamo tarehe 13 Aprili 2018 UDA-RT walitangaza kuiondoa kampuni ya Maxcom Africa kwenye mradi na kuipa kazi kampuni ya TTCL corporation bila kufuata taratibu zozote za kimkataba, bila kutoa notisi na bila kurasimishana makabidhiano ya mradi.

Hivi karibuni UDA-RT wametumia nguvu kuwatisha na kuwatoa wafanyakazi waliokuwa wanatoa huduma ya tiketi za kielektroniki katika vituo vya Mwendokasi, bila kufuata taratibu zilizoainishwa kwenye mikataba ya ajira, hii ikiwa ni pamoja na kuwalazimisha wafanyakazi wa Maxcom Africa PLC kuvunja Mikataba yao ya ajira na kampuni ya Maxcom Africa PLC na kusaini mikataba mipya na kampuni ya UDA-RT iii waweze kuendelea kufanya kazi.


Sisi kama Maxcom Africa PLC tunaamini haya yanayofanywa na UDA-RT ambaye mbia wake mkubwa ni Simon Group hayana nia njema kwa taifa hili, hayana nia njema kwenye mradi huu wa usafiri wa Mwendokasi, na pia hayana nia njema kwenye maendeleo ya Nchi yetu.Ni Dhahiri haya yanaweka doa katika mradi huu na yanaweza kuleta mazingira ya ufisadi na dhuluma hasa ikizingatiwa kesi ya Madai ipo Mahakamani.

Tunawaomba Watanzania na Umma uelewe kwamba huduma inayotolewa katika vituo vya mwendo kasi isiyohusisha tiketi za kielektroniki inatolewa na UDA-RT na sio Maxcom Africa PLC.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma
======

Tiketi zinazotolewa na UDA-RT hizi hapa
1.jpg
2.jpg
 
Mafisadi ni sawa na majambazi tu
Lazima inafika wakati wanadhulumiana na kutofautiana.

Simon Group na Maxcom ni walewale.

Shirika lenyewe la UDA wamechukua kimagumashi halafu hawa maxcom si ndo wale walishiriki kulazimisha watu kununua EFD feki kwa bei za juu mara tatu ya bei halali?

Bora wote mfe na biashara zenu mshakula sana keki ya taifa acheni wengine nao wapige pesa . Kila zama na mafisadi wake pisheni tu kwa amani
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Ufafanuzi juu ya utoaji wa huduma ya Ticketi za kielektroniki kwenye Mradi wa mabasi ya mwendo kasi.

Kampuni ya Maxcom Africa PLC ni mmoja kati ya wabia wanaoshiriki katika utoaji huduma katika Mradi wa uendeshaji wa Mabasi ya mwendo kasi Jijini Dar es Salaam, Kazi ambayo ilianza mnamo tarehe 16 Mei 2016 pindi tu Mradi huu ulipozinduliwa katika awamu ya Kipindi cha mpito (Interim period).

Kuanzia tarehe 13 Aprili 2018 kumekua na hali ya sintofahamu katika vituo vya Mwendo kasi, na kumekuwapo na uuzwaji wa tiketi za karatasi (za vishungi) ambazo hazitolewi kwenye mfumo wa Tiketi za Kielektroniki ulioidhinishwa na wasimamizi wa mradi huu (DART Agency), na pia kumekuwapo na nyakati ambazo abiria wanasafirishwa bila kulipa nauli.

Tunaomba ifahamike kwamba haya yanayoendelea yanaratibiwa na kampuni ya UDA-RT ambayo mbia wake mkubwa ni Simon Group ambao wanamiliki mabasi haya ya Mwendokasi. Maxcom Africa PLC waliingia mkataba kutoa huduma ya tiketi za kielektroniki katika mradi huu wa Mwendokasi chini ya kampuni ya UDA-RT kutokana na maagizo yaliyotolewa na serikali.

Kutokana na Mkataba huo Maxcom Africa PLC tuliweka Mifumo, Rasilimali watu, teknolojia na wasimamizi katika mradi huu. Ila katika hali isiyo ya kawaida tangu mradi huu umeanza Kampuni ya UDA-RT imeshindwa kuilipa kampuni ya Maxcom Africa PLC gharama za uendeshaji, uwekezaji na hata stahiki za wafanyakazi (ikiwamo michango ya hifadhi za jamii na tiba) hivyo mnamo Februari 2017 kampuni ya Maxcom Africa PLC tuliamua kufungua kesi ya madai katika Mahakama kuu ya Tanzania, Kesi ambayo mpaka sasa inaendelea kusikilizwa.
Kwa zaidi ya Miaka 2 sasa UDA-RT wamekua wakikwepa kulipa stahiki hizi za wafanyakazi, japo Maxcom imeendelea kutoa huduma iii kulinda heshima ya Mradi na nchi yetu.


Mnamo tarehe 13 Aprili 2018 UDA-RT walitangaza kuiondoa kampuni ya Maxcom Africa kwenye mradi na kuipa kazi kampuni ya TTCL corporation bila kufuata taratibu zozote za kimkataba, bila kutoa notisi na bila kurasimishana makabidhiano ya mradi.

Hivi karibuni UDA-RT wametumia nguvu kuwatisha na kuwatoa wafanyakazi waliokuwa wanatoa huduma ya tiketi za kielektroniki katika vituo vya Mwendokasi, bila kufuata taratibu zilizoainishwa kwenye mikataba ya ajira, hii ikiwa ni pamoja na kuwalazimisha wafanyakazi wa Maxcom Africa PLC kuvunja Mikataba yao ya ajira na kampuni ya Maxcom Africa PLC na kusaini mikataba mipya na kampuni ya UDA-RT iii waweze kuendelea kufanya kazi.


Sisi kama Maxcom Africa PLC tunaamini haya yanayofanywa na UDA-RT ambaye mbia wake mkubwa ni Simon Group hayana nia njema kwa taifa hili, hayana nia njema kwenye mradi huu wa usafiri wa Mwendokasi, na pia hayana nia njema kwenye maendeleo ya Nchi yetu.Ni Dhahiri haya yanaweka doa katika mradi huu na yanaweza kuleta mazingira ya ufisadi na dhuluma hasa ikizingatiwa kesi ya Madai ipo Mahakamani.

Tunawaomba Watanzania na Umma uelewe kwamba huduma inayotolewa katika vituo vya mwendo kasi isiyohusisha tiketi za kielektroniki inatolewa na UDA-RT na sio Maxcom Africa PLC.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma
======

Tiketi zinazotolewa na UDA-RT hizi hapa
View attachment 755729 View attachment 755730
Na TTCL watoa tamko lao pia. Weka kwenye main page hapo juu. Kunguru Mjanja.
20180424_190805.png
 
Duuuh! Kuna harufu mbaya hapa kwa upande wa UDART. TTCL yeye kazi yake sio kutoa tiketi bali ni network tu. Maxcom aliyekuwa anatoa huduma ya tiketi anafukuzwa! Ni ajabu!
 
Jamani huyu Maxcom ni Mtanzania mwenzetu. Siutaratibu ufuatwe tu ili tusivunje moyo watu wetu. Hata kama kuna makosa huko nyuma ni vyema yakasahihishwa kwa utaratibu.
 
kwa maana hiyo wanakwepa kodi kwa kutoa tiketi hizo za magumashi kama za daladala. kwa maxcom wameona genuineness ya kodi hivyo kukwepa wanarudi kwenye makaratasi.
 
Kutokana na Mkataba huo Maxcom Africa PLC tuliweka Mifumo, Rasilimali watu, teknolojia na wasimamizi katika mradi huu. Ila katika hali isiyo ya kawaida tangu mradi huu umeanza Kampuni ya UDA-RT imeshindwa kuilipa kampuni ya Maxcom Africa PLC gharama za uendeshaji, uwekezaji na hata stahiki za wafanyakazi (ikiwamo michango ya hifadhi za jamii na tiba) hivyo mnamo Februari 2017 kampuni ya Maxcom Africa PLC tuliamua kufungua kesi ya madai katika Mahakama kuu ya Tanzania, Kesi ambayo mpaka sasa inaendelea kusikilizwa

  1. Watakwambia suala likiwa mahakamani hupaswi kulizungumza kwingine kokote
  2. Pamoja na changamoto za hapa na pale, Maxicom mlifanya kazi nzuri sana, je zile kadi tulizonunua ndiyo zimefia hapo au zitaendelea kwa sura nyingine
 
Nimepanda UDART Leo na nimeshangaa kupewa hizo tiketi.Kama wataendelea hivi tutarajie hili Shirika kufa muda sio mrefu.Tiketi zenyewe ni rahisi sana kufojika.UDART wategemee mapato kushuka mpaka hiyo kampuni mpya Irudie mfumo wa Kielectronic.Hapo wametengeneza mwanya wa watu kupiga hela!
 
Hivi TTCL ni shirika la serikali au shirika la umma? Huyu afisa habari vipi?

Hili tatizo naliona kama limetengenezwa ili atoke huyu aingie huyu
Mkuu kwani nini utofauti kati ya shirika la umma na shirika la serikali?. Umma ndiyo mmiliki wa was vyote vinavyosimamiwa na serikali. Ikulu, mahakama, bunge, vyuo vikuu, hospital I za serikali kama muhimbili nk yote ni Mali ya umma bosi serikali ni msimamizi tu was Mali za umma.
 
Mkuu kwani nini utofauti kati ya shirika la umma na shirika la serikali?. Umma ndiyo mmiliki wa was vyote vinavyosimamiwa na serikali. Ikulu, mahakama, bunge, vyuo vikuu, hospital I za serikali kama muhimbili nk yote ni Mali ya umma bosi serikali ni msimamizi tu was Mali za umma.
Mwisho umesema kweli. Serikali ni 'agent' tu siyo mmiliki. Srrikali zinabadilika lakini mali za umma zinatakiwa kuwepo kwa manufaa ya umma. Serikali ikishindwa kuzisimamia sawa tuna haki kuiondoa.
 
Yaani Mimi ni Tomaso kwelikweli sijui Dart,Udart,Brt, simoni group,sijui ttcl huu mlolongo wote ni wa wizi tu

Haya matatizo yenu mngefanyia background sio had kina sisi matomaso tujue sisi tunataka Usafiri bora na tiketi zipatikane vizuri basi
 
Sasa wao walikuwa wameridhika wafanyakazi wao kutokulipwa stahiki zao kwny mifuko ya jamii,lkn cha ajabu baada ya kusitishiwa mkataba ghafla ndio wanasema yote hayo. Sheria zifuatwe kulinda maslahi ya wafanyakazi
Tangazo lao lasema walifungua kesi hiyo ya madai februari 2017, soma vizuri.
 
Back
Top Bottom