Mawaziri wa Magufuli maji mazito au mgomo baridi?

mr gentleman

JF-Expert Member
Aug 1, 2012
3,223
4,679
Wanasema ukitaka kujua uhondo wa ngoma basi ingia uicheze. Na wengine wanasema mpira unakuwa mrahisi sana ukiwa nje ya uwanja, ishu inakuja ukipewa jezi uonyeshe uwezo wako..

Mawazo yangu ni kuhusu serikali ya Magufuli. Magufuli kama Magufuli hana shaka anajulikana uwezo wake kiutendaji na kufatilia mambo. PM Kassim Majaliwa na yeye moto wake unaonekana ni mfuatiliaji wa mambo na mpiganaji wa kweli.

Ishu ipo kwa mawaziri wa Magufuli. Kiukweli wengi mimi bado hawajanivutia wala kunishawishi. Wameshindwa kabisa kukata kiu ya matarajio yetu kwao.

Najua wengine watajitetea kwamba wanakosa bajeti labda tusubirie bajeti au wana visingizio lukuki lakini kwa kweli kuna vitu haviitaji bajeti wala mabadiliko ya kisera.

Mfano Prof Ndalichako mpaka sasa sijaona alichofanya kikubwa kusimamia elimu yetu especially elimu ya msingi na secondary. Nchi bado ipo kwenye mataifa mawili ya kielimu ilihali mtaala ni mmoja. Kuna shule zina term tatu na kila term ina ada yake na kuna shule zina term mbili kwa mwaka. Kuna shule zina walimu hawana ata cheti kimoja, kuna shule zipo sebuleni, kuna shule wanaajiri walimu wa mpaka wa civics kutoka nje ya nchi. Waziri yupo idara ya ukaguzi ipo. Hakuna jipya.

Waziri wa kilimo Mwigulu naona anapiga ziara tu mkoa baada ya mkoa. Matatizo ya kilimo bado hayana majawabu. Kuna vitu kama connection za masoko kwa wakulima haviitaji kusubiri bajeti kuu Waziri angeweza kuanza na hili kama kuna vingine anasubiri.

Wizara ya kazi, ata Waziri nimesahau tayari. Hizo recruitment agencies bado zinatesa waajiriwa huko kuna unyonyaji wa hatari na Waziri yupo tu anafanya ziara. Hakuna kulinda ajira za wazawa yalifanyika maigizo ya wiki mbili kiwanda cha Dangote na godown la wachina baada ya hapo ni business as usual Mavunde pumzi imekwisha.

Wizara ya mazingira inayoongozwa waziri anayesemekana ni smart sana mpaka sasa hatujaona innovation yoyote kutunza mazingira na kusimamia usafi. January anatuangusha nae.

Waziri wa mambo ya ndani. Kitwanga nafikiri anashindwa tu kusema kazi imemzidi uwezo. Uhamiaji huko ni rushwa kwenda mbele. Polisi wa barabarani ni mrija wa rushwa. Yani huyu ndio mpaka namuonea huruma.

Maghembe ni mtu aliyepewa wizara ya leo wakati yeye anaishi jana. Pale zaidi ya kukamata majangili sijui ana ubunifu gani kufanya utalii utishe Tanzania na Africa kwa ujumla.

Kigwangwala na Ummy wanajitahidi japo bado wameshindwa kuri address tatizo.

Kuna huyu Makame Mbalawa namuona kama nae mfuatiliaji hivi.

Nape siasa nyingi utendaji kisoda. Mara wasanii watalipwa mpaka leo kimya. Mara bongo movies watalindiwa kazi zao na tra kimyaaa. Mara TFF watatoza kwa electronic. Huko kwenye michezo ndio sioni chochote anachofanya.

Kwa kweli mawaziri wanaotakiwa wajipange haswa. Maana Magufuli amekuwa kama one man army mawaziri nao wanamshangaa badala ya kumsaidia.

Na kuna mawaziri wanaonekana kama wana uwezo wa kufanya makubwa ila tatizo sijajua ni nini mpaka nahisi kuna kamgomo baridi au hii aina mpya ya kuongoza hawajaipenda.


Ni bora ata ya Makonda anafanana na kasi ya Magufuli.

Uccm na Uchadema pembeni wenzangu mnawaonaje awa mawaziri.
 
Mungu mwenye nguzu zote na uwezo wote tunaambiwa aliunda dunia kwa siku sita.

Hujawahi kujiuliza kama Mungu ana nguvu zote na uwezo wote kwa nini hakuunda dunia kwa milisecond achilia mbali dakika moja?

Ukipata jibu, rudi tena tuanze mjadala.

NOTE: Sahamani kama huamini kuna Mungu au huamini kama Mungu aliunda Dunia kwa siku sita!
 
Mungu mwenye nguzu zote na uwezo wote tunaambiwa aliunda dunia kwa siku sita.

Hujawahi kujiuliza kama Mungu ana nguvu zote na uwezo wote kwa nini hakuunda dunia kwa milisecond achilia mbali dakika moja?

Ukipata jibu, rudi tena tuanze mjadala.

NOTE: Sahamani kama huamini kuna Mungu au huamini kama Mungu aliunda Dunia kwa siku sita!

Mkuu nimekuelewa... Na ndio maana nikasema kuna mambo hayaitaji mlolongo kuyafatilia au kuyasimamia. Na hayo bado hatuoni mawaziri wakiangaika nayo. Wapo wapi? Kero ni nyingi sana waanze kuzipunguza.
 
Mbalawa anajitahidi sana kufuatilia. Kama ni marks ku score yuko na B+. Aongeze bidii. Jitihada zake zinaonekana na kweli anaonekana kuwa na nia ya dhati. Pia waziri wa afya na naibu wake wanajitahdi ila wanahitaji wakae na wataalam wawape mikakati mizuri. Wao wame score B. Prof muhongo, naona kama kasi aliyokuwa nayo imepungua ukilinganisha na kwamba wizara yake ndo imebeba issue sensitive sana kwenye rasilimali zetu. Mi nadhani, muonge saiz ana score C, inabidi apandishe kiwango walau kwa kuanza na ile mikataba 18 ya gas iliyosainiwa na China wakati wa utawala wa jk. Kwenye hili asisubiri Rais ndo aanzishe. Aanzishe yeye na ripoti ampelekee Rais, maana liko ndani ya uwezo wake.
 
Waziri lukuvi namuona kama anapambana haswa, nadhani anastahiki some credits here ukizingatia pia wizara yake ina madudu ya hatari, don't forget him.
 
Hao mawaziri hawajui tatizo la Tanzania ni nini hasa.

Kila wizara ingeandaa master plan ya miaka mitano ili kufikia malengo ambayo Magufuli anayataka.

Huyo waziri wa kilimo ndio namuonea huruma sana.
 
Hao mawaziri hawajui tatizo la Tanzania ni nini hasa.

Kila wizara ingeandaa master plan ya miaka mitano ili kufikia malengo ambayo Magufuli anayataka.

Huyo waziri wa kilimo ndio namuonea huruma sana.
Waziri wa kilimo anapiga route mikoani kutafuta kura za uraisi 2025
 
Serikali inapokuwa mpya mchecheto unakuwa mkubwa lakini kadri Muda unavyosogea tutawajua wenye malengo kutekeleza ilani ya Chama
 
Waziri wa afya wanatoa amri kwa hospital moja moja badala ya kufanya hivyo kwa hospital zote. Tatizo la hospital moja yanafanana karibia hospital zote nchini.
 
Waziri wa mazingira, mh marope anatakiwa aweke sera za kuboresha usafi kwenye vijijini, miji na majiji. Hii staili ya kila mwisho wa mwezi kufanya usafi sio endelevu. Waweke sera nzuri, na ikibidi suala la usafi kwa wanaochafua mazingira kwa makusudi iwepo kodi. Lkni vitendea kazi kama dust
 
Wala sio kwamba wana mgomo baridi; ni woga wa ushauri na maamuzi kwenye uwanja huu mpya wasasa ambapo kazi ya rais imechanganywa na kazi zao! Kocha mchezaji mara nyingi huchanganya wachezaji na hivyo kuwafanya wasahau kabisa mfumo! Rais atakapowaacha huru kikazi na kuwaamini katika maamuzi na ushauri ndio utakuwa wakati sahihi wa kuwapima. Ukiwapima mawaziri sasa utakuwa unawaonea!
 
Waziri wa mazingira, mh marope anatakiwa aweke sera za kuboresha usafi kwenye vijijini, miji na majiji. Hii staili ya kila mwisho wa mwezi kufanya usafi sio endelevu. Waweke sera nzuri, na ikibidi suala la usafi kwa wanaochafua mazingira kwa makusudi iwepo kodi. Lkni vitendea kazi kama dust
Waziri wa mazingira, mh marope anatakiwa aweke sera za kuboresha usafi kwenye vijijini, miji na majiji. Hii staili ya kila mwisho wa mwezi kufanya usafi sio endelevu. Waweke sera nzuri, na ikibidi suala la usafi kwa wanaochafua mazingira kwa makusudi iwepo kodi. Lkni vitendea kazi kama dust

Hayo uliyosema yote anaweza kufanya na zaidi ya hayo ndio maana wengine tunajiuliza nini kinamkwamisha.
 
Hivi waziri Lukuvi (Ardhi) kuamuru/kupiga marufuku Kwa wenye Nyumba kutoza kodi za miezi sita /mwaka nayo inahitaji bajeti au bunge ?!
 
nchemba ulitaka akae ofisini wizarani!wafugaji na wakulima wamfate DAR ?
 
Back
Top Bottom