Mawaziri kujiuzuru

Naona kama 2015 ni mbali sana.
Issue siyo mawaziri kujiuzulu au rais kufanya mabadiliko.
Issue ni kuiondoa serikali ya wezi wa mali ya umma.
Kikwete mwenyewe mtuhumiwa mkuu, mnategemea awateue akina nani mbadala?
Unless mtuambie wabunge ndiyo watakao wateua mawaziri
 
Wabunge wa ccm
kamwe hawawezi kukata tawi walilokalia. Nani atawadaka watakapofika chini? Kama kuna machozi yatakuwa ya mamba tu.
 
Tena huyo Filikunjombe mnafk sna! kachukua mashuka ya bima ya afya anagawa hosptalin halaf anaita media.2015 hana chake.
 
deo filikunjombe nilimwona kupitia ITV akitoa msaada wa madawa na mashuka jimboni kwake kuna hali mbaya sana msaada aliotoa hauendani na hadhi yake leo anawabwekea wenzake anapata wapi haki hiyo? aache cheap politics bhana.

Huyo mbunge wetu mumwache kwani amekuwa msaada kwenye jimbo letu. Na huo msaada ametoa mkubwa sana kwani mashuka waliokuwa wanatumia yalikuwa yamechakaa sana, wacha kurudisha moyo wa mbunge nyuma.
 
Kibananhukhu,

..Deo atafute mbinu za kuwawezesha wapiga kura wake waweze kujitegemea na siyo kusubiri misaada toka kwa mbunge.

..kwa kuanzia angewasaidia kupata mafunzo na teknolojia ya kuongeza thamani ya mazao wanayozalisha.

Kamanda, hiyo unayosema awafundishe kufanya value addition kwenye mazao yao, watafanya value aadion kwenye makaa ya mawe na chuma? Hata hivyo mbona makaa yote na Chuma cha Ludewa wamempa mshikaji wao Subash Patel!!!
 
Kujiuzulu kwa mawaziri haitoshi, inatakiwa wauawe kwa kupigwa za kichwa iwe mfano.
 
Yote hii ni Usanii tu , kelele nyingi hadi kukamaa misuli ya shingo, lakini baada ya hapo mambo yataendelea kama yalivyokuwa. Suluhisho: tufanye kama Misri au Tunisia.
 
Ni kutoka katika vikao vya ndani ila wanaona kuwa wameonewa wanataka waondolewe kwa njia ya mabadiriko ya baraza la mawaziri kuondoa aibu



Wanataka waondolewe au wanatakiwa wafungwe mpaka kamba zikatike
 
Hao wanapiga kelele kwasababu hawajapewa hizo nafasi, wakipewa watafanana tu na hao, Hizo ni chuki na bifu kati yao, Magamba wameoza wameshindwa kusimamia serikalini matokeo yake wajanja ndio wanafaidi hii NCHI. Hakuna hata Mmoja mwenye nafuu, wanapigia kelele wizi wakati na wao wanapata mgao, rushwa wakati wao wanatoa na kuchukua, ukweli uko wapi? Ni wasanii watupu. Uchaguzi wa Ubunge wa EAC wamepokea rushwa leo hii wanajifanya eti wanauchungu na INJI HII, Afadhalia Mzee wa Kilalacha yeye alikuwa anapiga kazi akizitamani anakuitwa Moshi ANAVUTA mkwanja . Hawa wanakula mpaka mbegu Wataua kabisa.
 
Katika hali isiyo ya kawaida kutokana na upepo unaovuma ndani ya bunge kuhusu kutokuwa na imani na waziri Mkuu Pinda inawezekana serikali ya CCM haitokuwa tayari kukubali kwa mara nyingine kuvunja bunge baada ya bunge kupiga kura ya kutokuwa na Imani na Waziri mkuu.

Hapa naona serikali lazima itawashinikiza mawaziri waliotajwa kusababisha au kutumia pesa za serikali hovyo kujiuzuru/kuondoka madarakani ili kuepuka aibu nyingine baada ya ile ya Richmond.
 
Mmmh, sijui lakini! Maana tayari kuna taarifa za chini kwa chini zinazodai mtoto wa mkulima ameamua kuachia ngazi. Sasa sijui hii itakuwaje. Pengine tusubiri tuone kesho asubuhi waziri mkuu atasema nini.
 
Wakurogwa kweli umerogwa mimi nilifikiri tayari wameshajiuzuru au watajiuzuru.

Nijuavyo mimi najua mawaziri hao hawatajiuzuru kwa maana CCM ina uhakika na kushinda kura endapo itapigwa kutokana na wingi.
 
lakini si mpaka zipatikane saini 70 wabunge?
nina uhakika wa kupatikana kwa saini 40 s za cdm lakini zilizo bakia sijui
 
Wakurogwa kweli umerogwa mimi nilifikiri tayari wameshajiuzuru au watajiuzuru.

Nijuavyo mimi najua mawaziri hao hawatajiuzuru kwa maana CCM ina uhakika na kushinda kura endapo itapigwa kutokana na wingi.
kura zikipigwa za siri anaweza kung'oka tu
 
lakini si mpaka zipatikane saini 70 wabunge?
nina uhakika wa kupatikana kwa saini 40 s za cdm lakini zilizo bakia sijui

Kuna ya Kafulila na zingine chache kutoka CCM. Mrema huyo hawezi. Labda Hamad Rashid anaweza kujitutumua
 
Hiyo ndoano kama ya Lema, wananchi wanfuatilia so wabunge wa ccm wakiwalinda mawaziri wao CDM inapata agenda ya kwenda kwa wananchi kuendeleza libeneke........wawe wazarendo na wise au PEOPLESSSSSSSSSSSS ndo wanaipalilia
 
Kura ikipigwa,trust me pinda anaondoka,tambua kuwa kabla ya Zito kutamka hivyo ni lazima ana back up ya wabunge wa magamba hushangai hakukuwa hata na mwongozo!ni bora mawaziri wajiuzuri,kuunda baraza jipya kanchi kenyewe kako hoi kiuchumi,tutafunga mikanda ya shingoni na sio kiunoni
 
Back
Top Bottom