maumivu makali yanatesa moyo wangu

maumivu makali yanatesa moyo wangu

Pole sana kaka Limbert :

Kitendo cha kukubaliana na wenzako kuwa ni kazi ya Mungu ni hatua ya kwanza kwenda kwenye uponyaji. Ni kawaida kabisa ukifiwa na mwenza upitie kipindi cha "grief" / 'Mourning'na ndicho unapitia sasa. Kipindi hiki huchukua muda tofauti kulingana na mazingira, ukaribu wako na mwenza aliyetangulia nk ila napenda kukushauri tu

  • Mshukuru Mungu aliyekupa muda ya kuwa na mpenzi wako (cherish the moments you had spent and thank God)
  • Kama una watoto - kuwa nao karibu ,na wasione moyo wako umekata tamaa maana wewe ndio muhumili wao daima
  • Mwambie Mola wako kweli yote kuwa unaumia na ni kwa neema tu ndio utaweza- kama kuna vikundi vya ibada/ maombi au counseling groups unaweza kuhudhuria kupata ushauri zaidi
  • Jumuika na jamii kwa kiasi : kama ulikuwa mpenzi wa mpira basi angalia au hudhuria mechi, tamasha la muziki nk
  • Kikubwa - Jiamini kuwa Mungu atakupitisha yote - maumivu kweli yapo kwakuwa tu binadamu ila kila sononi ijapo jipe moyo na jiambie nafsi yako kuwa nitaweza kuendelea mbele maana ni Lazima kipindi cha grief kipite ili uendelee mbele na maisha yako.
Nakutakia neema za Mungu tele katika kupita katika kipindi kigumu.

mkuu ufaham wako ukojuu. maneno yako yageuke kuwa MAOMBI iwe NEEMA Kwangju.Hekima ya MUNGU iwenawewe daima.
 
pole mkuu katika kipindi kigumu ulicho nacho. Hakuna njia mbadala zaidi ya kumtegemea Mungu na sali sana ili upate faraja ya kweli,Mungu wetu ni mwema soon hy hali itapotea maana wewe ukiwa hivyo na watoto watakuwa kwenye hali gani?

Nimekubali ushauli wako kiongozi .ukwelinikwamba nilikuwambali sana nikawa najiuliza kwanini watu wanakufa.?
 
Aaa nikweli ! hata mm kabula ningeweza kusema kama unavyosema lakini. ukisikia mtu anamsema mtu kuwaalibahatisha juwa huyomtu anahitaji msaada , unahitajimusaada kilashauli huwezikushauri wapo wanaoweza fatilia utajifunza. AMANI IDUM PAMOJA NAWE Kuanziasasa nazaidi.

Punguza speed unapokuwa unaandika ili uandike maelezo yanayoeleweka

Kuhusiana na nilichokushauri tanbua kuwa nimekushauri kile ninachoona mimi ni sahihi na unaweza kuacha kama unakiona hakifai

Lakini nakuambia kuwa wewe hujitendei haki na hata huyo mpendwa wako aliyetangulia mbele ya haki humtendei haki pia

Unaweza kuwa unatamani upewe ushauri uliokuwa unautarajia wewe lakini huo sio ushauri unaostahiki

Chukulia mfano mgonjwa wa malaria huwa ana kawaida ya kupenda kuota jua kali na hicho ndicho anachokifurahia,je yupo sahihi?

Wewe hapo utawaona wale watakaokuonesha huzuni kwa kuwa kiukweli una njaa ya huruma ilimujisikie vyema lakini huko kujisikia vyema ni kwa muda tu na hali itarudia

Jifunze kukubaliana na mambo na kukubali yaende!
 
Mtoa mada pole sana lakini ushapata wa kukufariji huyu amejitokeza naimani utasuuzika nafsi

sasa hajapatikana. nilichokiona kwaumri sawa na wangu. namaanisha lika kuanzia miaka 30.hasa wazuri WALiSHAUMIZWA Hawaamini kabisa kama anaweza kupendwa. na kupeda hiyo ndo changamoto.
 
Inasikitisha sana mtu wa umri kama huu kuondokewa na mpendwa wake miezi mitano iliyopita halafu analialia kiasi hiki

Ndugu, mioyo ya binadamu inatofautana, uwezo wa kukabiliana na matatizo haufanani...
Tujaribu kumpa njia m'badala ya kukabiliana na majonzi alonayo.
 
Ndugu, mioyo ya binadamu inatofautana, uwezo wa kukabiliana na matatizo haufanani...
Tujaribu kumpa njia m'badala ya kukabiliana na majonzi alonayo.

Hakuna njia mbadala tofauti na kumweleza ukweli!
 
Pole zako Mkuu inaelekea ulikuwa unampenda sana Mkeo, lakini yaliyotokea ndio yameshatokea na kama ulivyosema maisha ni lazima yaendelee. Ni kawaida kuumia kiasi hicho inapotokea mahusiano na yule uliyempenda kuvunjika. Kila la heri katika kuendelea na maisha yako.
 
Limbert
god_will_make_you_stronger-453069.jpg
 
Last edited by a moderator:
Pole sana kwa kuondokewa na ubavu wako Jambo Moja binadamu tunashindwa kulikubali kwamba hakuna kitakachobaki hapa duniani yeye katangulia tu na wewe utafuata cha umuhimu ni kumshukuru Mungu na kukubali kwamba vyote vyake, jiombee wewe sasa kwani mwenzio safari yake imeisha kazi kwako jipange na iko siku utakuja hapa utasema nimempata mwingine na kuomba ushauri hapa jaribu. usifananishe yule ni yule tu.kubali matokeo na uombe upate mwingine si kama bora zaidi ya yeye hayo ndio maombi zingatia.kila la kheri
 
Pole sana aisee.Mie naelelewa nini unamaanisha.Nimempoteza mme wangu kipenzi Mwezi wa Nane mwaka huu.Kweli asikwambie mtu.adi leo sijazoea kabisa.Pole sana mwenzangu.
kaniachia mtoto mmoja na umri wangu ni 32.Nipo kwenye wakati mgumu sana aisee.adi nimepata ugonjwa wa moyo. khaaaa kweli kifo cha umpendae ni matatizo makubwa. Pole sana mwenzangu.

karibu tushauriane na kupeana mawazo ya hapa na pel hasa kwenye mambo ya mirathi na nk maana ndo yanayotukabili wengi.
 
Pole ndugu,kuondokea na kipenzi cha moyo wako ni maumivu makali sana. Lakini yakupasa kujipa moyo na maisha yaendlee kama ulivosema,kama walivoshauri wengine penda kujichanganya na wengine,uwe mtu wa ibada taratibu mzigo wa maumivu yatapungua. Na Mungu atakupa mke mwingine atakaesuuza mtima wako. Muhimu ni kua makini usijeangukia kwenye janga
 
Back
Top Bottom