katika jamii hii nimeingia tangu sasa nina maumimivu makali katka moyo wangu.kwa miezi mitano sasa toka nimpoteza mpendwa wa moyo wangu (Alifariki). sasa ninaumri 40 lakini nakili kuwa nilikuwa nikiungana na Wengi kusema nikazi ya MUNGU na baada ya muda nazoea maisha yanaendelea. Kituambacho imekuwa kinyume toka nimpoteze mpendwa wangu mpenzi wa moyo wangu nakili kuwa alikuwa mke mzuri wa tabia sura naumbo .kilicho kuwa kikivutia zaidi hakujiunga namkologo wowote; nilikuwa nikivutiwa na ngozi yake. ninapotoka kazini toka ameniacha . huingiwa nahuzuni kila mara hushindwa kutoka hata nyumbaini nashindwa kufanya kazi za ziada ijapo MAISHA LAZIMA YAENDELEE . Nitaepukanaje na hali hii.
Tatizo lako kubwa hujiaini na kwakuwa hujiamini huwaamini binadamu wengine pia
Marehemu mpendwa wako huenda ni kweli alikuwa na sifa hizo
Hilo halimaanishi kuwa hakuna mwingine
Lakini pia hilo halimaanishi ndio ukae na huzuni kiasi hicho
Huko aliko anasikitika sana kwa kuona namna ulivyo dhaifu
Na anasikitika kuwahi kuwa na mahusiano na mtu dhaifu kama wewe
Uanaume sio kuwa na jinsia ya kiume tu
Ni pamoja na kuyaweza majaribu kama haya
Tena una umri wa miaka 40!!!!!!!!!!!!!!
Unasikitisha sana
Unadhani kuwa ulibahatisha kumpata
Hujiamini kabisa
Huamini kama kuna wanawake wazuri kama huyo
Unadhani ni vigumu sana kuwapata wa aina hiyo
hujui kwamba kuna wanawake bora sana zaidi ya huyo
Unajidanganya kuwa hayo ni mapenzi ndio yanakufanya hivyo
Ukweli ni kuwa hiyo ni hofu tu ya kupata mwingine kama huyo
Unaendelea kujidanganya kuwa kuna kama huyo
Unashindwa kujua tu kuwa hakuna kama huyo lakini kuna aliebora kuliko huyo
Hebu kua kiakili!
By the way
Pole na kuondokewa na mpendwa wako
Jambo zuri la kufanya na kumuenzi ni kukua kiakili na kuondokana na hayo mawazo!