Kwa muda wa miaka miwili sasa nimekuwa nasumbuliwa na maumivu chini kidogo ya ubavu wa kushoto, nimejaribu kwenda hospitali mara kadhaa, mara ya kwanza nikaambiwa UTI pamoja na kutumia dawa maumivu hayakuisha! Nimesharudia kupima mara 3 sina UTI tena, ila maumivu yanazidi! Kitu pekee kinacho nisaidia kupunguza maumivu ni kunywa maji mengi! Hali hii mpaka lini? Naombeni ushauri wa kitabibu wakubwa zangu!