MillionaireMan
Senior Member
- Jul 20, 2022
- 157
- 234
Hivi majuzi yapata majuma yaliyopita, Rais Samia aliwaeleza wananchi kuhusu mikopo aliyoipata kutoka Bank ya dunia na IMF ya kwamba ni mikopo ya bei nafuu.
Haitoshi, tukapata tena mikopo au niseme pesa zilizoolewa bure kwaajili ya nchi zinazoendelea zilizoathiriwa na Covid-19. Mgawanyo wa fedha hizo zilienda kwenye kujenga madarasa, sijui na kitu gani.
Jana tu, Serikali ya Rais Samia imekopa tena zaidi ya $ 1.B . Kama mtanzania wa kawaida nashangazwa na utitiri wa mikopo inayoendelea. Moja ya mikopo tajwa hapo, ilienda kujenga barabara Pemba huko, yaani inaenda nusu kwa nusu Bara na Visiwani Znz.
Mimi siamini kwamba huu ndio mfumo mzuri wa kujenga uchumi wa nchi madhubuti. Kwa mfano, tungebana matumizi na kuachana na stail au mfumo ule tuliozoea mfano, viongozi wa idara, taasisi, mashirika kuwa na madereva, mikutano ya hovyo, kamati zisizo na tija. Kwa mfano, wizara ya Habari imetoa PR kuhusu kamati itakayofanya kazi kutafuta mdundo wenye asili ya Tanzania.
Mama Samia, sijui kama unajua uchumi unavyokwenda na mimi naona hatuna nia ya dhati kweli kujitoa kwenye huu umaskini mkubwa. Watz wnataka kazi, watz wanataka maisha bora. Mimi naoma unajidhatiti na uchaguzi ujao badala ya kushughulikia hata jambo moja tu sawa once and for all.
Cheo ni dhamana, wakati wenu utapita, nchi hii itabaki milele, je watoto wetu tunawaachia nini?
Ndio maana tunataka katiba mpya kutokana na serikali kujiamulia kfanya mambo bila idhini ya Bunge wala mahakama kujua.
Haitoshi, tukapata tena mikopo au niseme pesa zilizoolewa bure kwaajili ya nchi zinazoendelea zilizoathiriwa na Covid-19. Mgawanyo wa fedha hizo zilienda kwenye kujenga madarasa, sijui na kitu gani.
Jana tu, Serikali ya Rais Samia imekopa tena zaidi ya $ 1.B . Kama mtanzania wa kawaida nashangazwa na utitiri wa mikopo inayoendelea. Moja ya mikopo tajwa hapo, ilienda kujenga barabara Pemba huko, yaani inaenda nusu kwa nusu Bara na Visiwani Znz.
Mimi siamini kwamba huu ndio mfumo mzuri wa kujenga uchumi wa nchi madhubuti. Kwa mfano, tungebana matumizi na kuachana na stail au mfumo ule tuliozoea mfano, viongozi wa idara, taasisi, mashirika kuwa na madereva, mikutano ya hovyo, kamati zisizo na tija. Kwa mfano, wizara ya Habari imetoa PR kuhusu kamati itakayofanya kazi kutafuta mdundo wenye asili ya Tanzania.
Mama Samia, sijui kama unajua uchumi unavyokwenda na mimi naona hatuna nia ya dhati kweli kujitoa kwenye huu umaskini mkubwa. Watz wnataka kazi, watz wanataka maisha bora. Mimi naoma unajidhatiti na uchaguzi ujao badala ya kushughulikia hata jambo moja tu sawa once and for all.
Cheo ni dhamana, wakati wenu utapita, nchi hii itabaki milele, je watoto wetu tunawaachia nini?
Ndio maana tunataka katiba mpya kutokana na serikali kujiamulia kfanya mambo bila idhini ya Bunge wala mahakama kujua.