Matokeo ya Oparesheni ya Makonda dhidi ya dawa za kulevya yalivyoitikisa Afrika ya Kusini

Mgodo visa

JF-Expert Member
Nov 1, 2016
3,562
3,559
Hakuna asiejua ni ujasiri kiasi gani aliojivika ndugu yetu na kiongozi wetu mwenye nia ya dhati na uchungu kwa vijana (maana ndio wahanga wakubwa) wanao angamia katika janga la dawa za kulevya.

Harakati anazofanya ndugu Makonda akiungwa mkono na VIONGOZI wa kada mbalimbali, ni kweli ZIMEBAMBA sio nyumbani tu Tanzania bali ni Afrika yote na zaidi nchini AFRIKA YA KUSINI....

Pitia miji yote mikubwa katika nchi mbalimbali..Harare...Lusaka....Maputo.....Johanesburg....Kigali...Kampala...Mombasa n.k.
Habari kubwa ni Makonda/Magufuri na Tanzania yetu... KEEPON MOVIN Brother Makonda wengi tuko nyuma yako....

Baada ya kile kinancho endelea nchini Tanzania...
Raia/wanaharakati na wazazi katika jiji la Pritolia wameomba kibali cha maandamano siku ya IJUMAA wakishinikiza serikali kupitia idara yake ya MAMBO YA NDANI....juu ya wahamiaji na wageni (watalii) zaidi kutoka nchini Tanzania..

Wakilaani kuishi na kuingia kwao nchini kuwa ni CHANZO NA SABABU moja wapo ya kukithiri kwa MADAWA na UHALIFU dhidi ya WATOTO wao (wazawa) hivyo kuomba serikali kupitia upya sera zake kuhusu uhamiaji na ni namna gani ya kuwadhibiti Watanzania waishio na wanaotembelea nchini (SA)

Ninatoa ombi kwa SERIKALI ya Tanzania kuangazia macho swala hili kuona ni namna gani itaweza kuwalinda RAIA WAKE WEMA dhidi ya tukio hilo la tarehe 24.

Nb: hii ni kama maandamano hayo yatapewa baraka na serikali.
 
Maandamano yatakayofanyika siyo kwa ajili ya madawa ya kulevya au wahamiaji haramu kutoka Tanzania pekee.
 
Tusije anza kutakiwa tuwe na visa kwenda kwa madiba.
Kumbe S.A ukitaka kuandamana unaomba kibari, mimi ninavyojua maandamano nchi za demokrasia hayahitaji kibari
 
Back
Top Bottom