Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,198
- 7,536
Kwa maoni yako kama CCM itatokea ikashinda kesho chalinze utajifuza nini na ikitokea CHADEMA wakishinda utakuwa umejifunza nini!? vile vile ikitokea CUF wakishinda utajifunza nini?
Kwa upande wangu CHADEMA wakishinda nitatafsiri kwamba CHADEMA itaingia kwenye uchaguzi mkuu 2015 ikiwa na morali kiasi na hivyo inaweza kufanya vizuri kiasi na wakishindwa ,CHADEMA itaingia 2015 ikiwa imekata tamaa na haiwezi kufika popote.
kama CUF watashinda itakuwa ni dalili kwamba CUF ikifufuliwa inaweza kufufuka.
CCM ikishinda, hii itakuwa inaashiria kwamba CCM itaingia uchaguzi 2015 ikiwa ni kama hakuna upinzani isipokuwa tu kama kutaibuka chama kipya na kikawa na muelekeo wa kueleweka.
Hii ni kwa sababu haitarajiwi kutokea uchaguzi mwingine mdogo tena kabla ya 2015.
Ni maoni tu lakini, naweza kukosolewa!
Kwa upande wangu CHADEMA wakishinda nitatafsiri kwamba CHADEMA itaingia kwenye uchaguzi mkuu 2015 ikiwa na morali kiasi na hivyo inaweza kufanya vizuri kiasi na wakishindwa ,CHADEMA itaingia 2015 ikiwa imekata tamaa na haiwezi kufika popote.
kama CUF watashinda itakuwa ni dalili kwamba CUF ikifufuliwa inaweza kufufuka.
CCM ikishinda, hii itakuwa inaashiria kwamba CCM itaingia uchaguzi 2015 ikiwa ni kama hakuna upinzani isipokuwa tu kama kutaibuka chama kipya na kikawa na muelekeo wa kueleweka.
Hii ni kwa sababu haitarajiwi kutokea uchaguzi mwingine mdogo tena kabla ya 2015.
Ni maoni tu lakini, naweza kukosolewa!