..nilikuwa kule mzalendo.net nikakutana na malalamiko ya waZNZ kuhusu matokeo ya form 4.
ABDISALUM @ mzalendo.net said:Yakhe nimepigwa na bumbuwazi. Sijui niseme nini kuhusu kufelishwa (KUFELISHWA0 vijana wetu, watoto wetu, na akhli zetu eti kwa kisingizo kuwa wamekopia mitihani. Basi kukopia huko ijulikane mwisho wa kufanya mitihani, na sio wakati wa marking (kusahihisha) au wakati wa kufanya mitihani yenyewe? Hii ni dhulma, na NECTA ime-watarget waislamu, na kadhalika Wazanzibari (ambao pia ni jumla ya waislamu).
Angalia mambo yalivyo: chuo cha kiislamu Pemba (kilichopo Kiuyu) chote kimefutiwa matokeo hawa ni wanafunzi wa mchepuo yaani ni best brain wanaingia kuanzia Form 1-4, tena ni science (takriban miaka mingi sasa wanachukua darja la juu TZ katika kufaulu).
Rungu dhidi ya Uislamu hilo.
ABDISALUM @ mzalendo.net said:Angalia kinyume chake: alikamatwa mtoto mmoja skuli ya Mwanakwerekwe Zanzibar na bomu yaani karatasi isiyoruhusiwa kuingia ndani ya chumba cha mtihani. Alipobanwa sana aseme ameipata wapi. Alisema kuwa amepewa na mwalimu mmoja anayeishi Uzini. Intelligence ilipofuata tip hiyo, walimkamata mwalimu huyo (jina xxx) na alikiri kuwa yeye ndiye amesambaza mitihani iliyovuja. Huyu Mwalimu XXX ni Mkiristo, aliposema tu jina lake kuwa yeye ni John au Charles hakukuwa tena na maneno ya zaida aliachiwa HURU. Ni miongoni mwao, na hana doa mfalme huyu.
Hii inajulikana na hata Wizara inajua hili.
Pia matokeo ya chuo cha kiislam Zanzibar (mazizini) kimefutiwa matokeo (hujuma hiyo). Ukijumlisha na wale wa wanafunzi wa skuli ya Ndanda (Mtwara waliotaka kusali) na wamenyimwa haki yao ya msingi, wamfukuzwa na hatimaye kunyimwa kufanya mtihani wa Form 6/F4.
Kosa la nani? msimamiaji mtungaji mtihani .msahihishaji au nani hasa mkosa mpaka wamehukumiwa watoto wetu kwa adhabu kali ya namna hiyo.
In short, NECTA inavujisha mitihani kwa makusudi na wanajua hilo, lakini target ni kuhukumu watu fulani fulani, na hasa waislamu. jamani Wazanzibari tuamke, na kama hatujaamka kwa haya yote, basi hatuamki tena, na bora tufe tuzikwe!
Mitihani siku hizi inasimamiwa na polisi, vipi inavuja? na Inavuja Zanzibar tu.
Nini msimamo wa SMZ kwa suala hili, na nini msimao wa kitufe chetu GNU kutetea maslahi ya vijana wetu? Hiiv kweli mpaka leo Wizara ya Elimu chini ya bunju mzoezi Ramdhan Abdullah Shaban na Bi.Zahra Hamad (CUF) wameshindw akutoa statement angalau ya kuwaliwaza wazee/wazazi.
Noamba SMZ- na kitufe chetu GNU (au toy ya GNU) wajue kuwa wazazi tumetumia millions of shs mpaka kuwasomesha watoto wetu hapa walipofika. leo inapita dhulma ya namna hii. Tufanye nini?
Kwa mtu yeyote mwenye akili timamu, hawezi kuamini narration ya NECTA kuwa eti tumekopia.
Sasa bado BLW wana nafasi nzuri na nzuri kuamua mastakabali wetu iwe mitihani au mafuta au katiba mpya. Waseme NO pale BLW, na warejeshe kadi CCM Dodoma, tuone tutayapata madhila kama haya tena? Je, ni lazima ufanye mtihani uliotungwa na Watanganyika ndio uwe msomi?
Bado BLW lina nafasi nzuri ya kupitisha bill tofauti ili kujinasua. BLW nayo inaokena kama vile ki-toy cha kuchezea watoto. Why? siku hizi (tokea imeanza GNU) huwa ninagombana sana na marafiki zangu hapa mjini wao wanaamini kuwa BLW sasa ni moja eti hakuna CUF wala CCM kuna uzanzibari. Ugomvi utakuja kuwa mimi sijauona huo Uzanzibari; na ninauona unafik zaidi. Jamani eeee .zanzibar inazama, inazamishwa .na wallah tunaikosa hivi hivi, si lazima upigwe rungu la kichwa na ufe ndio ujue mwisho wako, unaweza kuuliwa kidogo kidogo kama hii ya mitihani. Kwa ufupi athari ya kufutiwa matokeo na kufelishwa watoto wetu ni kuwa jamii itaharibika sana, tutapata wala unga wengi, walevi, na watoto wetu wa kike hatari ya .na ndoa umri mdogo. Hatari. hii itaimaliza jamii ya kizanzibari itakuwa haina elimu wala maarifa mazuri.
JAMANI EEE TUAMKE, BADO TUMELALA TU.
TUMEGANDA NI KITANDA KELELE ZOTE HAMZISIKII. AMKA WEE BABU WA MATANGATUANI, NA FINYA AU TAZARI, NA KINYASINI!!