Matokeo Form 4: Je, NECTA imewahujumu Wazanzibari?

Status
Not open for further replies.

JokaKuu

Platinum Member
Jul 31, 2006
30,441
54,984
..nilikuwa kule mzalendo.net nikakutana na malalamiko ya waZNZ kuhusu matokeo ya form 4.


ABDISALUM @ mzalendo.net said:
Yakhe nimepigwa na bumbuwazi. Sijui niseme nini kuhusu kufelishwa (KUFELISHWA0 vijana wetu, watoto wetu, na akhli zetu eti kwa kisingizo kuwa ‘wamekopia’ mitihani. Basi kukopia huko ijulikane mwisho wa kufanya mitihani, na sio wakati wa marking (kusahihisha) au wakati wa kufanya mitihani yenyewe? Hii ni dhulma, na NECTA ime-watarget waislamu, na kadhalika Wazanzibari (ambao pia ni jumla ya waislamu).
Angalia mambo yalivyo: chuo cha kiislamu Pemba (kilichopo Kiuyu) chote kimefutiwa matokeo — hawa ni wanafunzi wa mchepuo — yaani ni best brain wanaingia kuanzia Form 1-4, tena ni science (takriban miaka mingi sasa wanachukua darja la juu TZ katika kufaulu).
Rungu dhidi ya Uislamu hilo.
ABDISALUM @ mzalendo.net said:
Angalia kinyume chake: alikamatwa mtoto mmoja skuli ya Mwanakwerekwe Zanzibar na ‘bomu’ yaani karatasi isiyoruhusiwa kuingia ndani ya chumba cha mtihani. Alipobanwa sana aseme ameipata wapi. Alisema kuwa amepewa na mwalimu mmoja anayeishi Uzini. Intelligence ilipofuata tip hiyo, walimkamata mwalimu huyo (jina xxx) na alikiri kuwa yeye ndiye amesambaza mitihani iliyovuja. Huyu Mwalimu XXX ni Mkiristo, aliposema tu jina lake kuwa yeye ni “John au Charles” hakukuwa tena na maneno ya zaida aliachiwa HURU. Ni miongoni mwao, na hana doa – mfalme huyu.
Hii inajulikana na hata Wizara inajua hili.
Pia matokeo ya chuo cha kiislam Zanzibar (mazizini) kimefutiwa matokeo (hujuma hiyo). Ukijumlisha na wale wa wanafunzi wa skuli ya Ndanda (Mtwara waliotaka kusali) na wamenyimwa haki yao ya msingi, wamfukuzwa na hatimaye kunyimwa kufanya mtihani wa Form 6/F4.
Kosa la nani? msimamiaji…mtungaji mtihani….msahihishaji au nani hasa mkosa mpaka wamehukumiwa watoto wetu kwa adhabu kali ya namna hiyo.
In short, NECTA inavujisha mitihani kwa makusudi na wanajua hilo, lakini target ni kuhukumu watu fulani fulani, na hasa waislamu. jamani Wazanzibari tuamke, na kama hatujaamka kwa haya yote, basi hatuamki tena, na bora tufe tuzikwe!
Mitihani siku hizi inasimamiwa na polisi, vipi inavuja? na Inavuja Zanzibar tu.
Nini msimamo wa SMZ kwa suala hili, na nini msimao wa kitufe chetu GNU kutetea maslahi ya vijana wetu? Hiiv kweli mpaka leo Wizara ya Elimu chini ya bunju mzoezi Ramdhan Abdullah Shaban na Bi.Zahra Hamad (CUF) wameshindw akutoa statement angalau ya kuwaliwaza wazee/wazazi.
Noamba SMZ- na kitufe chetu GNU (au toy ya GNU) wajue kuwa wazazi tumetumia millions of shs mpaka kuwasomesha watoto wetu hapa walipofika. leo inapita dhulma ya namna hii. Tufanye nini?
Kwa mtu yeyote mwenye akili timamu, hawezi kuamini narration ya NECTA kuwa eti tumekopia.

Sasa bado BLW wana nafasi nzuri na nzuri kuamua mastakabali wetu – iwe mitihani au mafuta au katiba mpya. Waseme NO pale BLW, na warejeshe kadi CCM Dodoma, tuone tutayapata madhila kama haya tena? Je, ni lazima ufanye mtihani uliotungwa na Watanganyika ndio uwe msomi?
Bado BLW lina nafasi nzuri ya kupitisha bill tofauti ili kujinasua. BLW nayo inaokena kama vile ki-toy cha kuchezea watoto. Why? siku hizi (tokea imeanza GNU) huwa ninagombana sana na marafiki zangu hapa mjini – wao wanaamini kuwa BLW sasa ni moja eti hakuna CUF wala CCM – kuna uzanzibari. Ugomvi utakuja kuwa mimi sijauona huo Uzanzibari; na ninauona unafik zaidi. Jamani eeee….zanzibar inazama, inazamishwa….na wallah tunaikosa hivi hivi, si lazima upigwe rungu la kichwa na ufe ndio ujue mwisho wako, unaweza kuuliwa kidogo kidogo kama hii ya mitihani. Kwa ufupi athari ya kufutiwa matokeo na kufelishwa watoto wetu ni kuwa jamii itaharibika sana, tutapata wala unga wengi, walevi, na watoto wetu wa kike — hatari ya ….na ndoa umri mdogo. Hatari. hii itaimaliza jamii ya kizanzibari ……itakuwa haina elimu wala maarifa mazuri.
JAMANI EEE… TUAMKE, BADO TUMELALA TU.
TUMEGANDA NI KITANDA KELELE ZOTE HAMZISIKII. AMKA WEE BABU WA MATANGATUANI, NA FINYA AU TAZARI, NA KINYASINI!!

 
..hii ni taarifa ya gazeti la Nipashe kuhusu matokeo ya mitihani ya form 4.

MATOKEO KIDATO CHA NNE MAAFA!!

-- shule za serikali zaburuzwa.

-- waliofeli ni asilimia 47.

Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) limetangaza matokeo ya Mitihani ya Kidato cha Nne (CSEE) iliyofanyika nchini Oktoba, mwaka jana, huku kiwango cha kufaulu kikionyesha kuwa kiasi cha asilimia 46.63 na cha kufeli kwa kupata daraja sifuri ni asilimia 53.37
Matokeo hayo yaliyotangazwa jana na Katibu Mtendaji wa Necta, Dk. Joyce Ndalichako, yanaonyesha kuwa, licha ya kiwango cha kufaulu kuongezeka kwa asilimia 3.13, bado wanafunzi wengi wameendelea kufanya bibaya katika mtihani huo.
Kwa mujibu wa matokeo hayo, kati ya watahiniwa 426,314 sawa na asilimia 94.67 waliofaulu kati ya daraja la kwanza hadi la nne ni 180,216.
Hata hivyo, waliofaulu kwa daraja la nne ndio wengi wakiwa ni 146,639 sawa na asilimia 81.3 ya waliofaulu huku wale wa daraja la kwanza, pili na tatu wakiwa ni 33,577 sawa na asilimia 9.8.
Wakati hali kwa watahiniwa ikiwa hivyo, shule za sekondari za kata, zimeendelea kufanya vibaya kulinganisha na zile za watu binafsi.
Pia watahiniwa 3,303 wamefutiwa matokeo kutokana na baadhi kufanya udanganyifu na wengine kuandika matusi katika karatasi zao za majibu ya mitihani.
Hata hivyo, matokeo hayo yanaonyesha wavulana wakiongoza kufaulu mitihani hiyo kwa asilimia 53.53, huku wasichana wakifaulu kwa asilimia 44.36.

WATAHINIWA WA SHULE WALIOFAULU MTIHANI

"Mwaka 2010 watahiniwa waliofaulu walikuwa 177,021 sawa na asilimia 50.40 ya watahiniwa waliofanya mtihani huo. Hivyo, kiwango cha kufaulu kimeongezeka kwa asilimia 3.13," alisema Dk. Ndalichako. Ongezoko hilo ni sawa na watahiniwa 12,789.

WATAHINIWA WOTE
Alisema jumla ya watahiniwa 225,126 (asilimia 53.37) wamefaulu mtihani huo, wakiwamo wasichana 90,885 sawa na asilimia 48.25 ya wasichana waliofanya mtihani na wavulana 134,241 sawa na asilimia 57.51 ya wavulana waliofanya mtihani.
"Mwaka 2010 watahiniwa waliofaulu walikuwa 223,085 sawa na asilimia 50.74. hivyo, kufaulu kumeongezeka kwa asilimia 3.13," alisema Dk. Ndalichako.

WALIOSAJILIWA KUFANYA MTIHANI
Alisema jumla ya watahiniwa 450,324 walisajiliwa kufanya mitihani hiyo, kati yao wakiwamo wasichana 201,799 (aslimia 44.81) na wavulana 248,525 (asilimia 55.19), idadi ambayo imepungua kwa watahiniwa 7,790 (asilimia 1.70) kati ya watahiniwa 458,114 waliosajiliwa mwaka juzi.

WALIOFANYA NA AMBAO HAWAKUFANYA MTIHANI
Dk. Ndalichako alisema watahiniwa waliofanya mtihani huo ni 426,314 (asilimia 94.67) na kwamba, watahiniwa 24,010 hawakufanya mtihani, ambao ni sawa na asilimia 5.33 ya watahiniwa wote waliosajiliwa.


WATAHINIWA WA SHULE WALIOSAJILIWA
Alisema watahiniwa wa shule waliosajiliwa ni 349,390 wakiwamo wasichana 150,371 (asilimia 43.04) na wavulana 199,019 (asilimia (56.96), idadi ambayo inaonyesha kupungua kwa watahiniwa 14,209 (asilimia 3.91) kati ya watahiniwa 363,589 wa shule waliosajiliwa mwaka juzi.

VITUO VYA MITIHANI
Dk. Ndalichako alisema jumla ya vituo 4,795 vilitumika katika kufanya mitihani hiyo ikilinganishwa na vituo 4,653 vilivyotumika mwaka juzi.

WALIOFAULU MTIHANI WA MAARIFA
Alisema katika Mtihani wa Maarifa (QT) wa mwaka jana, jumla ya watahiniwa 9,069 (asilimia 40.70) ya waliofanya mtihani wamefaulu ikilinganishwa na asilimia 35.17 ya waliofaulu mtihani mwaka juzi.
"Hivyo, kiwango cha kufaulu kwa Mtihani wa Maarufu kimeongezeka kwa asilimia 5.53 ikilinganishwa na mwaka 2010," alisema Dk. Ndalichako.
Alisema katika mtihani huo, watahiniwa waliosajiliwa ni 29,447 ambapo wasichana walikuwa ni 18,019 na wavulana ni 11,428 na kwamba, jumla ya watahiniwa 22,400 (asilimia 76.07) ya waliosajiliwa wamefanya mtihani, wasichana wakiwa ni 13,898 na wavulana ni 8,502.

WATAHINIWA WA KUJITEGEMEA
Dk. Ndalichako alisema watahiniwa wa kujitegemea waliofaulu mtihani ni 44,910 (asilimia 52.52) ya waliofanya mtihani; wasichana wakiwa ni 20,972 (asilimia 47.90) na wavulana ni 23.938 (asilimia 57.38).
Alisema mwaka juzi watahiniwa wa kujitegemea walikuwa 46,064 (asilimia 52.09) walifaulu mtihani huo.

UBORA WA KUFAULU KWA JINSIA
Dk. Ndalichako alisema jumla ya watahiniwa wa shule 33,577 (asilimia 9.98) wamefaulu katika madaraja I-III; wasichana wakiwa 10,313 (asilimia 7.13 na wavulana 23,264 (asilimia 12.13).

SHULE BORA
Alizitaja shule 10 bora zilizoko katika kundi la shule zenye watahiniwa 40 na zaidi kuwa ni St. Francis Girls iliyoko mkoani Mbeya; Feza Boys (Dar es Salaam); St. Joseph Millenium (Dar es Salaam); Marian Girls (Pwani); Don Bosco Seminary (Iringa); Kasita Seminary (Morogoro); St. Mary's Mazinde Juu (Tanga); Canossa (Dar es Salaam); Mzumbe (Morogoro) na Kibaha (Pwani).
Pia alizitaja shule 10 bora zilizoko katika kundi la shule zenye watahiniwa chini ya 40 kuwa ni Thomas More Machrina (Dar es Salaam); Feza Girls (Dar es Salaam); Dung'unyi Seminary (Singida); Maua Seminary (Kilimanjaro); Rubya Seminary (Kagera); St. Joseph Kilocha Seminary (Iringa); Sengerema Seminary (Mwanza); Lumumba (Unguja); Queen of Apostels-Ushirombo (Shinyanga) na Bihawana Junior Seminary (Dodoma).

SHULE ZA MWISHO
Vilevile, alizitaja shule 10 za mwisho zenye watahiniwa 40 na zaidi kuwa ni Bwembwera (Tanga); Pande Darajani (Tanga); Mfundia (Tanga); Zirai (Tanga); Kasokola (Rukwa); Tongoni (Tanga); Mofu (Morogoro); Mziha (Morogoro); Maneromango (Pwani) na Kibuta (Pwani).
Kadhalika, alizitaja shule 10 za mwisho zenye watahiniwa chini ya 40 kuwa ni Ndongosi (Ruvuma); St. Luke (Ruvuma); Igigwa (Tabora); Kining'inila (Tabora); Ndaoya (Tanga); Kilangali (Morogoro); Kikulyungu (Lindi); Usunga (Tabora); Mto Bubu Day (Dodoma) na Miguruwe (Lindi).

WANAFUNZI WALIOFANYA VIZURI ZAIDI
Aliwataja watahiniwa 10 bora kitaifa kuwa na shule wanazotoka kwenye mabano kuwa ni Moses Andrew Swai (Feza Boy's-Dar es Salaam); Rosalyn Tandau (Marian Girls-Pwani); Mboni Maumba (St. Francis Girls-Mbeya); Sepiso Mwamelo (St. Francis Girls-Mbeya); Uwella Rubuga (Marian Girls-Pwani); Hellen Mpanduji (St. Mary's Mazinde Juu-Tanga); Daniel Wallace Maugo (St. Joseph Millenium-Dar es Salaam); Benjamin Tilubuzya (Thomas More Machrina-Dar es Salaam); Simon William Mbangalukela (St. Joseph Millenium-Dar es Salaam) na Nimrod Deocles Rutatora (Feza Boy's-Dar es Salaam).

WASICHANA 10 BORA KITAIFA
Pia aliwataja wasichana 10 bora kitaifa kuwa ni Rosalyn Tandau (Marian Girls-Pwani); Mboni Maumba (St. Francis Girls-Mbeya); Sepiso Mwamelo (St. Francis Girls-Mbeya); Uwella Rubuga (Marian Girls-Pwani); Hellen Mpanduji (St. Mary's Mazinde Juu-Tanga); Lissa Chile (St. Francis Girls-Mbeya); Elizabeth Ng'imba (St. Francis Girls-Mbeya); Doris Atieno Noah (Kandoto Sayansi Girls-Kilimanjaro); Herieth Machunda (St. Francis Girls-Mbeya) na Daisy Mugenyi (Kifungilo Girls-Tanga).

WAVULANA 10 BORA KITAIFA
Vilevile, aliwataja wavulana 10 bora kitaifa kuwa ni Moses Andrew Swai (Feza Boy's-Dar es Salaam); Daniel Wallace Maugo (St. Joseph Millenium-Dar es Salaam); Benjamin Tilubuzya (Thomas More Machrina-Dar es Salaam); Simon William Mbangalukela (St. Joseph Millenium-Dar es Salaam); Nimrod Deocles Rutatora (Feza Boy's-Dar es Salaam); Simon Gabriel Mnyele (Feza Boys-Dar es Salaam); Paschal John Madukwa (Nyegezi Seminary-Mwanza); Henry Justo Stanley (St. Joseph Millenium-Dar es Salaam); Frasisco Paschal Kibasa (Mzumbe-Morogoro) na Tumaini Charles (Ilboru-Arusha).

MATOKEO YA MTIHANI YALIYOSITISHWA
Katibu Mtendaji huyo alisema Baraza limesitisha kutoa matokeo ya watahiniwa 264 wa kujitegemea waliofanya mtihani wa kidato cha nne, 116 waliofanya mtihani wa maarifa na 873 wa shule za binafsi mwaka jana bila kulipa ada ya mtihani hadi watakapolipa ada pamoja na faini.
Alisema ikiwa watahiniwa hao hawatalipa baada ya miaka miwili tangu matokeo yatakapotangazwa, matokeo yatafutwa.
Dk. Ndalichako alisema wengine ni watahiniwa 67 ambao hawajawasilishiwa alama za tathmini ya masomo (Continuous Assessment) katika masomo yote waliyofanya hadi hapo Mkuu wa Shule husika atakapowasilisha pamoja na sababu za kutowasilisha mapema.

WALIOFANYA UDANGANYIFU KATIKA MITIHANI
Alisema Baraza pia limefuta matokeo ya watahiniwa 3,303 waliobainika kufanya udanganyifu katika mitihani ya Oktoba mwaka jana; ambao kati yao alisema watahiniwa 3,301 ni wa mtihani wa kidato cha nne na wawili ni wa maarifa.
Alizitaja aina za udanganyifu zilizobainika kufanywa na watahiniwa hao kuwa ni pamoja na watahiniwa kukamatwa na wasimamizi ndani ya chumba cha mtihani wakiwa na notes, simu kufanyiwa mitihani na watu wengine na kubainika wamesajiliwa kufanya mtihani kwa kutumia majina ya wengine wakati walishafanya mtihani.
Aina nyingine za udanganyifu ni watahiniwa kubainika kuwa na mfanano wa majibu usio wa kawaida, kuwa na karatasi zao kuwa na miandiko tofauti au kuwa na miandiko tofauti katika katarasi ya somo moja, kubadilishana karatasi za maswali/vijitabu vya kujibia mtihani ili kuandikiana majibu, au kujadiliana ndani ya chumba cha mtihani.
Pia watahiniwa kukamatwa na vijitabu vya kuandika mitihani zaidi ya moja ambayo moja hakupewa na msimamizi, kubainika kuwa na kesi mbili tofauti; kama vile, mfanano wa majibu, notes, kijitabu cha kujibia zaidi ya kimoja na kubadilishana karatasi ya majibu au kijitabu cha kujibia mtihani.

WATAHINIWA WALIOANDIKA MATUSI
Dk. Ndalichako alisema matokeo mengine yaliyofutwa na Baraza ni ya watahiniwa wanane walioandika matusi katika karatasi za majibu yao.
Alisema kitendo hicho ni kosa kwa mujibu wa kifungu 5 (13) cha kanuni za mtihani.
Dk. Ndalichako alisema kitendo cha kuandika matusi kwenye karatasi za majibu, kinaonyesha utovu wa nidhamu wa hali ya juu na kwamba Baraza halitavumilia hata kidogo watahiniwa wa aina hiyo.
"Hivyo, pamoja na kuwafutia matokeo ufuatiliaji zaidi utafanyika ili kuona hatua zaidi wanazoweza kuchukuliwa," alisema Dk. Ndalichako.
Aliwataka watahiniwa walioanza mitihani ya kidato cha sita jana kujiepusha na udanganyifu katika mitihani na pia kuepuka mtindo wa kuandika matusi katika skripti zao au mambo yasiyohusiana na mtihani.

HATMA YA WATAHINIWA WALIOFUTIWA MATOKEO
Alisema Baraza limekuwa likifuta matokeo ya watahiniwa wanaofanya udanganyifu, lakini idadi ya wanaojihusisha na vitendo hivyo imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka.
"Hivyo, katika kikao chake cha 86 kilichofanyika tarehe 7/2/2012, Baraza liliamua kuwa watahiniwa wote waliofutiwa matokeo yao kutokana na kujihusisha na udanganyifu au kuandika matusi kwenye karatasi zao za majibu hawataruhusiwa kufanya mtihani wa Baraza kwa kipindi kisichopungua miaka mitatu," alisema Dk. Ndalichako.

VITUO NA WALIOHUSIKA NA UDANGANYIFU
Alitoa onyo kali kwa wamiliki wote wa vituo na shule ambazo zimejihusisha na udanganyifu.
"Tunapenda kuwajulisha wamiliki wote wa vituo vya watahiniwa wa kujitegemea kuwa ni wajibu ao kuhakikisha kuwa kanuni zote za uendeshaji mitihani zinazingatiwa ipasavyo," alisema Dk. Ndalichako.



SOURCE: NIPASHE
 
Hahaha Abdisalum amenichekesha mno,badala ya kuangalia chanzo cha tatizo anasingizia udini!pole yao
 
BMT wamedanganya! Ukweli ni kwamba waliofeli ni asiliwia 90. Hakuna shule ya juu,high school, inayopokea Div. IV. Hii 90% ya mwaka huu na mwaka jana na mwaka juzi na kurudi nyuma ni JANGA la Taifa. Muda tu ndio utafafanua zaidi.
 
Acheni ujinga,badala ya kuwaincourage watoto wenu wasome mnawapumbaza na hadithi zisizo na kichwa wala miguu!kuna wengine badala ya kuwaincourage wanafunzi wasome wakawa wanawaambia wasubiri watakuja kuzuia mitihani isifanyike!kweli!!kwa mtindo huu nadhani hata div4 watakuwa wanawapendelea.nonsence!!
 
Zanzibar in vilaza hao hawana jipya na wakijitenga hali itakuwa mbaya zaidi.
Sheria za mitihani zipo wazi kama huridhiki na matokeo unakata rufaa usahihishiwe tena. Hawa mzalendo wanapaswa kushitakiwa ili waathibitishe madai yao. Yaani kila kitu wao wanaonewa what a shame kwa zanzibari. Badala ya kuwaruhusu watoto wenu wasome muda mwingi mnawapeleka kwenye vigenge vya udini matokeo yakitoka mnasingizia mnahujumiwa, tena mkome kabisa.
 
Zanzibar in vilaza hao hawana jipya na wakijitenga hali itakuwa mbaya zaidi.
Sheria za mitihani zipo wazi kama huridhiki na matokeo unakata rufaa usahihishiwe tena. Hawa mzalendo wanapaswa kushitakiwa ili waathibitishe madai yao. Yaani kila kitu wao wanaonewa what a shame kwa zanzibari. Badala ya kuwaruhusu watoto wenu wasome muda mwingi mnawapeleka kwenye vigenge vya udini matokeo yakitoka mnasingizia mnahujumiwa, tena mkome kabisa.

ningekuwa karibu na pc ningekupa like mtu wangu!!
 
This dunia bana, is very interesting!! Wakati mwenzenu na-take opportunity ya kuifahamu hiyo mzalendo.net ili nikatangaze mishemishe zangu kule, wengine mtaishia kukashifiana hapa...!!! Thank u Joka Kuu kwa kunifahamisha uwepo wa hii kitu, wiki mbili zilizopita nimeshinda mashada.com (kenya) na sasa ngoja nikacheki upepo kule mzalendo.net! Kama kuna mwenye info kuhusu community network(like JF) in Uganda or any african country/or elsewhere ; please, let me know! Najua wapo watakaosema nenda ka-google!
 
Mimi kanimaliza kabisa huyu hapa

abdulmajid 09/02/2012 kwa 5:06 um · Ingia kujibu
yaani mm imeniumiza sana mtoto wa ami yangu nilijsha kujipanga nimpeleke DMI akasome ubaharia hawa wayahudi wa tanganyika wenye rangi nyeusi ndio wamemfutia matokeoo smz wekeni baraza la mitihani la zanzibar wacheni hizooo kila kitu kinawezekakana kwa nini mulipitisha sheria ya marekebisho ya katiba ya mwaka 2010 sasa ishindwe hili vunja muungano wa kuungana na mayahudi weusi wa tanganyika inauma ndugu zetu wanyonge wataanza na sigara na kumalizia bangi na unga na wanawake wawe papa badala ya changu halafu muwapeleke warabuni bila ya kuwa na colificationa ili wawe mahanisi na watumwa wa juwani MAPINDUZI DAIMA
 
kwa kweli hali ya kielimu ni mbaya sana kwa wafuga ndevu angalia shule 10 bora, watoto 10 bora ( kike na kiume) vyote havina halufu ya mfuga ndevu. Hapa inabidi tu wanyowe hizo ndevu.
 
Zanzibar in vilaza hao hawana jipya na wakijitenga hali itakuwa mbaya zaidi.
Sheria za mitihani zipo wazi kama huridhiki na matokeo unakata rufaa usahihishiwe tena. Hawa mzalendo wanapaswa kushitakiwa ili waathibitishe madai yao. Yaani kila kitu wao wanaonewa what a shame kwa zanzibari. Badala ya kuwaruhusu watoto wenu wasome muda mwingi mnawapeleka kwenye vigenge vya udini matokeo yakitoka mnasingizia mnahujumiwa, tena mkome kabisa.
Na ndo tatizo la Nchi feki,wao wenyewe hawana majibu kwa matatizo yao,kutwa kuchwa matatizo ni ya Tanganyika.
Kwani hiyo mitihani wanaihitaji Kama Nchi? Si wawapeleke watoto tu bila hiyo mitihani ya Tanganyika!
 
Miaka yote viongozi wa Zanzibar, watoto wao wanasoma bara tena kwenye shule za wagalatiya, Kifungilo na nyinginezo, wale akina kajamba nani wanaachwa wasome wamevaaa baibui na kanzu
 
Naona shule zilizoshika mkia Tanga inaongoza, vp maafisa elimu Tanga shughuli imewashinda?
 
Elimu dunia inapewa first preority zenji. Huwezi panda mahindi ukavuna karanga
 
Much as shule za kiislam na kutoka zanzibar zina matatizo ya ndani lakini naamini shule hizo zinafanyiwa ujinga fulani baraza la mitihana pamoja na wizara..

Kuna uwezekanao mkubwa kuwa pia baraza wanauza mitihani kwa shule za kikristo kwa siri ili ziendelee kuongoza; kwani watoto hao st. wakifika chuo ni mabogus ile mbaya..

naamini shule za kikanisa zinapewa mitihani; ili ziendelee kuongoza..
 
yaani sisi ni wayahudi weusi? huyu jamaa angesema hilo neno mbele yangu hakika hakuna rangi ambayo asingeiona!
 
Much as shule za kiislam na kutoka zanzibar zina matatizo ya ndani lakini naamini shule hizo zinafanyiwa ujinga fulani baraza la mitihana pamoja na wizara..

Kuna uwezekanao mkubwa kuwa pia baraza wanauza mitihani kwa shule za kikristo kwa siri ili ziendelee kuongoza; kwani watoto hao st. wakifika chuo ni mabogus ile mbaya..

naamini shule za kikanisa zinapewa mitihani; ili ziendelee kuongoza..
Umefanya utafiti au unaandika propaganda za misikitini? Mbona mimi nawafahamu wengi sana waliopitia seminary na wame perform vizuri vyuoni.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom