Katika siku za karibuni kumekuwa na matatizo sana ktk ndoa.na kwa utafiti wangu mdogo naona wanaume ndio waathirika wakubwa kila wanaume watano watatu au wanne wanatatizo hilo wengine wanaficha lakini wanaumia.na tatizo nililo liona ni pesa na ndugu.kwani utasikia mke wangu hela sijui anapeleka wapi anafanyakazi bt hela zake hazionekani au utasikia kila siku ndugu wamejaa nyumbani.Je wewe unaona nini tatizo na kipi cha kufanya?
As they say "Kosea Kujenga Nyumba,Usikosee kuoa"
mbona sijaona tatizo hapa? kama ni swala la pesa hili sio tatizo la walio kwenye ndoa pekee ni watu wote wana hili tatizo, tofauti ni kwamba walio kwenye ndoa wanalizungumzia na labda inafikia hatua ya kuona kama ni tatizo sababu wengine wanatumia approach mbaya kulizungumzia, lakini watu walio kwenye ndoa wanamanage tatizo la pesa vizuri kuliko walio nje ya ndoa.
cku hiz hakuna mpenz ya dhat ktk ndoa,weng wanasaka kampany na wengne rizk upendo wa kwel amna.hivyo m2 akiona mambo ayanyok kama alivyotegemea anaamua kusepa au kujivurugua.
vijana na wazee walio ktk ndoa wengi nanakunywa pombe na kukaa vijiweni kupoteza mawazo coz wanasema ukikaa nyumbani ni kero.
Uongo mbaya mie tangu nafunga ndoa (7years now) hata sijui mke wangu anapokea mshahara shs.ngapi (infact wote wife and I ni middle level public servant) na wala sijui huwa anazifanyia nini , na ndugu (kutoka upande wake na wangu) wapo kwa wingi sana hapa home na wanakuja na kuondoka anytime bila kugonga passport, cha muhimu wanachokikuta tunakula and wakilala sebuleni ni wao tu, ila marufuku kugusa room kwangu, anyway ninachotaka kusema ni kuwa maisha ni mpangilio wenu (couples) na wala si wa mawifi au mashemeji au wazazi, is how you set it na wanaokuzunguka wawaelewe
kwanza nakupa hongera kwa miaka saba ya ndoa.sasa hapo kwenye kutokutambua mshahara wa mkeo ni sh ngapi na unatumika vp naona kuna walakini kidogo coz umesema maisha ni mipango sasa mmepanga wewe na wife usijue mshahara wake au wewe ndio umepanga mwenyewe.na kama nyie ni wana ndoa hilo la kipato chake ww kwa nn usijue.Au wewe ni mmoja kati ya wale nanaopata shida bt wanavumilia tu.
nilimuao yeye wala si mshahara wake, mume ni kichwa cha nyumba...tunapanga kupitia income yangu na wala si ya wife, hakuna kulalama na wala sijalalama kama mleta thread
mkuu siku ukirudisha number kwa mola mkeo atapata shida sana,ndio kuanza kutafuta mwanaume mwingine wa kurovide...mshirikishe sasa hivi a-contribute kidogo kidogo aizoee pesa na financial renspossibilities.