Matapeli watumia mitandao ya kijamii kuwaibia watafutao ajira.

Matapeli watumia mitandao ya kijamii kuwaibia watafutao ajira.

kisugujira

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2012
Posts
774
Reaction score
200
WanaJF,

Ni lini tutaondokana na hali hii ngumu ya upatikanaji wa ajira? Kwa wale wasio na ajira kama mimi nawashauri kuwa makini sana na baadhi ya matangazo ya kazi yanayowekwa mitandaoni.

Kutokana na ugumu wa ajira, matapeli wameamua kutumia mwanya huo kwa kuweka matangazo feki ya kazi mitandaoni na kuwaibia wale wote wanaomba kazi hizo! Kuna tangazo la nafasi za kazi toka kampuni inayojiita HD CO Ltd liliwekwa katika mtandao wa zoomtanzania.com siku kadhaa zilizopita kwa lengo lililofanikiwa kwa kuwaibia walengwa.

Kuna mtu anayejiita HR DIRECTOR wa kampuni hiyo kwa jina la ERICK URASA aliweza kumwibia kila mtu aliyepata walaka wa elektroniki (email) unaomtaarifu kuwa anatakiwa kuhudhuria mafunzo ya kazi kama sehemu ya usaili kabla ya kuchaguliwa na kupangiwa sehemu ya kwenda na kuanza kazi.

Watu waliopata walaka au ujumbe huo walitakiwa kuchangia kiasi cha shilingi elfu kumi (10,000/-) kwa kutuma kwa njia ya MPESA namba +255764660443 na kupangiwa sehemu za kuhudhuria mafunzo hayo ya awali kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini. Kwa mfano hapa Dar ES salaam kuna watu walielekezwa kwenda TANZANITE EXECUTIVE SUITE lakini watu walipofika pale hakukuwa na mafunzo wala semina yoyote zaidi ya kuambiwa wametapeliwa!

Namba hiyo ya simu (+255764660443) ikipigwa haipatikani na imesajiliwa kwa jina la ERICK SAMSON URASA! Hawa watu ni hatari sana katika soko la ajira kama walivyo baadhi ya mawakala wa kazi toka nchi jirani wenye upendeleo na ubaguzi kwa wasiotoka nao sehemu moja na hivyo kuchochea uwakaji wa utambi wa bomu la ukosefu wa ajira na kusababisha siku moja likalipuka na kuleta madhara kwa Taifa.
 
Mjini hapa jamani lakini sio mbaya tunajifunza kutokana na makosa!!
 
Poleni sana na asante kwa taarifa, pia ni vizuri kuripoti Polisi.
 
poleni wote mliotapeliwa hizo elfu 10000. Ndo maisha utasimulia watoto wako
 
karipoti police coz iyo sim no yake itafatiliwa kwa humakini zaidi.
 
Mutuz Le Baharia at work Yo Yo alitahadharisha juu ya tapeli hili la kinataifa modes wakafinyanga uzi
 
Last edited by a moderator:
Dah poleni, ila haileti logic mtu anatafuta mfanyakazi halafu anamuomba na hela 10,000/= anyway na wanaolipa hela hizo ni kutokana na shiday ya ajira, naomba mungu siku moja magamba yaondoke madarakani nikiwa bado hai nishuhudie utawala mwingine utarekebishaje hili janga
 
kwel hilo si la kwanza mm ningeshauri wenye kuwapa nafasi au post katka job website wajilizishe km kweli mtu huyo anazo nafasi za kazi kama kuonesha ofisi, ID, na kama kasajiliwa na wakala wa usajiri, it is pain.
 
Back
Top Bottom