Maswali

Kichankuli

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2008
Posts
887
Reaction score
191
Swali langu linatokana na sehemu ya mchango wa Mwakyembe katika Bunge kama ilivyo hapo chini

Mheshimiwa Mwakyembe aliwasilisha hoja zake kama hivi:


"Wakili wa Serikali hana usafiri. Yeye na daladala, daladala na yeye. Mvua inyeshe, jua kali, akiwa na mafaili ya Serikali. Wakili wa Serikali tunamtegemea awe smart; suti nyeusi, kiatu cheusi, soksi nyeusi, shati jeupe na haliwezi kuwa moja tu, litaleta utando wa kutisha, kwa hiyo, mashati ya kutosha meupe, tai nyesi na tai maalum nyeupe. Lakini pesa tunayompa Wakili wa Serikali kununulia vitu hivyo, haitoshi hata kununulia robo ya vitu hivyo. Nafikiri kuna umuhimu sasa hivi kuongeza bajeti ya Wizara hii".

1) Ni mtumishi yupi wa Serikali ambaye ana sifa za kielimu kama za wakili wa Serikali ambaye hastahili kuwa na usafiri

2) Ni mtumishi yupi wa Serikali ambaye hastahili kuwa smart? je ni Mhasibu, Daktari, Nesi, Mwalimu, Afisa Mifugo na Kilimo, Afisa Mipango, Mchumi, Mhandisi, au Mhudumu, Katibu Muhtasi, Afisa Mtendaji wa Kijiji, Dereva au Mesenja?

3) Hao Askari waPolisi, JWTZ ambao wanapiga raia na Askari wenzao wa majeshi mengine kila kukicha ambao kwa mujibu wa taratibu zao wanatakiwa kukaa kwenye makambi na siyo kuchanganyikana na Raia hawajafanyiwa hivyo?

Wabunge wanatakiwa kujenga hoja ambazo zinalenga kuwapatia maslahi mazuri watumishi wote wa Serikali kulingana na sifa za kielimu na kiutendaji walizonazo bila kuwabagua kuwa hawa ni wa hazina, Ofisi ya Rais au usalama wa Taifa

http://www.parliament.go.tz/POLIS/PA...12-45-2008.pdf
 


Swali lako ni lipi hapa mkuu sijaelewa?
 
Swali lako ni lipi hapa mkuu sijaelewa?

Maswali yangu ni haya matatu

Ni mtumishi yupi wa Serikali ambaye ana sifa za kielimu kama za wakili wa Serikali ambaye hastahili kuwa na usafiri

2) Ni mtumishi yupi wa Serikali ambaye hastahili kuwa smart? je ni Mhasibu, Daktari, Nesi, Mwalimu, Afisa Mifugo na Kilimo, Afisa Mipango, Mchumi, Mhandisi, au Mhudumu, Katibu Muhtasi, Afisa Mtendaji wa Kijiji, Dereva au Mesenja?

3) Hao Askari waPolisi, JWTZ ambao wanapiga raia na Askari wenzao wa majeshi mengine kila kukicha ambao kwa mujibu wa taratibu zao wanatakiwa kukaa kwenye makambi na siyo kuchanganyikana na Raia hawajafanyiwa hivyo?

Samahani ile website ilitakiwa ije kabla ya maswali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…