Kuhusu swali la Mbunge wa Kwela, Dk. Chrisant Mzindakaya (CCM) ambaye alitaka kufahamu kwa nini kati ya visiwa vinne vya Comoro kimoja bado kiko chini ya Serikali ya Ufaransa, Pinda alisema hali hiyo inatokana na historia ya visiwa hivyo ambapo kwa sasa hakuna la kufanya zaidi ya kusubiri uamuzi wa wananchi wenyewe wa kisiwa hicho dhidi ya Ufaransa.