Maswali tunayoulizana kuhusu ukomo wa Waziri mkuu, Spika wa Bunge na uteuzi wa Mwanasheria mkuu

Magazetini

JF-Expert Member
Aug 16, 2014
588
1,698
Je, Kassim Majaliwa ni Waziri Mkuu? Jibu ni HAPANA
Waziri Mkuu, mawaziri na naibu mawaziri leo wamefikia kikomo cha uwaziri wao. Asubuhi ya leo waliamka wakiwa mawaziri, lakini kabla ya mchana wakawa si mawaziri tena. Kikatiba leo Baraza la Mawaziri limevunjika automatically. Si mawaziri tena. Uwaziri unakoma ukiwadia wakati wa Rais mteule kushika madaraka ya Rais, yaani kuapishwa. (Ibara 57(1)(f)). Kwa hiyo viti vyao viko wazi kuanzia leo.

Je, Job Ndugai ni Spika wa Bunge? Jibu ni NDIYO
Job Ndugai bado ni Spika wa Bunge ingawa bunge jingine halijaanza baada ya kuvunjwa kwa lile lililomaliza muda wake. Ingawa Majaliwa amekoma kuwa waziri, Ndugai bado anaendelea kuwa Spika wa Bunge pamoja na kwamba Bunge lilishavunjwa zaidi ya miezi minne iliyopita. Kwanini?

Kwa mujibu wa Katiba ya JMT, Ndugai anaendelea kuwa Spika wa Bunge hadi Bunge litakapokutana kwa mara ya kwanza baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanywa baada ya Bunge kuvunjwa (Ibara ya 84(7)(c)). Kwa hiyo Ndugai bado ni Spika hata baada ya Rais mteule kuapishwa.

Kwa maneno mengine, Ndugai atakoma kuwa Spika wa Bunge siku ile Bunge linakutana kwa mara ya kwanza baada ya kumalizika kwa uchaguzi Mkuu.

Leo Rais atamteua mshauri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano juu ya mambo ya sheria, na huyo atatajwa tu kwa kifupi kama "Mwanasheria Mkuu". Tutatajiwa jina. Kabla ya Novemba 19 tutakuwa tumeshatajiwa jina la Waziri Mkuu. Je, atakuwa ni Kassim Majaliwa? Jibu langu lolote kwa swali hili ni la kubahatisha.
 
Mi sijakuelewa

Katiba inasema ndani ya mda usozidi siku saba raisi atalitangaza jina la PM ambaye atatokana na wabunge wa kuchaguliwa ndani ya jamuhuri hii.

Sasa nadhani bunge lilipofunjwa tuu Majaliwa akawa sio PM tena ispokuwa aliendeleea kujinrojuzi kama PM kwavile sasa hivi muongozo hautokani na katiba tena bali ni fikra za mwenyekiti.
 
Mi sijakuelewa

Katiba inasema ndani ya mda usozidi siku saba raisi atalitangaza jina la PM ambaye atatokana na wabunge wa kuchaguliwa ndani ya jamuhuri hii.

Sasa nadhani bunge lilipofunjwa tuu Majaliwa akawa sio PM tena ispokuwa aliendeleea kujinrojuzi kama PM kwavile sasa hivi muongozo hautokani na katiba tena bali ni fikra za mwenyekiti.
Naomba provision kutoka kwenye katiba inayosema PM office inakuwa vacant pale bunge linapovunjwa?

Kwa sababu mtoa mada juu katupa provision inayoonyesha PM anakuwa madarakani hadi immediately president elect assume office,toa provision inayoenda contrary na Aritcle 57(2)(f) of the CURT
 
katiba yetu ni very contradicting eti huwezi kuwa spika, waziri, naibu waziri na waziri mkuu kama usipokuwa mbunge
halafu eti bunge linavunjwa wabunge wote wanakuwa sio wabunge eti halafu baadhi wanaendelea na vyeo vyao wakati sio wabunge
huu ni upumbavu uliopitiliza
 
katiba yetu ni very contradicting eti huwezi kuwa spika, waziri, naibu waziri na waziri mkuu kama usipokuwa mbunge
halafu eti bunge linavunjwa wabunge wote wanakuwa sio wabunge eti halafu baadhi wanaendelea na vyeo vyao wakati sio wabunge
huu ni upumbavu uliopitiliza
Kiukweli katiba yetu ina matundu mno
 
Back
Top Bottom