liljeff87
Senior Member
- Jan 3, 2016
- 174
- 85
MASWALI KUMI KWA PROF. KABUDI
Ameandika Dr. Farrell Jnr.
[HASHTAG]#Moja[/HASHTAG]
Unajuwa kuwa Prof. Kabudi ni waziri wa masuala ya bara na hana mamlaka yoyote visiwani. Yaani sheha wa shehia ya Tomondo anaweza kumnyima barua ya ukaazi na isiwe chochote. Hana haki ya kupiga kura zaidi ya yale ya muungano tu, na Wizara yake visiwani ina sehemu ndogo sana ya uwakilishaji kwa sababu ya uwepo wa katiba ya Zanzibar, Wizara ya Sheria ya Zanzibar, Mwanasheria Mkuu Zanzibar na Waziri wake anaeteuliwa na huyo anaemuota kuwa memba wa mawaziri Bara.
[HASHTAG]#Mbili[/HASHTAG]
Anaemuita Rais wa Zanzibar kuwa member tu wa Baraza la Mawaziri la Muungano, hakupigiwa kura hata moja na wananchi si Tanganyika wala Zanzibar lakini ana nguvu ya kuidogosha nafasi adhim ya Rais wa Zanzibar anaechaguliwa katika Uchaguzi Mkuu akibeba maslahi ya kikatiba yanayotambua uwepo wake, BLW na Mahakama Kuu Zanzibar. Kuna “motive” ipi ya kumdogosha mdau mmoja wa muungano na kumtukuza mwengine wakati tuna mfumo uliotukuza heshima za pande mbili tokea kuasisiwa kwake?
[HASHTAG]#Tatu[/HASHTAG].
Kama Rais wa Zanzibar ni memba wa Baraza la Mawaziri tu kwa tafsiri ya kuwa nae ni Waziri asie na wizara maalum basi atujulishe anateuliwa na nani katika nafasi hio kama alivyoteuliwa yeye na wote akiwamo makamo wa Rais anaemteua mwenyewe Rais akiwa kama mgombea mwenza wake? Jee kuna mwengine anaeingia pale kinyemela bila ya uteuzi wa huyo anaeitwa Jemedari Mkuu zaidi ya Rais wa Zanzibar?
[HASHTAG]#Nne[/HASHTAG]
Jee Rais wa Jamhuri anaeongoza vikao vya Baraza la Mawaziri nae anaingia pale akiwa kama nani? Waziri? Au Rais wa Jamhuri? Jee haiwezekani basi kuwa na Rais mwengine anaeingia katika Baraza la Mawaziri kwa sababu ya kofia yake ya Urais tena wa kuchagulia, akiwa na vyombo vyote vya heshima na mamlaka ya Urais ikiwamo katiba, vyombo vya kutunga sheria na mahakama?
[HASHTAG]#Tano[/HASHTAG]
Tuseme kuwamo kwa mwanasheria mkuu wa serikali katika Bunge kuna mhesabu nae kuwa mbunge asie na jimbo au anawakilisha mamlaka yake yanayomvyesha kofia ya kuwa sehemu ya Bunge? Bunge linaitambua nafasi ya Mwanasheria Mkuu kama nani bungeni? Jee Rais wa Zanzibar katika BLW anaingia kwa kofia ipi?
[HASHTAG]#Sita[/HASHTAG].
Kabla ya hapo Rais wa Zanzibar aliingia kama nani? Jee nae kwa vile ni Makamo wa Rais wakati ule hakuwa sehemu ya Baraza la Mawaziri kwa tafsiri ya kishabik ya Kabudi? Hauoni huu ubabaishaji na uhadaifu wa tafsiri holela ni sehemu ya kero zilizosimamiwa na kamati aliokuwa nae ni mjumbe ilioweka wazi ubabaishaji huu na kuja na formula ya serikali tatu? Basi anasahau kuwa Rais wa Zanzibar ana dhamana ya Umakamo Mwenyekiti wa Chama kinachoongoza nchi?
[HASHTAG]#Saba[/HASHTAG]
Unafaham huwa huyu huyu Profesa Kabudi ndie aliekuwa katika kamati ya Warioba iliochambua mashaka ya katiba ya Muungano na Zanzibar na kufika hadi wakaja na mfumo ambao hakuna yoyote hadi leo alieuikiuka wa serikali tatu huku ya muungano yakiwa machache tena ya pamoja.
[HASHTAG]#Nane[/HASHTAG]
Alilolisema hasa ya kuwa Rais wa Muungano ana haki ya kuingilia na kutoa amri kwa waziri wa SMZ haoni linakwenda kinyume na kauli ya aliemteua kuwa hana mamlaka ya kuingilia ya Zanzibar ikiwamo la Jecha kwa sababu hayamo katika kapu la muungano hasa kwa vile ndie Jemedari Mkuu wa Jamhuri.
[HASHTAG]#Tisa[/HASHTAG]
Jee kuna Waziri anabeba heshima sawa na Rais wa Zanzibar akiwa Zanzibar au Bara, akabeba mamlaka aliokuwa nayo, akachaguliwa kwa kura, akabeba ukuu wa nchi, heshima ya ulinzi kama mkuu wa nchi, katiba inayompa mamlaka ya kugawa mikoa na wilaya atakavyo, uwezo wa kuteua Mawaziri wengine, na protocol nzima ya kijeshi inayolinda heshima ya ukuu wake ikiwamo bendera ya mamlaka yake na ya utambulisho wa nafasi yake katika mamlaka yake?
[HASHTAG]#Kumi[/HASHTAG]
Jee wanakosea watu wanapowaita manyumbu maana muna kiongozi na safu yake, lakini akatokea mtu mmoja, mteule asie na jimbo wala asiejuwa uchungu wa kutafuta kura leo akasimama na matamshi holela likiwamo hili la muliesimama mukamfutia uchaguzi alieshindwa lakini basi tu abaki ili aje adhalilishwe kuwa na nafasi sawa na wateule wengine kama yule Shonza, au Mbarawa alieshindwa uchaguzi wa ubunge Pemba alikokuita vichochoroni na vijiwe i au Kabudi anaeona uteuzi wake ni sawa na nafasi adhim ya Rais wa Zanzibar na mamlaka yake kwa udhalili wa kiasi hiki?
Ameandika Dr. Farrell Jnr.
[HASHTAG]#Moja[/HASHTAG]
Unajuwa kuwa Prof. Kabudi ni waziri wa masuala ya bara na hana mamlaka yoyote visiwani. Yaani sheha wa shehia ya Tomondo anaweza kumnyima barua ya ukaazi na isiwe chochote. Hana haki ya kupiga kura zaidi ya yale ya muungano tu, na Wizara yake visiwani ina sehemu ndogo sana ya uwakilishaji kwa sababu ya uwepo wa katiba ya Zanzibar, Wizara ya Sheria ya Zanzibar, Mwanasheria Mkuu Zanzibar na Waziri wake anaeteuliwa na huyo anaemuota kuwa memba wa mawaziri Bara.
[HASHTAG]#Mbili[/HASHTAG]
Anaemuita Rais wa Zanzibar kuwa member tu wa Baraza la Mawaziri la Muungano, hakupigiwa kura hata moja na wananchi si Tanganyika wala Zanzibar lakini ana nguvu ya kuidogosha nafasi adhim ya Rais wa Zanzibar anaechaguliwa katika Uchaguzi Mkuu akibeba maslahi ya kikatiba yanayotambua uwepo wake, BLW na Mahakama Kuu Zanzibar. Kuna “motive” ipi ya kumdogosha mdau mmoja wa muungano na kumtukuza mwengine wakati tuna mfumo uliotukuza heshima za pande mbili tokea kuasisiwa kwake?
[HASHTAG]#Tatu[/HASHTAG].
Kama Rais wa Zanzibar ni memba wa Baraza la Mawaziri tu kwa tafsiri ya kuwa nae ni Waziri asie na wizara maalum basi atujulishe anateuliwa na nani katika nafasi hio kama alivyoteuliwa yeye na wote akiwamo makamo wa Rais anaemteua mwenyewe Rais akiwa kama mgombea mwenza wake? Jee kuna mwengine anaeingia pale kinyemela bila ya uteuzi wa huyo anaeitwa Jemedari Mkuu zaidi ya Rais wa Zanzibar?
[HASHTAG]#Nne[/HASHTAG]
Jee Rais wa Jamhuri anaeongoza vikao vya Baraza la Mawaziri nae anaingia pale akiwa kama nani? Waziri? Au Rais wa Jamhuri? Jee haiwezekani basi kuwa na Rais mwengine anaeingia katika Baraza la Mawaziri kwa sababu ya kofia yake ya Urais tena wa kuchagulia, akiwa na vyombo vyote vya heshima na mamlaka ya Urais ikiwamo katiba, vyombo vya kutunga sheria na mahakama?
[HASHTAG]#Tano[/HASHTAG]
Tuseme kuwamo kwa mwanasheria mkuu wa serikali katika Bunge kuna mhesabu nae kuwa mbunge asie na jimbo au anawakilisha mamlaka yake yanayomvyesha kofia ya kuwa sehemu ya Bunge? Bunge linaitambua nafasi ya Mwanasheria Mkuu kama nani bungeni? Jee Rais wa Zanzibar katika BLW anaingia kwa kofia ipi?
[HASHTAG]#Sita[/HASHTAG].
Kabla ya hapo Rais wa Zanzibar aliingia kama nani? Jee nae kwa vile ni Makamo wa Rais wakati ule hakuwa sehemu ya Baraza la Mawaziri kwa tafsiri ya kishabik ya Kabudi? Hauoni huu ubabaishaji na uhadaifu wa tafsiri holela ni sehemu ya kero zilizosimamiwa na kamati aliokuwa nae ni mjumbe ilioweka wazi ubabaishaji huu na kuja na formula ya serikali tatu? Basi anasahau kuwa Rais wa Zanzibar ana dhamana ya Umakamo Mwenyekiti wa Chama kinachoongoza nchi?
[HASHTAG]#Saba[/HASHTAG]
Unafaham huwa huyu huyu Profesa Kabudi ndie aliekuwa katika kamati ya Warioba iliochambua mashaka ya katiba ya Muungano na Zanzibar na kufika hadi wakaja na mfumo ambao hakuna yoyote hadi leo alieuikiuka wa serikali tatu huku ya muungano yakiwa machache tena ya pamoja.
[HASHTAG]#Nane[/HASHTAG]
Alilolisema hasa ya kuwa Rais wa Muungano ana haki ya kuingilia na kutoa amri kwa waziri wa SMZ haoni linakwenda kinyume na kauli ya aliemteua kuwa hana mamlaka ya kuingilia ya Zanzibar ikiwamo la Jecha kwa sababu hayamo katika kapu la muungano hasa kwa vile ndie Jemedari Mkuu wa Jamhuri.
[HASHTAG]#Tisa[/HASHTAG]
Jee kuna Waziri anabeba heshima sawa na Rais wa Zanzibar akiwa Zanzibar au Bara, akabeba mamlaka aliokuwa nayo, akachaguliwa kwa kura, akabeba ukuu wa nchi, heshima ya ulinzi kama mkuu wa nchi, katiba inayompa mamlaka ya kugawa mikoa na wilaya atakavyo, uwezo wa kuteua Mawaziri wengine, na protocol nzima ya kijeshi inayolinda heshima ya ukuu wake ikiwamo bendera ya mamlaka yake na ya utambulisho wa nafasi yake katika mamlaka yake?
[HASHTAG]#Kumi[/HASHTAG]
Jee wanakosea watu wanapowaita manyumbu maana muna kiongozi na safu yake, lakini akatokea mtu mmoja, mteule asie na jimbo wala asiejuwa uchungu wa kutafuta kura leo akasimama na matamshi holela likiwamo hili la muliesimama mukamfutia uchaguzi alieshindwa lakini basi tu abaki ili aje adhalilishwe kuwa na nafasi sawa na wateule wengine kama yule Shonza, au Mbarawa alieshindwa uchaguzi wa ubunge Pemba alikokuita vichochoroni na vijiwe i au Kabudi anaeona uteuzi wake ni sawa na nafasi adhim ya Rais wa Zanzibar na mamlaka yake kwa udhalili wa kiasi hiki?