Ni masoudMasoud Masoud ni nani?
Hivi huwa hastaafu tu ? Tangu 1994 yuko tu hadi leo ndani ajira TBC FMWanamwita manju wa muziki. Huyu ni mtangazaji mkongwe na nguli wa maswala ya muziki na wanamziki, kupitia TBC.
Ukimsikiliza Masoud, utaelewa umuhimu wa specialization katika utangazaji, uandaaji vipindi na uandishi habari kwa ujumla.
Masoud anaelewa ni nini anachofanya na kwa muktadha muafaka.
Ukifuatia simulizi zake kimuziki sio tu zina mizania ya kimantiki bali pia zina mtiririko kama movie fulani hivi inayokushawishi kuendelea kuitazama uone mwisho wake.
Masoud Masoud ni nani?
Uzi tayari
Bado anakomaa yuko vizuri.Hivi huwa hastaafu tu ? Tangu 1994 yuko tu hadi leo ndani ajira TBC FM
Ukiwaambia vijana wafanye specialization ya Music na kuwa proffessional hawataki na hawana Interest wao wanapenda kuchukuliwa na Upepo, ikija Amapiano twende, ikija nini twende, yani mwendo wa kutoa Copy tuu... Aliwa kusema huyu Manju wa Music ukiuliza sisi Mziki wetu ni upi wala hutapata jibu.. anaeleza Music wa Nchi ya Congo umepata hadhi na UNESCO kupewa hadhi ya Urithi wa Africa, sasa sisi sijui... Bongo fleva, Taarabu, Singeli, Mziki wa Dansi bado hakuna wa kuundeleza...Wanamwita manju wa muziki. Huyu ni mtangazaji mkongwe na nguli wa maswala ya muziki na wanamziki, kupitia TBC.
Ukimsikiliza Masoud, utaelewa umuhimu wa specialization katika utangazaji, uandaaji vipindi na uandishi habari kwa ujumla.
Masoud anaelewa ni nini anachofanya na kwa muktadha muafaka.
Ukifuatia simulizi zake kimuziki sio tu zina mizania ya kimantiki bali pia zina mtiririko kama movie fulani hivi inayokushawishi kuendelea kuitazama uone mwisho wake.
Masoud Masoud ni nani?
Uzi tayari
Huyu mwamba ametisha sana akuna wa kumkaribia hata chembe.
.Huyu mwamba ametisha sana akuna wa kumkaribia hata chembe.
Huyu Bwana kama angepata wadhamini au Serikali ikamsaidia kutekeleza Mawazo yake hasa tungeweza kuwa na pakuanzia, Wizara ya Utamaduni wangeona ni wapi huyu bwana anaweza kufiti na kuanzisha vionjo vya Music wa TanzaniaInatakiwa muelewe kitu Kimoja;
Kuna tofauti kubwa sana kati ya kusomea na kufanya kitu unachokipenda ata kama kina maslahi madogo wewe utakifanya tu na Kusomea kitu ambacho hukipendi
Masoud music kwake ni maisha na anaishi nao ndani ya moyo wake,ndiyo maana amekomaa sana pale TBC na hakuna mtangazaji ambae uwa napenda kumfuatilia pale TBC kama yeye ukimtoa Djaro Arungu
Watangazaji wa kileo wengi wao wapo kwenye media kwa ajili ya Maslahi yao binafsi na wanajihisi kuwa hawana deni la kufanya kwa Media
Mtu kama Baba levo,Mwijaku au Kitenge hawa sio watangazaji na ata ukifuatilia elimu zao zinatia shaka na wengine hawakusomea kabisa journalism ila ni vile tu wamejikuta ndani ya media kwa sababu ya ugumu wa maisha mtaani