ndege JOHN
JF-Expert Member
- Aug 5, 2015
- 24,804
- 60,650
Napoishi Mimi Nina jirani yangu mmoja Ni maskini tu Kama mimi anaishi maisha ya kuunga unga Sana kapanga chumba kimoja na ana mke na watoto wawili.sasa huyu jamaa ana hasira Sana,nadhani ipo siku atakuja kuua mke au mtoto.juzi niliamka asubuhi nikakuta anampiga mwanae wa kiume kisa alipoteza hela shilingi 1000.sasa kweli imagine unampiga mtoto wa darasa la tano fimbo Kama 20 na mazoezi ya kijeshi push-ups.mambo hayo nakumbuka Ni vijijini tu ndo mtu ukipoteza hela unachezea kichapo.jana mchana saa Saba akawa anampiga mke wake kampiga Sana ngumi.akawa anamwambia mke wake "unasema Mimi nakubaka una akili wewe".akampiga Sana na libao mke wake naye anaonekana Ana kiburi badala akimbie ye ametulia tu anamwambia mumewe nitakupeleka polisi mbona ulivonitongoza hukuwa hivi ulikuwa unanipa maneno matamu.jamaa akawa haelewi anamchezeshea tu Tena mbele ya watoto anamwambia nitakubaka kweli na polisi nakusindikiza.akampiga sana akamchania hadi nguo akawa anamwambia mke wake kwanini kuna meseji anatumiwa na wanaume wengine.mimi hapo nikawa nachungulia tu kwa mbali nashuhudia yote huruma ilinishika lakini nikaona nitulie Sina la kufanya.leo nimekutana na huyu jamaa asubuhi akawa anajifanya ananilalamikia kuwa arsenal jana kamchania mkeka alikuwa ale laki mbili na sabini.me nikawa hata Sina hamu ya Kuongea naye nikikumbuka alivyompiga mkewe na mtoto nikaona sio rafiki mwema nikamwambia ndo hivo Bhana ipo siku utakula tu Kaka usijali akawa anajichekesha chekesha.akiwa na sisi kijiweni anaonekana Ana cheka Ana furaha lakini kumbe akiwa nyumbani Ni Simba.kweli nyumba zinaficha mengi hasa nyumba za masikini.kwa matajiri wao familia zao naona Zina amani watoto wanacheza Hawana wasiwasi hawamuogopi baba.