Maskini UKAWA ni mungu tu atakaewaokoa

Maskini UKAWA ni mungu tu atakaewaokoa

vevenononombo

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2015
Posts
1,289
Reaction score
421
Nimekuwa mfuatiliaji wa siasa za Tanzania zaidi ya miaka 30 iliyopita,kiukweli hakuna wakati ambapo kama Taifa tumekutana na changamoto za kiutawala na hamasa za kisiasa kama wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu,na nitofautiane kabisa na wale wanaolinganisha wakati wa mrema (1995) na wakati huu wa lowasa(2015) tofauti kubwa ni kuwa mwaka 1995 mrema aliibuka lkn hakuwa na nguzo na mtandao wa kiitikadi kwa watu,tofauti na wakati huu ambapo kuna watu wanaishi ktk imani za vyama vyao,lkn pia 1995 ulikuwa ni muda mchache tu taifa lilikuwa limeingia ktk mfumo wa vyama vingi takribani miaka 3 lkn upinzani wa sasa una umri wa zaid ya miaka 23,lkn pia sasa wapinzani wakubwa wa serikali.iliyoko madarakani wameungana(ukawa) hii ni turufu kubwa sana ktk mabadiliko ya siasa za Tanzania.Pamoja na yote hayo "NAISIKITIKIA UKAWA"Maskini Ukawa ni mungu tu atakaewaokoa!" Kwa nini nasikitikia ukawa
1,Mgombea wa Ccm anapata nafasi yakuitumia serikali na idara zake kupanga mipango mbali mbali yakufanikisha uchaguzi mkuu hii ni faida kubwa sana kwa ccm ktk kufanya lolote hata kama watu watapiga kura kwa upinzani
2,Viongozi wa kiserikali kama wakuu wa mkoa na wilaya kama viongozi wa ulinzi na usalama wanakaa vikao na timu za ushindi za ccm na kujadili amri gani itolewe kwa wananchi lkn isiyokuwa na athari kwa chama tawala hivyo chochote anachokuja nacho mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa kimepata baraka za ccm hii ni bao lingine la mkono kwa Ukawa
3,Vyombo vya ulinzi na usalama hasa viongozi wakuu wamepata kukutana mara kadhaa na chama tawala na kuamua chakufanya hivyo nao chochote wanachosema ktk jamii mrengwa mkubwa ni upinzani
4,Mgombea wa urais kupitia ccm kwa sasa anafulsa ya kuwapigia simu za moja kwa moja watu wote muhim ktk uchaguzi huu na wakatii
NB.ukawa isipojizatiti ktk eneo la ujasusi ktk kila hatua wanatofanya na namna nambo yanavyokwenda Hakina Lowassa ataisikilizia ikulu redion na Ccm itashinda Saa 5 asubuhi ndio maana Naonyesha masikitiko yangu "Maskini ukawa ni mungu tu atakaewaokoa"
 
Kwa bahati nzuri umekiri mwenyewe kuwa ni Mungu pekee mwenye uwezo wa kuipa ushindi Ukawa.

Nakubaliana nawe kwa asilimia 100 kuwa analolitaka Mola wetu, hakuna binadamu mwenye uwezo wa kulizuia.

Naamini hata katika uchaguzi wa mwaka huu Mungu atakwenda kutenda miujiza ya aina ya kwenye maandiko ya kwenye biblia namna 'mnyonge' Daudi alivyoliangamiza 'dubwasha' Goliath kwa kombeo.

Katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu naweza kuwalinganisha Ukawa na Daudi na CCM kama Goliath.

Hebu tusubirie matokeo ya mpambano huo wa karne kati ya 'Mayweather' na 'Manpaciao' hapo Oktoba 25 mwaka huu.
 
Sasa unakuta mtu anajivunia uchaguzi usio wa haki na kujiita mshindi kwa sababu ya KATIBA ISIYO FAIR KWA VYAMA VYOTE. Aibu nyingine hii. CCM imekomaa ilitakiwa iikubali uchaguzi wa FREE AND FAIR ELECTION
 
TULIANZA NA MUNGU NA TUTAMALIZA NA MUNGU.


swissme
 
Ukawa lazima waingie ikulu huo ndio mpango wa mungu
askofu kakobe aliwaeleza ccm mapema mwaka jana.
 
Hata wafilisti, wapagani wana mungu wao....kakobe, gwajima ambao wanaenda kinyume na utii wa mamlaka iliyotajwa ktk biblia ya kikristo nao wanamfuata mungu yupi?
 
Back
Top Bottom