Maskini, Maiko Wambura!

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
21,883
18,299
Ni muda mrefu sasa Michael Wambura amekuwa akivutana na uongozi wa Simba kwenye issue ya uchaguzi wa viongozi ktk klabu hiyo. Hii ni mara ya pili Wambura anawekewa pingamizi baada ya kufanikiwa kuchomoa lile pingamizi alilowekewa mara ya kwanza. Nasikia kuna wanachama wamepeleka issue hii kunako CAS, na kuna hatari ya uchaguzi wa wa Klabu ya Simba kusimamishwa hadi kitendawili hiki kitakapoteguliwa.

Mtakumbuka kwamba mivutano kama hii imeanza kumuandama Michael tangu akiwa FAT (sasa TFF). Mimi sio mfuatiliaji mzuri wa mpira wa nyumbani Tanzania lakini namuomba Bw Maiko aachane na mambo ya mpira. Ndio. Kitumbua chake kwenye mpira kimeishaingia mchanga. Namshauri atafute kazi nyingine ya kufanya badala ya kung'ang'ania kwenye mpira tu miaka yote. Kwani yeye aliandikiwa kwamba riziki yake ipo kwenye mpira tu?

Bw Maiko achana na biashara kichaa hiyo, haina tija kwako. Muda unaoupoteza ni bora ukautumia kujiajiri kwenye sekta nyingine ya kiuchumi. Hii sekta ya mpira imeishaingia shubiri.

Nawasilisha.
 
Simba sio sehemu ya ku-recycle viongozi! akatafute pa kujaribia uongozi..Ana uchu wa madaraka tu
 
Ni muda mrefu sasa Michael Wambura amekuwa akivutana na uongozi wa simba kwenye issue ya uchaguzi kwa muda mrefu sasa. Hii ni mara ya pili Wambura anawekewa pingamizi baada ya kufanikiwa kuchomea lile pingamizi alilowekewa mara ya kwanza. Nasikia kuna wanachama wamepeleka issue hii kunako CAS, na kuna hatari ya uchaguzi wa wa Klabu ya Simba kusimamishwa hadi kitendawili hiki kitakapoteguliwa.

Mtakumbuka kwamba mivutano kama hii imeanza kumuandama Michael tangu akiwa FAT (sasa TFF). Mimi sio mfuatiliaji mzuri wa mpira wa nyumbani Tanzania lakini namuomba Bw Maiko aachane na mambo ya mpira. Ndio. Kitumbua chake kwenye mpira kimeishaingia mchanga. Namshauri atafute kazi nyingine ya kufanya badala ya kung'ang'ania kwenye mpira tu miaka yote. Kwani yeye aliandikiwa kwamba riziki yake ipo kwenye mpira tu?

Bw Maiko achana na biashara kichaa hiyo, haina tija kwako. Muda unaoupoteza ni bora ukautumia kujiajiri kwenye sekta nyingine ya kiuchumi. Hii sekta ya mpira imeishaingia shubiri.

Nawasilisha.

Ungekuwa enzi za Mandela ungemshauri Mandela aachane na harakati za ukombozi? Changamoto anazopata wambura ni za kawaida sana kuliko wanazopata wanasiasa.waulize majimboni katika kutafuta ubunge
 
Tunajua mbinu zenu mwisho wa kutegea Simba iwatajirishe umefika, mtachonga sana Wambura mbele kwa mbele, eti ooo tunasajiri kimataifa timu yenu? Si mkasaji Lipuli huko,
 
Ni muda mrefu sasa Michael Wambura amekuwa akivutana na uongozi wa simba kwenye issue ya uchaguzi kwa muda mrefu sasa. Hii ni mara ya pili Wambura anawekewa pingamizi baada ya kufanikiwa kuchomea lile pingamizi alilowekewa mara ya kwanza. Nasikia kuna wanachama wamepeleka issue hii kunako CAS, na kuna hatari ya uchaguzi wa wa Klabu ya Simba kusimamishwa hadi kitendawili hiki kitakapoteguliwa.

Mtakumbuka kwamba mivutano kama hii imeanza kumuandama Michael tangu akiwa FAT (sasa TFF). Mimi sio mfuatiliaji mzuri wa mpira wa nyumbani Tanzania lakini namuomba Bw Maiko aachane na mambo ya mpira. Ndio. Kitumbua chake kwenye mpira kimeishaingia mchanga. Namshauri atafute kazi nyingine ya kufanya badala ya kung'ang'ania kwenye mpira tu miaka yote. Kwani yeye aliandikiwa kwamba riziki yake ipo kwenye mpira tu?

Bw Maiko achana na biashara kichaa hiyo, haina tija kwako. Muda unaoupoteza ni bora ukautumia kujiajiri kwenye sekta nyingine ya kiuchumi. Hii sekta ya mpira imeishaingia shubiri.

Nawasilisha.

watakuja wenyewe kuwasuluhisha, mbona Malinzi alikoma na wakasuluhishwa uchaguzi ukafanyika na akapita? Mshikaji waka mico atashindwaje?
 
Tunajua mbinu zenu mwisho wa kutegea Simba iwatajirishe umefika, mtachonga sana Wambura mbele kwa mbele, eti ooo tunasajiri kimataifa timu yenu? Si mkasaji Lipuli huko,

Nahisi umetumwa wewe, mbona wakati wasajili hamjawahi kuwakataa hao wachezaji ndo kwanza mnawashangilia. WANAFIKI WAKUBWA NYIE.
 
Ungekuwa enzi za Mandela ungemshauri Mandela aachane na harakati za ukombozi? Changamoto anazopata wambura ni za kawaida sana kuliko wanazopata wanasiasa.waulize majimboni katika kutafuta ubunge

hii issue haifanani na ubunge. ukishaukwaa ubunge, iwe kwa halali au haramu, hakuna mwananchi wa kukupindua hadi umalize kipindi chako cha miaka 5. sasa kama wambura akiforce akachukua uongozi simba (ijapokuwa hili jambo haliwezekani sasa) atakaa madarakani siku ngapi kabla ya kupinduliwa? mkuu, hebu soma kwanza alama za nyakati.
 
Tunajua mbinu zenu mwisho wa kutegea Simba iwatajirishe umefika, mtachonga sana Wambura mbele kwa mbele, eti ooo tunasajiri kimataifa timu yenu? Si mkasaji Lipuli huko,

mkuu, mimi sina maslahi yoyote simba ila nimetoa tu ushauri wangu kwa JEMBE Maiko Wambura. sasa nyie wanachama mnaomsapoti huku mkijua kwamba anawekewa mizengwe na watu wenye pesa mtafanyaje kama asipopitishwa kugombea au ikiwa akipitishwa na akaangushwa kwenye uchaguzi na vigogo wa Simba?
 
Mapinduzi mpaka yabarikiwe na TFF ndo utang'oka ,mbona MADENI YA MAHARAGE kapinduliwa mara kibao na vikao alivyoita vya harusi na hakung'oka
hii issue haifanani na ubunge. ukishaukwaa ubunge, iwe kwa halali au haramu, hakuna mwananchi wa kukupindua hadi umalize kipindi chako cha miaka 5. sasa kama wambura akiforce akachukua uongozi simba (ijapokuwa hili jambo haliwezekani sasa) atakaa madarakani siku ngapi kabla ya kupinduliwa? mkuu, hebu soma kwanza alama za nyakati.
 
By Ndakilawe
Simba sio sehemu ya ku-recycle viongozi! akatafute pa kujaribia uongozi..Ana uchu wa madaraka tu


we nae unaasili ya india???
Au umeajiriwa na hao watu?
Mtatumiwa sana na wahindi,walioigeuza simba kitega uchumi

Haya ya India na Wahindi yametoka wapi? Kwani Mkuu Ndakilawe alitaja Wahindi? Kumbe ndani ya washabiki wa Wambura kuna wenye mawazo ya kibaguzi kiasi hicho?
 
Ni muda mrefu sasa Michael Wambura amekuwa akivutana na uongozi wa Simba kwenye issue ya uchaguzi wa viongozi ktk klabu hiyo. Hii ni mara ya pili Wambura anawekewa pingamizi baada ya kufanikiwa kuchomoa lile pingamizi alilowekewa mara ya kwanza. Nasikia kuna wanachama wamepeleka issue hii kunako CAS, na kuna hatari ya uchaguzi wa wa Klabu ya Simba kusimamishwa hadi kitendawili hiki kitakapoteguliwa.

Mtakumbuka kwamba mivutano kama hii imeanza kumuandama Michael tangu akiwa FAT (sasa TFF). Mimi sio mfuatiliaji mzuri wa mpira wa nyumbani Tanzania lakini namuomba Bw Maiko aachane na mambo ya mpira. Ndio. Kitumbua chake kwenye mpira kimeishaingia mchanga. Namshauri atafute kazi nyingine ya kufanya badala ya kung'ang'ania kwenye mpira tu miaka yote. Kwani yeye aliandikiwa kwamba riziki yake ipo kwenye mpira tu?

Bw Maiko achana na biashara kichaa hiyo, haina tija kwako. Muda unaoupoteza ni bora ukautumia kujiajiri kwenye sekta nyingine ya kiuchumi. Hii sekta ya mpira imeishaingia shubiri.

Nawasilisha.

hakijaingia mchanga wambura mbele kwa mbele simba oyeeeee
 
Nahisi umetumwa wewe, mbona wakati wasajili hamjawahi kuwakataa hao wachezaji ndo kwanza mnawashangilia. WANAFIKI WAKUBWA NYIE.

Ninashangaa sana watu wanasema eti FOS waondoke Simba ijitegee.Hawaelezi watapata wapi za kuendeshea klabu kipindi cha mwanzo .
 
Keshatupwa nje ya kinyang'anyiro
Source: Radio One

bora ametupwa. ngoja sasa aende akajikite kwenye shughuli zingine za uzalishaji mali. usikate tamaa jembe wambura, maisha hayapo kwenye soka tu--maisha ni popote.
 
[h=3]RUFANI YA RICHARD MICHAEL WAMBURA YAKWAMA TFF[/h]


Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imeikataa rufani ya Michael Richard Wambura (pichani) kupinga kuenguliwa kugombea urais katika uchaguzi wa klabu ya Simba unaotarajiwa kufanyika baadaye mwezi huu.






Wambura aliwasilisha rufani yake mbele ya Kamati hiyo iliyokutana leo (Juni 19 mwaka huu) jijini Dar es Salaam chini ya Kaimu Mwenyekiti Wakili Mwita Waissaka kupinga uamuzi wa kumwengua katika kinyang'anyiro hicho uliofanywa na Kamati ya Uchaguzi ya Simba kwa kufanya kampeni kabla ya muda uliopangwa.




Baada ya kupitia vielelezo, kanuni na sheria, Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF imeridhika kuwa mrufani (Michael Wambura) alifanya kampeni kabla ya muda kinyume na Ibara ya 6(1)(a) na (g), Ibara ya 6(1)(l) pamoja na Ibara ya 14(3) ya Kanuni za Uchaguzi za TFF toleo la 2013.




Kwa mujibu wa ibara hizo, Kamati ya Uchaguzi ya Simba inayo mamlaka ya kumwengua (disqualify) mgombea anayefanya kampeni ama kukiuka maagizo halali ya Kamati ya Uchaguzi.




Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF imeziagiza kamati zote za uchaguzi za wanachama wa TFF kufuata kanuni za uchaguzi kama zilivyoainishwa katika Katiba zao ili kuepusha rufani za mara kwa mara.






Uamuzi wa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF umezingatia Katiba ya TFF pamoja na kanuni zake, na pia Katiba ya Simba.

Hakimiliki; 1999 ; 2014 Google
 
Back
Top Bottom