Karishia Mbarikiwa
Member
- Aug 1, 2017
- 7
- 5
Hapana sio busha mkuu. Naiman utakua unazifahamu hizo honi na kiwango cha kelele zake. Otherwise utakua unatania tuu mzee wa kisovieti.mzee na anabusha tu huyu ishu sio gari ni kitenesi
eti hadi alimnunulia maji!! alijuaje kama maji ndio dawa ya mshtuko wake wa honi?mzee na anabusha tu huyu ishu sio gari ni kitenesi
Hizo horn ni kero hata kama upo ndani ya hilo basi maana unaweza hisi wamefunga horn zingine ndani ya basi.Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu, ni namna magari almaarufu kama EICHER yanayofanya kazi katika viunga mbalimbali vya maeneo ya mijini na vijiji. Imekua kero kubwa kutokana na kelele za honi zao ambazo ni kero kutokana na kelele zake pale tuu inavyopigwa.
Nitoe mfano wa hivi majuzi nlikiwa maeneo ya posta mpya hapa mjini Dsm ilitokea basi moja ya aina ya EICHER ilipiga honi nkiwa nimesimama pembeni na mzee wa makamo ilitushtua sana. Mzee yule alishtuka mpaka kupelekea kukaa chini huku mapigo ya moyo yakimwenda mbio sana. Ilinibidi kumnunulia maji ili mwili kukaa sawa. Na hii sio mara ya kwanza kwa madereva wa magari hayo pindi tuu wanapokua wakiingia kwenye vituo vya mabasi hupiga honi hizo pasipo kua na ulazima wowote ile.
Rai yangu ni kwa mamlaka husika kuchukua hatua stahiki juu ya wamiliki wa vyombo hvyo kuangalia nmna nyingine ya kubadilisha honi hzo na kuweka zitakazo kua za kistaarabu au ikiwezekana ziwekwe honi za kawaida ambazo hazitapelekea watu kushtuka ama sivyo zinaweza kuleta madhara makubwa maana watu wengi wanamagonjwa ambayo hayaitaji kelele za kiasi kile. Nawasilisha.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hana dalili yoyote ya SOVIET huyu ni Kada Teleza wa CCMHapana sio busha mkuu. Naiman utakua unazifahamu hizo honi na kiwango cha kelele zake. Otherwise utakua unatania tuu mzee wa kisovieti.
Sent using Jamii Forums mobile app
Serikali imeshafanya kila kitu, kama sheria zipo, kama kanuni zipo, kama mamlaka za kushughulikia zipo. kilichobaki ni mimi na wewe kuchukua hatua tu, inapoonekana kero ya sound pollution waathirika wanaanzia serikali za mtaa na kupanda juu. shida inakuwa kwenye ushirikiano na muda utakaopotea ikiwa pollution sio jambo la kudumu.Sound Pollution ni mojawapo ya vipengele ktk uharibifu mazingira
Kuna hizo honi za Eicher, kuna wauza CD, kuna wapiga debe, kuna wauza mitumba.
Serikali inabidi ifanye kitu kwenye hili hamna katazo lolote hususan kuhusu suala la sound Pollution kuna jamaa mmoja siku moja alikuwa na furaha zake basi alichukua baiskeli mithili ya Gutta amejaza speakers na mziki mkubwa toka kariakoo shule ya uhuru mpaka mtaa wa libya amefungulia sauti ya mwisho kabisa. Alivyofika libya st akaingia chaga st. hapo akapata vijana kama watano omba omba wakaanza kucheza. Hebu angalia hii kero ya furaha ya mtu 1 inavyosumbua watu wengi
Nakumbuka ktk miaka ya 1980s ndege za Tz na Zambia zilishawahi pigwa marufuku kupita ktk anga la London 7bu ya sound Pollution.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ma-engineer wa hayo magari inaonekana somo la acoustics hawalipi uzito. Pia kuna taa fulani za magari, bajaj, hadi boadaboda ukipigwa usiku ni full kiza! Huoni kabisa na bodaboda wanazipenda hasa. Huwa najiuliza TBS wako wapi? Wanaruhusu vipi products za aina hiyo zinaingia nchini?Nafikiri zile honi hazina viwango vya ubora..wahindi wamefeli sana