Masikini tunalindwa sana na Mungu

Masikini tunalindwa sana na Mungu

kula yangu ni ya shida sana...tokea mwaka umeanza nimeandamwa na majanga yaliyo nizidi uwezo, sina furaha, mwili unadhohofika kwa njaa, mawazo kila saa...huu uzi mpaka nahisi unanihusu mim...kwa kweli naelekea kukata tamaa..

Shida ni hiyo jina unayotumia
 
kwa bahati mbaya hujakaa vijijini ila unasikiliza hadithi za vijiweni, usiombe yakukute
kijiji gani ulichokulia wewe kitaje kwanza ?? isije ikawa sehemu zenye ukame na kwa Tanzania sehemu zenye ukame ni chache sana usilete habar ya kijinga
 
Trump anasema miili ya wafrika ni sebule ya magonjwa. Ukitaka kujua kwamba vijijini watu wanakufa sana ingawa watu wachache wanaugua magonjwa yasiyoambukizwa kuliko mjini. Itisha sensa ya wazee zaidi ya miaka 70 kijijini kwako kama watafika robo ya wakaazi.
 
hakuna kitu kama hicho cha mlo mmoja mnapeana habar za uongo watu wa kijijini wanaongoza kwa kula chakula bora elewa hivyo

Ushawahi kukaa kijijini?

Achana na stori za mitandaoni na vijiweni.

Kwanza asilimia kubwa ya maisha ya kijijini asubuhi hakuna kifungua kinywa, asilimia kubwa kuanzia saa sita/saba ndio watu wanapata mlo hadi saa mbili usiku baada ya hapo ni kesho tena mchana.........familia chache ndio zinapata uji mkavu asubuhi......Maisha ya kijiji yasikie tu......wewe hujiulizi kwanini watu wengi wakitoka bush kuja town ndio wananawiri.

Kama huwa mnaenda kutembea tu vijijini mnachinjiwa kuku msione ndio maisha ya kila siku.

 
Kweli tupu Baba 2Pac.

Yaani siyo kwa Chakula tu, angalia hata Nyumba zetu.

Yaani utakuta Nyumba kama vile inauliza nianguke au nisianguke? Lakini utakuta mvua hata saba zinapita salama.

Yaani ni jambo la kumsifu na kumshukuru Mungu wetu.

Tazama Maji tunayokunywa vijijini, hadi unaona kabisa unakunywa uchafu lakini Mungu analinda huugui.

Mungu ni mwema .
 
kijiji gani hicho unakula mara moja kwa siku? labda upareni. vijiji vyakula viko vingi waweza kula hata mara 4 kwa siku?
Hahahahah mkuu unaugomvi na kina mshana Jr
Hahaaaha
 
Watu wote wanalindwa na Mungu, Hakuna anayelindwa na pesa,jeshi au sijui nn
Mtu muovu halindwi na Mungu mkuu,unless mtu huyo Mungu ana mpango na yeye.It's only by chance that an evil man survives.Maisha ya uovu ni maisha ya kutisha sana.
 
kula yangu ni ya shida sana...tokea mwaka umeanza nimeandamwa na majanga yaliyo nizidi uwezo, sina furaha, mwili unadhohofika kwa njaa, mawazo kila saa...huu uzi mpaka nahisi unanihusu mim...kwa kweli naelekea kukata tamaa..
Usikate tamaa mkuu.There is a God out there who cares for you.

Jambo la kwanza la kufanya katika mazingira uliyopo ni kumpa Bwana Yesu maisha yako, kwa kuwa inawezekana hizo ni laana za ukoo au huo ni uonevu wa Shetani.Baada ya hapo,labda unahitaji kubadili mazingira.Kama unaishi mjini hama rudi kijijini, halafu badili mtizamo wako wa maisha,change your mindset,maisha sio ajira tu.Kama ulikuwa una amini katika ajira futa hayo mawazo na anza kujenga maisha yako from another angle,labda kwa kilimo au biashara ndogo ndogo,kutokana na hela za kuazima kutoka kwa ndugu,marafiki nk.Naamini kwa kuwa utakuwa umemwamini Kristo,Mungu atafungua milango ya fedha.Jambo la msingi katika mazingira uliyo nayo ni kuridhika na kidogo utakachokuwa unapata wakati unajenga maisha yako pole pole.Kumbuka kuweka akiba ya utakachokuwa unapata na kutumia fedha vizuri.Ukiheshimu fedha itakuheshimu.Wakati unajenga maisha yako through
biashara ndogo ndogo au kilimo, si vibaya pia kutafuta ajira.Wakati huu inaweza kuwa rahisi kwa kuwa milango imefunguliwa na Kristo mwenyewe.Ajira nyingi siku hizi ziko kwenye mtandao, kwa hiyo huhitaji kutembea from office to office kuomba kazi au kupeleka barua,labda kwenye interview tu.

Kila la heri ndugu yangu.Mungu akuhariki na akusaidie.
 
Ushawahi kukaa kijijini?

Achana na stori za mitandaoni na vijiweni.

Kwanza asilimia kubwa ya maisha ya kijijini asubuhi hakuna kifungua kinywa, asilimia kubwa kuanzia saa sita/saba ndio watu wanapata mlo hadi saa mbili usiku baada ya hapo ni kesho tena mchana.........familia chache ndio zinapata uji mkavu asubuhi......Maisha ya kijiji yasikie tu......wewe hujiulizi kwanini watu wengi wakitoka bush kuja town ndio wananawiri.

Kama huwa mnaenda kutembea tu vijijini mnachinjiwa kuku msione ndio maisha ya kila siku.

Huu ndio uhalisia kweli kweli, nasapoti kwakuwa nimeyapitia.
 
kula yangu ni ya shida sana...tokea mwaka umeanza nimeandamwa na majanga yaliyo nizidi uwezo, sina furaha, mwili unadhohofika kwa njaa, mawazo kila saa...huu uzi mpaka nahisi unanihusu mim...kwa kweli naelekea kukata tamaa..
Usimkufuru Mungu ya bando umepata wapi mpaka ukakoment? Mwenye afya dhoofu anapata na muda wa kukoment?
 
Back
Top Bottom