Mashindano ya Pool World Cup

Motowntzjpm

Senior Member
Jun 16, 2023
118
191
Usiku wa Kuamkia leo kulikuwa na Mashindano ya Pool World Cup. Watanzania wangapi tulijuwa hayo. Mashindano yalifanyika Spain. Fainali Philipines dhidi ya Ujerumani. wafilipino waliibuka washindi 11-7.

Nimeuliza wangapi walifahamu na lilikuwa live DSTV channel 225.

Tusibiri tuone Kitenge Sports wakitujuza.

Kwa Taifa linalojitutumua na kupenda michezo ni dhahiri tunapenda Simba na Yanga tu

Hayo mengine hatuna habari nazo. Sasa nauliza millioni 61 lakini hatumo kwenye hockey, volleyball, riadha, basketball, table lawn tennis hata Pool jamani ambacho kila bar ina pool table
 
Nakumbuka miaka ya nyuma kuna wana wao walikuwa kama wamejiajili kwenye mchezo wa pool table ila wao waliufanya kikamari zaidi,kuna wana walikuwa wanatembea mabaa tofauti tofauti na walikuwa hatari, ukiweka nao kidau kama haupo vizuri atazila hela zako sana.
 
Usiku wa Kuamkia leo kulikuwa na Mashindano ya Pool World Cup. Watanzania wangapi tulijuwa hayo. Mashindano yalifanyika Spain. Fainali Philipines dhidi ya Ujerumani. wafilipino waliibuka washindi 11-7.

Nimeuliza wangapi walifahamu na lilikuwa live DSTV channel 225.

Tusibiri tuone Kitenge Sports wakitujuza.

Kwa Taifa linalojitutumua na kupenda michezo ni dhahiri tunapenda Simba na Yanga tu

Hayo mengine hatuna habari nazo. Sasa nauliza millioni 61 lakini hatumo kwenye hockey, volleyball, riadha, basketball, table lawn tennis hata Pool jamani ambacho kila bar ina pool table
Daaaah!!!! Nilikuwa live na nilienjoy sana fainali Ujerumani walikuwa tayari wamesha shinda fainali tatu za huko miaka ya nyuma na hata game ilivyoanza walikuwa wanajiamini sana mpaka score board ikawa inasoma 2-2 baada ya hapo kilichofuata ni msiba wafilpino wale walifanya comeback ya hataree mpka score board ikabadilika ujerumani2-ufilpino9 wafilpino wakaja kujichanganya wajerumani wakarudi mchezoni na ubao kusomeka 7-9 wajerumani wakiwa na munkari ya kuchukua game mkononi mtu akala kete afu akjificha na kushindwa kuitafutia kiwango kilichofuata hapo ni mchezo wa fitna tu wafilpino nao wakaificha kete wajerumani walivyokuja kuitafuta wakacheza kete ambayo haikuwa mchezoni na wafilpino kupata advantage ya kuweka kete nyeupe popote watakapo hii iliperekea mechi kuisha 9-11
NB: pooltable ni mchezo wa fitna tu hasa huu wa nine balls mjerumani hakuamini macho yake๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
 
Jitahidini tu......! Jadilini jadilini iyo pool table Labda wengine wanaweza kuijua. Pia Anzisheni Sredi nyingi nyingi kuhusu pool table, huwezi jua Watu wakaanza kufuatilia
 
Jamachk na wadau wote lengo la bandiko hili lilikuwa kuhoji sio kejeli dhidi ya wasiokuwa na DSTV ilikuwa kuhoji vyombo vyetu vya habari kwamba iweje kila wakitujuza sasa ni muda wa habari za michezo , habari zenyewe ni Simba am Yanga. Mpira wa Miguu tu. Tuna milioni 61 mbona magazeti na vituo visihamasishe michezo mingine ili uchu wetu wa kujimwambafai kuwa taifa kubwa litimie kwenye Olimpiki na Kombe la dunia mbali mbali
 
Back
Top Bottom