Masharti kuelekea December 9

Masharti kuelekea December 9

The Burning Spear

JF-Expert Member
Joined
Dec 23, 2011
Posts
8,551
Reaction score
20,346
MASHARTI 10 KWA SERIKALI BATILI, HARAMU NA KATILI YA SAMIA KABLA YA TAREHE 09/12/2025
1. Serikali ikabidhi miili ya wapendwa wetu ili tuwazike kishujaa. Mwili usipotezwe wala kuchomwa moto Wazo Hills au kuzikwa kwenye makaburi ya siri kama mnavyofanya sasa hivi.

2. Serikali itumie kodi ya Wananchi (Pesa zetu) na iwape familia husika ili kugharamia mazishi ya wapendwa wetu.

3. Walioumizwa na majangili waliotumwa na serikali batili na haramu watibiwe bure na wapewe matibabu mazuri bila kusumbuliwa.

4. Waliohusika na mauaji ndani ya Tanganyika wakamatwe wote haraka na waoneshwe mubashara kwenye Tv na mbele ya waandishi wa habari wa kimataifa wakitajwa majina na walipotokea.

5. Waliohusika kwenye mchakato mzima wa kupanga mauaji ya raia wasio na hatia wajulikane wote kwa majina yao.

6. Mkuu wa Majeshi (CDF), IGP na Mkurugenzi wa usalama taifa wote wajiuzulu nafasi zao kwa kushindwa kuwajibika kwa kulinda nchi na wananchi jambo ambalo ndio waliapa kufanya. Hii pia iwahusishe wote walioshiriki katika njama za kuteka na kuua raia. Majina yao mnayo na sisi tunayo.

7. Watanganyika wote waliotekwa na kupotezwa warudishwe wakiwa hai.

8. Watanganyika wote waliopewa kesi feki za Uhaini na Ugaidi(kesi za kubuni/kutengeneza) kwa nia ovu waachiwe haraka sana bila masharti yoyote na waliohusika kubuni au kutunga kesi hizo au kushiriki kwa namna yoyote wakamatwe mara moja.

9. Uchafuzi feki na batili iliyofanyika ifutwe mara moja na Samia aachie ngazi haraka maana hatambuliki kama rais kwa mujibu wa katiba ya Tanzania. Hakuchaguliwa bal amejiteua, Katiba haina rais wa kujiteua.

10. Bunge feki ya sasa ivunjwe na Serikali ya mpito iundwe chini ya usimamizi wa UN hatimaye mchakato wa Katiba mpya ianze mara 1.

NB: Tunajua huwa mnadharau maoni ya Umma kama kawaida yenu huku mkishirikiana na viongozi wa kidini hao waliokosa uhalali, vyombo vya habari zilizokosa maadili, watu tuliowapa umaharufu pamoja na kikundi cha wachache wanaotafuna nchi yaani wanamtandao. Taifa hili ni letu sote sio mali ya kikundi au familia. Yasipozingatiwa tarehe 09/12/2025 tutaanza maandamano yasiyo na kikomo kudai haki na uhuru wa Tanganyika.

Imetolewa na waratibu wa Maandamano Kitaifa kutoka kila mkoa wa Tanzania.

1762590393650.png
 
Maandamano yasiambatane na vitendo vya uhalifu. Kama vile uharibifu wa mali,wizi na uporaji. Bebeni mabango yenye jumbe za kila mnachotaka kifanyike.
Watanganyika wengi wako nyuma yenu, wasichounga mkono ni fujo sizizo za lazima. Epukeni mamluki wenye nia ovu. Nawatakia maandamano mema.
 
Maandamano yasiambatane na vitendo vya uhalifu. Kama vile uharibifu wa mali,wizi na uporaji. Bebeni mabango yenye jumbe za kila mnachotaka kifanyike.
Watanganyika wengi wako nyuma yenu, wasichounga mkono ni fujo sizizo za lazima. Epukeni mamluki wenye nia ovu. Nawatakia maandamano mema.
Father Inategemea police watakavyo tupokea. Watakavyokuja ndivyo watakavyopokelewa.
 
Maandamano yasiambatane na vitendo vya uhalifu. Kama vile uharibifu wa mali,wizi na uporaji. Bebeni mabango yenye jumbe za kila mnachotaka kifanyike.
Watanganyika wengi wako nyuma yenu, wasichounga mkono ni fujo sizizo za lazima. Epukeni mamluki wenye nia ovu. Nawatakia maandamano mema.
Mali za kifisadi za Kikwete,Rostam na machawa ziharibiwe tu hazina faida kwa nchi

Mwendo Kasi imejengwa kwa Kodi zetu halafu Ridhiwani ndiye mwendeshaji na waarabu.

Huu upuuzi lazima ukome tuheshimiane

Mali za mafisadi na machawa Tia moto
 
Kwenye hayo maandamano ya kuelekea Dec 9 2025 Watanganyika ni muhimu iwepo kamati ya kujitolea (volunteers) itakayochangisha pesa kuanzia sasa pesa zitakazo tumika
kununua na kutoa mahitaji ya kibinadamu. Kama maji,vitafunio vya kupunguza njaa na wawepo watu wakutoa msaada wa kiafya wa dharura.
 
Maandamano yasiambatane na vitendo vya uhalifu. Kama vile uharibifu wa mali,wizi na uporaji. Bebeni mabango yenye jumbe za kila mnachotaka kifanyike.
Watanganyika wengi wako nyuma yenu, wasichounga mkono ni fujo sizizo za lazima. Epukeni mamluki wenye nia ovu. Nawatakia maandamano mema.

Kudai roho za marehemu na. Kulipa kisasi utabeba bango gani nyumbu wee
 
Maandamano yasiambatane na vitendo vya uhalifu. Kama vile uharibifu wa mali,wizi na uporaji. Bebeni mabango yenye jumbe za kila mnachotaka kifanyike.
Watanganyika wengi wako nyuma yenu, wasichounga mkono ni fujo sizizo za lazima. Epukeni mamluki wenye nia ovu. Nawatakia maandamano mema.
Mtanzania ni mstaarabu sana
Wameongea kwa Kila namna ,Kila namna unayoijua wewe namaanisha Kila namna.
 
Mimi nadhani tufanye maandamano ya amani lakini tuwe tumejiandaa kwa scernario zote. Wakituletea fujo na sisi tunaanzisha.
Jamani tusiogope. Tukionyesha uoga basi jua kuwa tumekwisha . Ulimsikia raisi haramu anasema hata mataifa ya nje yasitupangie kitu cha kufanya. Huyu raisi haramu anakiburi sana
 
Mimi nadhani tufanye maandamano ya amani lakini tuwe tumejiandaa kwa scernario zote. Wakituletea fujo na sisi tunaanzisha.
huezi shindana na serikali, na pia mda wa uchaguzi ushaisha watu wafocus na kujipatia utajiri sasa
 
huezi shindana na serikali, na pia mda wa uchaguzi ushaisha watu wafocus na kujipatia utajiri sasa
Kwa hiyo unataka kusema tuendelee tu kukubali watu wanatekwa, wana nyimwa haki zao, katiba iliyopo iendelee, tume iendelee etc
 
Kwa hiyo unataka kusema tuendelee tu kukubali watu wanatekwa, wana nyimwa haki zao, katiba iliyopo iendelee, tume iendelee etc
Nyerere, Mandela, Mugabe et al. wangekuwa na fikra kama zako hadi leo tungekuwa tunatawaliwa na wakoloni.
 
Kwa hiyo unataka kusema tuendelee tu kukubali watu wanatekwa, wana nyimwa haki zao, katiba iliyopo iendelee, tume iendelee etc
ukisema watu wametekwa unatakiwa kua na ushahidi ametekwa na nani ama kikundi gan,

2) katiba imekuzuia wap kufanya shuhuli zako kama mwananchi?

3) haki unaoitafuta apa ni ipi ambayo hauna?
 
Back
Top Bottom