Marufuku kuokota embe hapa!!

Marufuku kuokota embe hapa!!

Joined
May 8, 2012
Posts
29
Reaction score
4
Mtoto mmoja alikuwa akiokota embe kwenye shamba la miembe la Mzee-Kijana. Mara yule Mzee-Kijana naye ghafla akaja kuliangalia shamba lake na kumkuta yule Mtoto akiokota embe kwenye shamba lake. Mzee-Kijana akamwambia yule Mtoto; leo iwe mwanzo na mwisho wa kuokota embe kwenye shamba langu. Yule Mtoto akajibu; sawa Mzee nimekuelewa. Baada ya siku 3 yule Mtoto akaenda tena kwenye shamba la miembe la yule Mzee-Kijana ili kula embe; lakini safari hii yule Mtoto aliamua kupanda juu kwenye mwembe ili akale embe akiwa juu. Mara na Mzee-Kijana akaja kwenye shamba lake kama kawaida na akamkuta yule Mtoto aliyemkataza asiokote embe kwenye shamba lake; tena safari hii akiwa juu ya mwembe. Akamwuliza; we Mtoto, hivi unakumbuka kwamba nilikuambia iwe mwanzo na mwisho kuokota embe kwenye shamba langu? Mtoto akajibu, ni kweli Mzee; lakini kumbuka kwamba ulinikataza KUOKOTA EMBE na sio KUCHUMA EMBE; sasa mimi leo SIOKOTI ila NACHUMA na ndio maana nikaamua kupanda juu ili NISIOKOTE EMBE zako ila NICHUME tu.
 
Back
Top Bottom