Marriage is a sacrifice


Mimi nadhani umekurupuka maana hii mada imeongelea changamoto za kwenye Ndoa na sio kwenye Uchumba. Haijagusa kugongewa mchumba. Kuna mwanaume Amelia hapo kwamba kuna demu kamkataa. Nahisi bado hujaelewa kiini cha changamoto tunazozungumzia. Karibu Chai
 


Ni muendelezo wa mada zile zile tu za Wanaume kulia lia, mambo kama hayo hujadili Wanawake, lkn Mwanaume kuanza kujadili na kuuliza watu mwanamke gani uoe inaonyesha jinsi usivyojiamini.

Kama unajiamini na unajua unataka nini unatafuta demu anayekufaa unaoa, kwisha!
 
Sio ndoa tu ndo sacrifice.
Bali kuingia katika biashara ni sacrifice.
Kumaliza chuo ukaingia mtaani ni sacrifice.
Kila unachofanya lazima ujitoe muhanga kwa uhakika.

Sijui nani alikuja kutudanganya kwamba ndoa ni kitu rahisi na cha mchezo mchezo kisichohitaji utayari uvumilivu na uelewa.

Tuna tatizo la kuona ndoa ni ngumu na ya kujitoa muhanga ila hatuna tatizo la kuona kwamba biashara nayo ni ngumu kweli kweli tena ni kujitoa muhanga.

Tuache biashara,tuache ndoa
 
siku hizi naona kumekuwa na mabandiko mengi sana ya ku-discourage maisha ya NDOA.

ila ukweli maisha ya ndoa sio kitu cha mchezo mchezo. it's a lifetime commitment.

i have been there, saw it and experienced it. sishauri kijana wa jinsia yoyote kuingia ktk mfumo huo wa maisha.

you better stay alone.
 
Kweli kabisa.
Ndoa huwa jambo la kheri sana kwa binadamu na mbele ya Mungu.

Mnapofunga ndoa, tayari mmetangaza bifu na shetani. Na hili bifu huwa ni unstoppable.

Maisha yenu yakiwa ya kumtanguliza Mungu kwa kila jambo mnaweza kuwa salama kabisa. Ila ikitokea upenyo wowote, shetani huutumia ili kuwavuruga.
Angalia Mch. alivyomchoma visu visivyo na idadi mkewe baada ya kugundua amemsaliti.
Shetani hapandi ndoa. Pindi mnapofunga ndoa mmemkaribisha shetani. Kitakachowaokoa kila jambo mnalofanya mshirikisheni Mungu
 
Wako kimya kwa kuwa wao ndiyo walioongea live na shetani. Huwezi jua waliongea nini kuhusu mwanaume.
Mwanaume alifika analishwa tu matango pori bila kujua agano la mwanamke na shetani.
 
Kaka ndoa Hapana.....wakwangu nimekaa nae kwa miaka mitano tunasomana lakini nikajilipua kufunga ndoa.....lakini tulivofika nyumbani siku hiyohiyo tukae hoi binitaabani nikamuomba dr nitadikie kitanda nipumzike kidogo alinijibu wewe huna mikono au yeye ana mikono minne.....duh nilichoka hiyo siku nilijiona kwamba nimenaswa kwenye mtegoni
 
Wako kimya kwa kuwa wao ndiyo walioongea live na shetani. Huwezi jua waliongea nini kuhusu mwanaume.
Mwanaume alifika analishwa tu matango pori bila kujua agano la mwanamke na shetani.


Mwanaume real humuongoza Mwanamke, na Mwanamke humtambua real man na kumfwata!
 
Hawa ndio wakina barbaverosa
 
Kwahyo mwanaume haruhusiwi kujadili, akijadili tu kwa akili yako ushamfananisha na shoga yako. Sio Poa
 
Siku moja moja muwe mnatupa thread za furaha na utamu wa ndoa ili vijana wasiwe na stress kuhusu ndoa, kuwajenga katika misingi bora ya kuishi na kufurahia ndoa. Tuwajenge kisaikolojia wawe na mitazamo chanya kuhusu ndoa.

Kila kitu kina changamoto, na changamoto ni maisha. Hatupaswi kuzikimbia changamoto
 
asante kwa kutupa "ilim" muhimu kabisa....maana mambo sio mambo!
 
Mmmh!!!! I am afraidoooooo.... "Binafsi nilijiwekea kuoa mwenye elimu mwenzangu nikijua we shall be thinking kwenye direction moja na it will be easy kueleweshana, this has been one of the biggest mistakes in my life"
 
Uzi wako mkuu kama nimekuelewa vzr sana na hii hutokea sana Kwenye mahusiano mengi.....

Kile unachokidhania Wewe ni sahihi, na ukataka kufanya kwa kuamini kuwa ni sahihi na kwa kuwa unaamini ni sahihi basi unakomalia, pasi kutarajia mwenzio anaona Hakuna usahihi wowote katika jambo Lako, nae anazo sababu anazoziona ni sahihi kuliona jambo Lako sio sahihi....

Sasa hapo ndipo usipokuwepo kitu Inaitwa Sucrifies... NI MOTO FIRE NDANI ya nyumba..

Kumbe basi miongoni mwa Elimu muhimu sana za watu kabla hawajajitosa Kwenye ndoa wanazotakiwa kupata elimu hii ya SUCRIFIES(KUJITOA) kikamilifu.

Asante sana kwa Elimu mkuu
 
Wanawake wengi hawatumii jf na hawaijui kabisa.....wangelilia fb au IG ila kule hamna privacy......wao husimuliana saluni
 
Hebu tusimulie...umeona nn huko
 
Wengi tumesahau majukumu yetu mwanamke amuheshimu mume wake, na mume ampende mke wake, hasa wanawake tunajisahau sana Mungu hatusaidie jamani
 
Una sacriface uhai wako furaha yako mda, pesa kwaajili ya lijitu ambalo halijitambui kabisa unateseka nusu ya uhai wako eti unalinda ndoa....whats ndoa??? hell with your ndoa nahitaji uhuru wangu bana......nilikosea sitarudia tena God forbid
 
Forever sio
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…