Marketing strategy E-fm vs Clouds fm

mayowela

JF-Expert Member
Nov 2, 2014
2,124
1,746
Natumai tuko salama, nimeona nigusie hili suala kwa kuwa mi napenda maendeleo ya hivi vituo na ninapenda ubunifu.mimi sio mzuri sana wala sina ujuzi kwenye masoko pia kwenye media masscom (mawasiliano ya umma) siyafahamu ila napenda kufuatilia hivo vitu.

Clouds fm ni kituo cha muda mrefu na nikituo kinachoaminiwa sana na makampuni, mashirika ya serikari hata binafsi kwa kuteka vijana, na imeaminika na ndivyo ilivo kuwa biashara yako ili isikike kwenye masikio ya watanzania wengi ni vizuri upeleke tangazo lako Clouds, hiyo ina maanisha idara ya masoko na mauzo iko vizuri na ina ubunifu wa kutosha ili kuuza brand yao.

Lakini Clouds imekuwa ikifanya matamasha na udhamini mbalili mbali ili kujitangaza na kujipanua yaani kufikia wasikilizaji wake moja kwa moja hiyo ni nzuri.

Kwa upande wa Efm haina muda mrefu sana ila imejichukulia umaarufu sana kupitia matamasha kama komaa concert, saka saka, shika ndinga, nk na misemo yao kama ni kwikwi, Idara yao ya masoko pia iko vizuri kwa kubuni maudhui yanayomteka msikilizaji wa kawaida japo ilikuwa sehemu mmoja ila kwa sasa inajitanua kwa kasi.

(Marketing strategy) mbinu za kimasoko ni kama zinafanana ila hazifanani hata kidogo E-fm amekuja na vitu vipya ambavyo Clouds alikuwa hajasanuka navyo na alihisi havihitajiki kwa mlaji wake (msikilizaji) kama Singeli.. Clouds aliona anaenda kupoteza wasikilizaji wa Dar es salaam na pwani yote akacopy na kuiba mtangazaji wa E-fm (kicheko) japo alipokuwa kule alikuwa bora sana kuliko alipo sasa hii yaweza sabababishwa na kipindi anachofanya na muda kilipo.
Lakini pia E-fm akaja na Mida ya Kubet, vipindi vya michezo kufanyika ne hasa maeneo ya bar zinazoonesha mpira, Clouds akaona naachwa sasa nayeye akaanza na Kijiwe soka japo sijui kimefia wapi.hiin yote nikutafuta milage
E-fm alianza na kurusha vipindi nje ya studio alipata wasikilizaji sana na ilipendeza sana ila Clouds ni kama aliproove failure ikabidi abuni kitu kingine.
E-fm amekuja na vitasa day amabayo hufanyika kama leo sabasaba hupigwa mziki kutwa nzima hii naona Clouds hajaona kama inahamasa kwake.
E-fm kaja na shika ndika, wese day ambapo hugawa mafuta kwa wasikilizaji wenye boda boda na bajaji, pia joging club ambayo kwa sasa iko kule Mwanza mkoa mpya kimatangazo

Huu ni ubunifu mzuri kwa redio zote na zimeleta chahcu ya umsikilize nani na uzime wapi pia hii huvuta makampuni kudhamini vipindi mbali mbali ili yaweze kuuza bidhaa zao. Ila pia redio zingine nazo zijitahidi naona zinazidi kupotea tu na ukongwe wao ubunifu zero.
 
Idara ya masoko kazini..Ni kweli usemavyo mkuu E-fm imempa changamoto sana Clouds
na invozidi kujitanua kwa sasa ndio inazidi kumpa changamoto na itaendelea kumpa changamoto, yote hiyo nikugawana wasikilizaji na wadhamini
 
Efm wamejipanga vizuri

- Wanagharamika sana kiuwekezaji kuliko CLOUDS

- Wanagharamika sana kwenye kujitangaza

- Ni wabunifu

UDHAIFU

- Wapunguze kujichomeka chomeka kwenye BEEF za kijinga na WATU/WASANII bila sababu za msingi

- Wajiepushe na tabia kama za CLOUDS kwamba ukishakuwa na BEEF na kiongozi/mmiliki wa KAMPUNI basi unakuwa huelewani na KAMPUNI nzima. Ingawa hili naona na wao wamekuwa kama CLOUDS tu. Watangazaji wote kutumia muda mwingi kurusha vijembe kwa mtu kina KIONGOZI wenu ana BEEF naye

Anyway, So Good So far !
 
Efm wamejipanga vizuri

- Wanagharamika sana kiuwekezaji kuliko CLOUDS

- Wanagharamika sana kwenye kujitangaza

- Ni wabunifu

UDHAIFU

- Wapunguze kujichomeka chomeka kwenye BEEF za kijinga na WATU/WASANII bila sababu za msingi

- Wajiepushe na tabia kama za CLOUDS kwamba ukishakuwa na BEEF na kiongozi/mmiliki wa KAMPUNI basi unakuwa huelewani na KAMPUNI nzima. Ingawa hili naona na wao wamekuwa kama CLOUDS tu. Watangazaji wote kutumia muda mwingi kurusha vijembe kwa mtu kina KIONGOZI wenu ana BEEF naye

Anyway, So Good So far !

nadhani sio Udhaifu tuseme Zingatio itapendeza zaidi
 
viongozi wa clouds ni kama magu tu akikuchukia sharti team nzima ikuchukie
 
Wabongo walivyo na wivu wakaamua kimchafua mmliki wa E-fm kwa kumtaja kwenye ordha yao ya watuhumiwa wa madawa yao.
 
Wabongo walivyo na wivu wakaamua kimchafua mmliki wa E-fm kwa kumtaja kwenye ordha yao ya watuhumiwa wa madawa yao.
Kuwa huru kifikra Mkuu. Kuwa makini sana maana hata huyo jamaa akiua hadharani, akikamatwa basi itaonekana ameonewa

- Mara nyingi watu wenye ushawishi mkubwa kwenye jamii ni kama miungu hawakosei hata kama WATAUA MTU HADHARANI
 
Kuwa huru kifikra Mkuu. Kuwa makini sana maana hata huyo jamaa akiua hadharani, akikamatwa basi itaonekana ameonewa

- Mara nyingi watu wenye ushawishi mkubwa kwenye jamii ni kama miungu hawakosei hata kama WATAUA MTU HADHARANI

Mkui kwani fikra zangu zimefungwa?

Tunasema ilikuwa wanachafuana maana walitaja majina ya watu mbele ya kamera za waandishi wa habari na kusema wanajihusisha na madawa ila hadi leo wapo mtaani maisha yanaendelea.
 
Clouds anaisoma namba haswa .....E-fm wamesaidia kuondoa baadhi ya upupu wa Clouds waliokuwa wanawamwagia vijana, na kuwafanya vijana kujikuna mchana kutwa na usiku kucha. E-fm heko, lakini msibweteke na pongezi hizi.
 
  • Thanks
Reactions: dtj
Honger efm hongera sports headquarter kipindi bora cha michezo kwasasa Tanzania.

East Africa Radio hebu zindukeni basiii ,Mzee Mengi hebu mtoe mwanao tafuta meneja kijana wa mujini aichangamshe hiyo radio na tv, maana kila siku wafanyakazi wanakimbia .

Tunataka mpambano wa haki kati ya clouds ,efm na ea radia
 
Muda naenda kazini asubuhi ndio ninasikiliza redio. Sina muda mwingine zaidi ya morning kusikiliza redio.

So far, Clouds is my first choice for now.
 
Back
Top Bottom