Maridhiano ya kweli - uwajibikaji kwanza

Maridhiano ya kweli - uwajibikaji kwanza

M SELENHO

New Member
Joined
Jul 27, 2026
Posts
2
Reaction score
0
Maridhiano ya kweli yalipaswa kufanyika kabla ya uchaguzi wa kiini macho wa Oktoba 2025. Lakini kwa sababu walikaza fuvu, walitawala kimabavu baada ya kuua, kuteka na kubambikia raia kesi za uongo, sasa maridhiano yenye dhamira njema lazima yaanze na uwajibikaji kwanza.

1. Uchunguzi huru (pigia mstari huru) na wa kweli wa mauaji "MO29", majeraha na utekaji (Humphrey Polepole na wengine) ufanyike mara moja. Tume ya serikali peke yake haitoshi na haina uhalali. Wanaohusika, iwe polisi, majeshi au viongozi wa serikali, washtakiwe, wahukumiwe na wapewe adhabu ya haki.

2. Viongozi wa upinzani na wananchi wengine walioko jela kwa kesi za uhaini zisizo na msingi thabiti waachiliwe au wahukumiwe kwa haki waziwazi mahakamani. Kesi za kisiasa hazipaswi kuendelea kutumika kama silaha ya kutisha na kunyamazisha watu.

3. Mazungumzo ya kitaifa yaanze tu baada ya hatua za uwajibikaji, si kabla. Yahusishe CCM, CHADEMA, waathirika wa mauaji na utekaji, kubambikiwa kesi na vurugu, viongozi wa dini, asasi za kiraia na jamii kwa ujumla.

4. Katiba mpya iandaliwe kwa ushirikishwaji wa wote, ikifuatiwa na uchaguzi huru na wa haki chini ya tume huru kabisa kabla ya 2028.

Bila haki, adhabu kwa wahalifu na uwajibikaji wa kweli, maridhiano ni maneno matupu tu. Amani endelevu inatokana na uwajibikaji, si kujisahaulisha au kuficha ukweli.
 
Maridhiano ya kweli yalipaswa kufanyika kabla ya uchaguzi wa kiini macho wa Oktoba 2025. Lakini kwa sababu walikaza fuvu, walitawala kimabavu baada ya kuua, kuteka na kubambikia raia kesi za uongo, sasa maridhiano yenye dhamira njema lazima yaanze na uwajibikaji kwanza.

1. Uchunguzi huru (pigia mstari huru) na wa kweli wa mauaji "MO29", majeraha na utekaji (Humphrey Polepole na wengine) ufanyike mara moja. Tume ya serikali peke yake haitoshi na haina uhalali. Wanaohusika, iwe polisi, majeshi au viongozi wa serikali, washtakiwe, wahukumiwe na wapewe adhabu ya haki.

2. Viongozi wa upinzani na wananchi wengine walioko jela kwa kesi za uhaini zisizo na msingi thabiti waachiliwe au wahukumiwe kwa haki waziwazi mahakamani. Kesi za kisiasa hazipaswi kuendelea kutumika kama silaha ya kutisha na kunyamazisha watu.

3. Mazungumzo ya kitaifa yaanze tu baada ya hatua za uwajibikaji, si kabla. Yahusishe CCM, CHADEMA, waathirika wa mauaji na utekaji, kubambikiwa kesi na vurugu, viongozi wa dini, asasi za kiraia na jamii kwa ujumla.

4. Katiba mpya iandaliwe kwa ushirikishwaji wa wote, ikifuatiwa na uchaguzi huru na wa haki chini ya tume huru kabisa kabla ya 2028.

Bila haki, adhabu kwa wahalifu na uwajibikaji wa kweli, maridhiano ni maneno matupu tu. Amani endelevu inatokana na uwajibikaji, si kujisahaulisha au kuficha ukweli.
Gentleman,
hakuna haja ya personal glorification kwenye maridhiano ya hiyari miongoni mwa waTanzania wote.

porojo, upotoshaji, uongo, uzushi na hekaya za kutafuta kiki na public sympathy hazina maana yoyote kwenye kutafuta utakatifu fake, hasa tunapoelekea kwenye maridhiano ya kitaifa ambayo yataweka na kujenga msingi wa kuelekea mchakato wa katiba mpya kama sehemu ya utekelezaji wa vipaumbele vya wananchi vilivyo ainishwa kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM 2025-2030🐒
 
Gentleman,
hakuna haja ya personal glorification kwenye maridhiano ya hiyari miongoni mwa waTanzania wote.

porojo, upotoshaji, uongo, uzushi na hekaya za kutafuta kiki na public sympathy hazina maana yoyote kwenye kutafuta utakatifu fake, hasa tunapoelekea kwenye maridhiano ya kitaifa ambayo yataweka na kujenga msingi wa kuelekea mchakato wa katiba mpya kama sehemu ya utekelezaji wa vipaumbele vya wananchi vilivyo ainishwa kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM 2025-2030🐒
Sasa unaleta ilani ya CCM 2025-2030 kama msingi wa maridhiano? Ilani ya chama kilichopata “ushindi” baada ya kuua, kuteka na kufunga wapinzani? Hiyo ilani haina uzito wowote kimaadili wala kisheria kwa sababu serikali inayotaka kuitekeleza imepoteza uhalali mbele ya wananchi wake wenyewe na mbele ya dunia. Maridhiano ya kweli hayawezi kujengwa juu ya damu na uongo. Yanaanza na uchunguzi huru (si tume ya serikali peke yake), mashtaka kwa wahalifu (polisi, majeshi, viongozi), kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa, na kisha mazungumzo. Bila hiyo, “maridhiano” yako ni maneno matupu ya kujaribu kujisahaulisha na kuficha ukweli.
Ukipenda ukweli, usilete ilani ya chama kilichokaza fuvu. Lete uwajibikaji. Amani endelevu inatokana na haki, si propaganda.
 
Back
Top Bottom