Kuna tofauti kati ya walimu(shuleni) na wakufunzi(vyuoni) we umeambiwa wameletwa walimu kufundisha mashuleni maana yake ni kwamba hawana sifa ya kuwafundisha walimu tarajali vyuoni au kwa vile ni wamarekani ndo maana umeona wakafundishe vyuoni?Ni jambo zuri kupata uzoefu. Ningeshauri walimu hawa wangepelekwa kwenye vyuo vinavyofundisha kozi za science ili kuwapa walimu wetu watarajiwa mafunzo ya science ili watakapoondoka baada ya miaka miwili watazalisha waalimu wengi wazoefu na kusambaa nchi nzima. Wanafunzi wengi watafaidika hata baada ya walimu hawa kurudi kwao marekani.
Sawa mkuu nimekuelewaKuna tofauti kati ya walimu(shuleni) na wakufunzi(vyuoni) we umeambiwa wameletwa walimu kufundisha mashuleni maana yake ni kwamba hawana sifa ya kuwafundisha walimu tarajali vyuoni au kwa vile ni wamarekani ndo maana umeona wakafundishe vyuoni?

Hakuna watakachosaidia ni sawa na kupeleka polisi wawili kila mkoa halafu unasema umepunguza ujambazi.Embu wawe serious kidogo, walimu 51 watasaidia vp kwa mikoa 22 ukipiga hesabu ya haraka 22*2=44 na kubaki waalim 7 kwa maana hiyo kila mkoa utakua na waalim 2, kwel itasaidia kupunguza tatizo la waalimu wa sayansi? na isitoshe hao waalimu wawil wanakaa kwa mda wa miaka miwili. Tujiulize ni waalimu wangapi wa sayansi ambao wamemaliza hawajaajiriwa hadi leo , achana na hawa waliomaliza mwaka huu . Kama kwel wana nia ya dhati serikali yenyewe ya Tz iangalie hawa waalim waliomaliza vyuo ili wawapatie ajira. Na pia hata waalim wa arts kuna maeneo bado wanahitajika saana sio kwamba hawahitajiki . Embu serikali iliangalie hili kwa jicho la tatu.