Marekani yaifungua iPhone ya Mlipuaji

Marekani yaifungua iPhone ya Mlipuaji

kcamp

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2014
Posts
8,526
Reaction score
8,029
Wizara ya Sheria ya Marekani inasema
imefanikiwa kuzisoma data zilizohifadhiwa
kwenye Simu ya iPhone mali ya mmoja wa
walipuaji katika tukio la mauaji la San
Bernardino na kutangaza kuacha mpango wake
wa kisheria dhidi ya Kampuni ya Apple.
Wakili wa Marekani Eileen Decker alisema kuna
mtu aliisaidia idara hiyo kuifungua Simu hiyo ya
iPhone bila kuathiri data zilizohifadhiwa.
Kampuni ya Apple ilikataa kusaidia uchunguzi ,
kwa kusema ni kuweka ' historia mbaya.
Simu hiyo ni mali ya Rizwan Farook ambaye,
pamoja na mke wake, waliuua watu kumi na
wanne kusini mwa California Desemba mwaka
jana.

#mod huu uzi sijui kwanini mmeutoa asubuhi


d92969eeeed0fa51a0aaa1ddc4f105b4.jpg
 
Hivi hiyo simu ilikua inatakiwa kufunguliwa PASSCODE au ICLOUD LOCK?

Namaanisha je ilikua inawaka ila inataka password ili kuitumia au ilikua imejilock icloud na inataka Apple id?
 
Back
Top Bottom